Jarida la CCM Habari Mpya Historia ya TANU na ASP Kutoka Magazetini Hotuba

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

JARIDA LA MKEREKETWA

Toleo la Tano

Toleo la Nne

Toleo la Pili

Toleo la Kwanza 

       
KAULI YA KATIBU MKUU WA CCM
 
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi imeamua kuanzishwa kwa Jarida la CCM linaloitwa MKEREKETWA.
Lengo kuu la MKEREKETWA ni kufikisha kwa wanachama na Jumuiya zilizo chini ya CCM za Wanawake, Vijana na Wazazi maamuzi na maelekezo ya Chama.
Ni muhimu ikafahamika kwamba siyo viongozi wa Chama katika ngazi fulani fulani tu ndio wanaostahili kupewa taarifa na ripoti za Chama, bali ni lazima wanachama wetu wa ngazi zote waelimishwe juu ya maendeleo ya Chama na Serikali zote mbili za CCM za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Jambo hili ni muhimu sana kwani "Bila ya kuwa na taarifa kamili, hakuna mwanachama awezaye kuzitetea Sera za CCM mbele ya umma".
Zaidi ya kutoa taarifa za maamuzi, maelekezo na maendeleo ya Chama, Mkereketwa litakuwa pia likifanya uchambuzi na kutoa ufafanuzi wa sera za CCM hasa pale zinapopotoshwa. Litakuwa pia na makala za historia ya Chama na viongozi wake pamoja na mashujaa mbali mbali waliojitoa muhanga katika kupigania Uhuru wa Tanganyika na kufanikisha Mapinduzi ya Zanzibar.
 
Mkereketwa litaongozwa na ukweli na usahihi wa mambo katika makala zake na halitokuwa na ushabiki. Lengo la Mkereketwa zaidi ya kuwaarifu wanachama wa CCM, ni kuwa kimbilio la Watanzania wote la kutafuta ukweli na usahihi wa mambo.
Wanachama wa CCM, wasomi na wananchi wote kwa jumla wanakaribishwa kuchangia makala katika jarida hili kwa kuzingatia sera na malengo yake.
Tofauti na magazeti ya kawaida, MKEREKETWA litakuwa linachapishwa kila baada ya vikao vya Halmashauri Kuu ya Taifa au wakati wote wowote mwingine Chama kitapoona kuna umuhimu wa kuchapisha Jarida hili ili kufikisha ujumbe haraka kwa walengwa.
Ningependa kuchukua nafasi hii kuwataka Makatibu Wenezi wa Chama chetu wa ngazi zote kuhakikisha kwamba Jarida hili linawafikia wanachama wetu. Jitihada zote hizi zitakuwa za bure endapo MKEREKETWA haliwafikii walengwa na kwa haraka mara tu lichapishwapo.
 
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI