|
|
| JARIDA
LA MKEREKETWA
|
Baada
ya hali ya amani na utulivu kurejea Zanzibar |
| |
- Karume
asambaza maendeleo Pemba na Unguja
- Sera
za ‘Jino kwa Jino’ zimefifia
- Na
heshima ya SMZ inang’ara
|
|
|
| |
Matokeo
ya Uchaguzi wa Rais wa Zanzibar yalitangazwa tarehe
7 Novemba, 2000. Kufuatia matokeo hayo, mgombea wa Urais
kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa
Amani Abeid Karume alishinda kwa kishindo kwa kupata
kura 248,095 (65%), ambapo mgombea wa nafasi hiyo hiyo
kupitia CUF, Seif Shariff Hamad alipata kura 122,000
(33%).Hata hivyo, kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa 2000
kulizaa hali ya mivutano mikubwa ya kisiasa, vurugu
baadhi ya nyakati na hujuma dhidi ya mali za Serikali
na wananchi.
Mivutano hiyo ilipelekea fujo na maandamano haramu ya
tarehe 26 na 27 Januari, 2001 huko Pemba, fujo zilizosababisha
kupotea kwa maisha ya watu 23, wengine kujeruhiwa na
baadhi ya wananchi kukimbilia Shimoni-Kenya. Tukio hili
liliisikitisha sana Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM kuhusu ujenzi
wa mshikamano na umoja wa Kitaifa, awamu ya pili ya
mazungumzo ya kujenga maelewano ya kisiasa baina ya
vyama vikuu vya siasa vya CCM na CUF yalifanyika. Baada
ya miezi 9 ya majadiliano na mashauriano Muafaka ulifikiwa
kati ya CCM na CUF na ulitiwa saini tarehe 10 Oktoba,
2001 Ikulu Zanzibar.
|
|
| |
|
|
|
|
|
|
|
|
| |
|
Katibu
Mkuu wa CCM, Ndugu Philip Mangula akipeana mkono na
Katibu Mkuu wa CUF, Seif Shariff Hamad baada ya kutiwa
saini Muafaka baina ya vyama vyao viwili tarehe 10/10/2001
Ikulu Zanzibar |
|
|
|
| |
Hatua
kadhaa zilichukuliwa na Serikali zote mbili za Muungano
na ya Zanzibar ili kuhakikisha kwamba vurugu za aina
hiyo zilizotokea Pemba hazirudiwi tena.
Faida zilizokwishapatikana kutokana na kutekelezwa
kwa Muafaka ni pamoja na:-
.Hali ya maelewano katika jamii imerejea na umoja
na mshikamano wa Kitaifa unaendelea kujengeka tena.
· Sera za chuki na uhasama (jino kwa jino)
za CUF zilizokuwa zikiwavutia wafuasi wengi wa chama
hicho zimefifia kwa kiasi kikubwa.
· Hadhi na heshima ya Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar na Mheshimiwa Rais Amani Abeid Karume
imerejea na inaendelea kuimarika siku hadi siku.
· Kupitishwa kwa marekebisho ya sheria za Uchaguzi
ya Zanzibar (ZEC) kumewezesha kufanyika kwa amani
na utulivu chaguzi ndogo za majimbo 17 Kisiwani Pemba
tarehe 18 Mei, 2003. Matokeo yake ni kwamba CUF ilipata
viti 11 na CCM ilipata viti 6.
Kutokana na mafanikio hayo, mazingira mazuri yamejengeka
Zanzibar ambayo yameiwezesha Serikali ya CCM ya Zanzibar
kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka
2000 kwa ufanisi mkubwa na kuharakisha maendeleo.
Katika
kipindi cha mwaka 2000-2003 uchumi wa Zanzibar umekuwa
kutoka asilimia 3.2 mwaka 2000 hadi asilimia 5.6 mwaka
2002. Mfumko wa bei umeshuka kutoka asilimia 6.2 mwaka
2000 hadi asilimia 5.2 mwaka 2002.
Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ulioanzishwa na
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mkopo
wa Benki ya Dunia umesaidia kupunguza matatizo ya
wananchi wa Zanzibar hasa vijijini. Mfuko huu umetenga
shilingi bilioni 3 kwa ajili ya miradi ya maendeleo
katika sekta za elimu, afya na huduma za maji.
Mpaka sasa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii umeshatekeleza
miradi 65, Unguja 37 na Pemba 28. Miradi hii ina thamani
ya shilingi bilioni 1,737,218,255. Katika fedha hizo,
wananchi wamechangia shilingi milioni 239,505,855
kama nguvu kazi na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii umetoa
shilingi bilioni 1,497,712,400. TASAF pia inaifadhili
miradi miwili ya kilimo cha umwagiliaji maji katika
vijiji vya Mtwango na Ndijani, Unguja. Halikadhalika
TASAF inayafanyia utafiti maeneo ya mto Mwanakombo,
Upenja, Chaani na Kibokwa kwa Unguja na Weni pamoja
na Gae la Mtungi kwa Pemba ili kuangalia uwezekano
wa kuyatumia maeneo hayo kwa ajili ya kilimo cha kumwagilia
maji.
|
|
|
| |
|
|
|
|
|
|
|
|
| |
|
|
|
“Sasa
mambo safi”, Naibu Katibu Mkuu CCM (Zanzibar), Ndg.
