
Uongozi wa kwanza ambao hatuna budi tuhakikishe kuwa unatokana na raia wenyewe ni uongozi wa T.A.N.U. Kila mmoja wetu aliye katika hali ya uongozi – toka President mpaka Chairman wa Kijiji – Toka Secretary General mpaka Secretary wa Kijiji – hana budi ajiulize: Ikiwa nilichaguliwa kwa kura, hizo kura nilizipataje? Nilizipata kwa hila, kwa rushwa, kwa vitisho au kwa ujanja wa aina yoyote, au nilizipata kwa hiari ya wapiga kura wenyewe?
(Baba wa Taifa Mwl. J.K. Nyerere)

“Chama imara ni kile ambacho viungo vyake vimekamilika na vinafanya kazi vizuri. Chama ni Wanachama, Viongozi, Vikao, Watendaji, Rasilimali na Jumuiya za Chama”
J.M. Kikwete
Mwenyekiti wa CCM
Chimwanga, Dodoma 25.6.2006
|