| |
Chama
cha Mapinduzi (CCM) kimewapongeza waanchi na Serikali
kwa juhudi za waziwazi zinazoonekana za kuondoa umaskini
nchini.
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ulianzishwa na Serikali
mwaka 2000 kutokana na mkopo wa Dola za Kimarekani 60
milioni toka Benki ya Dunia. Serikali ya Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania nayo imetoa Dola za Kimarekani
3.2 milioni kuchangia juhudi za wananchi katika kuondoa
umaskini.
TASAF imejitanua katika wilaya 40 za Tanzania Bara na
wilaya zote za Unguja na Pemba ambapo imeshughulikia
jumla ya miradi mingi kote nchini.
Inatazamiwa kwamba katika miaka miwili ijayo, shughuli
za TASAF zitaenea katika wilaya zote za Tanzania Bara.
Miradi iliyokamilishwa hadi sasa ni pamoja na madarasa
ya shule za msingi 1,888; nyumba za walimu 481; vyoo
vya matundu 277; zahanati 272; nyumba za waganga 330;
visima 244; mabwawa 6; barabara za vijijini kilomita
1,354; bustani za miche na mingineyo kadhaa.
Kwa mujibu wa taarifa ya Serikali liyowasilishwa hivi
karibuni kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya
CCM, TASAF hadi sasa imetoa ajira kwa wananchi 69,699
ambao kati yao hawa wanawake ni 32,800.
Halmashauri Kuu ya Taifa ambayo ilikutana chini ya Mwenyekiti
wa CCM, Rais Benjamini Mkapa imeridhika na mafanikio
haya makubwa yaliyokwisha patikana na imewataka wananchi
kushiriki katika ujenzi wa miradi hiyo ili isaidie kuwaondolea
au kuwapunguzia tatizo la umaskini.
|
|
|
|
|
Tovuti
(Website) ya CCM ilizinduliwa rasmi tarehe 5 Februari,
2002 na Mwenyekiti wa CCM, Mheshimiwa Rais Benjamin
Mkapa wakati wa sherehe za Jubilel ya miaka 25 ya Chama
Cha Mapinduzi zilizofanyia Zanzibar.
Hata hivyo, muda mfupi baada ya uzinduzi huo, Tovuti
ilikabiliwa na matatizo kadhaa yaliyosababisha isiwepo
kwenye mtandao kwa kipindi kirefu.
Kutokana na kasoro hiyo, hatua za kuifufua Tovuti iyo
zilichukuliwa hivi karibuni. Hivi sasa Tovuti ya CCM
ambayo ni www.ccmtz.org au www.ccmtz.com imeundwa upya
na ipo hewani. Taarifa nyingi za Chama Cha Mapinduzi
zinaendelea kujazwa katika Tovuti hiyo.
Baadhi ya mambo muhimu yaliyowekwa ili kuitangaza CCM
ni pamoja na Hotuba mbali mbali; Mwelekeo wa Sera za
CCM katika miaka ya 2000 hadi 2010; Katiba ya CCM; ILANI
ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2000; Historia ya TANU na
ASP na mambo megine kadhaa.
Mtandao
wa Internet:
Kazi ya uundaji wa Tovuti imekwenda sambamba na uunganishaji
wa mtandao wa kisasa wa INTERNET katika Ofisi Ndogo
ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba Dar es Salaam. Kazi
hiyo imekwishakamilika na hivi sasa kompyuta ya Ofisi
ya Katibu Mkuu wa CCM imekwisha unganiswa na INTERNET.
Ili kila kompyuta katika jengo iweze kupata INTERNET,
kazi ya kuweka mtandao wa ndani (Local Area Network-
LAN) imekwishaanza.
|