Saleh R. Ferou |
|
|
|
|
| |
|
|
|
|
|
|
|
|
| |
|
|
|
|
Wake
kwa waume wakishiriki katika mradi wa TASAF wa ujenzi
wa kusambaza maji wa Kiuyu Mnungwini (Pemba) |
|
|
|
|
|
| |
|
Tangu
Serikali ilipozindua mpango wa kupunguza umaskini mwezi
Mei, 2002 imekuwa ikiweka mkazo mkubwa katika uimarishaji
wa sekta ya elimu, mawasiliano, afya na maji. Serikali
imeshatekeleza mambo yafuatayo:-
· Imeandikisha asilimia 98 ya watoto waliofikia
umri wa kwenda skuli.
·. Mpango Mkuu wa Elimu umefanyiwa mapitio.
· Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar kimeshatimiza
mwaka wa pili tangu kilipofunguliwa rasmi mwaka jana.
Chuo hiki kina wanafunzi 54 wanaochukua shahada ya ualimu
na sanaa.
· Imejenga barabara zenye urefu wa kilomita 60
kwa kutumia fedha za Serikali.
· Zabuni ya utanuzi wa uwanja wa ndege wa Zanzibar
tayari zimeshatangazwa.
· Inaimarisha huduma za maji safi katika maeneo
mbalimbali ya Unguja na Pemba.
· Serikali ya Japani iko katika hatua za mwisho
inashughulikia ombi la mradi wa maji katika Manispaa
ya Zanzibar wenye thamani ya shilingi bilioni 11.
· Serikali imeyatengeneza majenereta ya umeme
Pemba kwa thamani ya shilingi 497,000,000/=.
· Katika sekta ya kilimo, Serikali inakiimarisha
Chuo cha Kizimbani kwa ajili ya shughuli za utafiti
wa kilimo na mifugo. Serikali pia inayafanyia utafiti
mabonde 57 ya Unguja na Pemba yenye ukubwa wa hekta
17,042.
Kwa kuwa Ilani ya Uchaguzi ya CCM inatilia mkazo suala
la ustawi wa jamii wa wananchi wake katika utekelezaji
wa ahadi za Serikali, suala la mafao ya wastaafu lilishguhulikiwa
mara moja baada ya Rais Amani Abeid Karume kuchukuwa
madaraka mwaka 2000.
Kuanzia Novemba 2000 hadi Juni 2003, jumla ya wafanyakazi
3,741 wameshalipwa viinua mgongo yenye thamani ya shilingi
2,914 milioni. Kadhalika wafanyakazi 1662 wameshalipwa
malimbikizo ya pensheni zao.
Wakati Rais Karume anaingia madarakani, Serikali ilikuwa
inadaiwa mafao ya viinua mgongo vya wastaafu wapatao
4967 yenye thamani ya shilingi 5,325 milioni.
Wastaafu 2293 pia walikuwa wanaidai Serikali shilingi
1,092.2 milioni kama malimbikizo ya pensheni.
Malipo hayo yamefanywa kwa wadai wote wa Unguja na Pemba.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutekeleza
Ilani ya Uchaguzi ya CCM pia imeweka mkazo katika ujenzi
wa barabara mijini na vijijini.
Katika kipindi cha miaka miwili na nusu ya utekelezaji
wa Ilani, Serikali imeweza kujenga barabara Unguja na
Pemba ili kuimarisha miundo mbinu ya uchumi.
UNGUJA
barabara zilizojengwa ni:-
·
Kitogani-Paje Kilomita 11-2
· Barabara ya Bambi – kilomita 6.0
· Jang’ombe-Mpendae – kilomita 0.6
· Kaebona-Kaepwani – kilomita 4.5
· Makunduchi-Mtende – Kilomita 5.5
PEMBA
barabara zilizojengwa ni:-
·
Chake-Wesha – kilomita 7.0
· Chake-Vitongoji – kilomita 7.0
· Kilindi-Micheweni – kilomita 6.0
Jumla ya shilingi 2,282 bilioni zimetumika kugharamia
ujenzi wa barabara hizi. Kati ya hizo, shilingi 1.319
bilioni zimetolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
na shilingi 963 milioni ni msaada wa lami kutoka Serikali
ya Libya.
Barabara zinazoendelea kujengwa hivi sasa kwa nguvu
za Serikali ni kwa upande wa Unguja barabara ya Mahonda-Donge
yenye urefu wa kilomita 14; na Pemba ni barabara ya
Mtu Haliwa-Chokocho ya kilomita 12.
Barabara nyingine zinazojengwa kwa msaada wa wafadhili
ni:-
· Kidimni-Kitope – kilomita 29.6
· Mkoani-Chake – kilomita 30.5
Mafanikio yote haya yameweza kupatikana katika kipindi
cha miaka miwili na nusu tu cha uongozi wa Rais Amani
Abeid Karume.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Rais
Karume akikagua ujenzi wa barabara mpya ya Kilindini -
Micheweni huko Pemba |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Mjumbe
wa Kamati Kuu ya CCM na Waziri Kiongozi wa SMZ akizindua
mradi wa maendeleo Zanzibar. |
|
|
|
|
|
|
|
|
|