|
|
| JARIDA
LA MKEREKETWA
|
Uhusiano
kati ya Chama Cha Mapinduzi na Vyama vya Nje vya kidugu
na rafiki |
| |
Chama
Cha Mapinduzi (CCM) kimeendelea kuwa na uhusiano na
ushirikiano wa karibu na vyama rafiki. Miongoni mwa
vyama hivyo ni ZANU-PF (Zimbabwe), SWAPO (Namibia),
FRELIMO (Msumbiji), ANC (Afrika Kusini), UNIP (Zambia)
na MPLA (Angola). |
|
| |
|
|
|
|
| |
|
Katibu
Mkuu wa FRELIMO, Komredi Armando Emilio Guebuza akisalimiana
na Mweka Hazina wa CCM Taifa, Mama Salome Mbatia katika
ofisi ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba Dar
es Salaam. |
|
|
| |
Aidha,
CCM imeendeleza uhusiano na ushirikiano wa karibu na
Chama cha Kikomunisti cha China, Chama cha Kikomunisti
cha Cuba, Chama cha Wafanyakazi cha Jamhuri ya Kidemokrasia
ya watu wa Korea na vyama vingine rafiki ndani na nje
ya Bara la Afrika.
Viongozi Wakuu wa CCM wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM,
Rais Benjamin Mkapa wamekuwa wakitumia fursa ya ziara
za nchi za nje kukutana na viongozi wa vyama rafiki
kwa lengo la kuimarisha uhusiano na ushirikiano na CCM.
Vile vile, Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Philip Mangula
alifanya mazungumzo na Mabalozi na Wawakilishi kutoka
nchi za vyama rafiki kwa lengo la kuimarisha uhusiano
na ushirikiano na CCM.
Baadhi ya vyama rafiki vilivyo-tembelea Tanzania hivi
karibuni kwa mwaliko wa CCM ni pamoja na ANC, SWAPO,
Labour Party ya Uingereza na FRELIMO.
Aidha, CCM ilialikwa na kushiriki katika mikutano kadhaa
ya siasa pamoja na kutembelea vyama vya ANC - Afrika
Kusini, NRM ya Uganda, Botswana Democratic Party (BDP),
UDF ya Malawi na Labour Party ya Uingereza. |
|
| |
|
|
 |
|
|
| |
|
|
|
Mjumbe
wa NEC, Capt. John Komba ambaye pia ni Mkurugenzi wa
TOT akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu wa UDF, Ndugu
Kennedy Makwangaza Makao Makuu ya CCM, Dodoma |
|
|
|
|
|
Wajumbe
wapya wa NEC wateuliwa |
|
|
|
|
|
|
|
- Mwasamale
awa Katibu
wa CCM wa Mkoa
|
|
|
|
|
|
Halmashauri
Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) ilimaliza
kikao chake cha siku mbili mjini Dodoma tarehe 14/9/2003
kwa kuwateua wanachama wa CCM sita kuwa Wajumbe wa
Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC).
Walioteuliwa ni Ndugu Asha Abeid Faraji, Ndugu Mohammed
Mohammed Jecha, Ndugu Abdallah Said Natepe, Ndugu
Cleopa David Msuya, Ndugu Grace Soka na Ndugu Jumanne
Mangara.
Wajumbe hao wameteuliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa
ya CCM kwa mujibu wa Katiba ya CCM ambayo imetenga
nafasi kumi kwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Benjamin W.
Mkapa kupendekeza kwa Halmashauri Kuu ya Taifa ya
CCM majina ya wanachama kuingia kwenye NEC.
Katika nafasi kumi alizotengewa Kikatiba Mwenyekiti
wa CCM, ni nafasi saba sasa zilizokwisha jazwa ikiwemo
na ile ya uteuzi wa Ndugu Saleh R. Ferouz ambae kwa
sasa ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar.
Aidha, Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM ilithibitisha
uteuzi wa Ndugu Aron T. Mwasamale kuwa Katibu wa CCM
wa Mkoa wa Iringa.
SEMINA
Chama Cha Mapinduzi kimekuwa kinaendelea kutekeleza
kwa ufanisi mkubwa programu ya kujenga uwezo wa viongozi
wake kwa ngazi zote kupitia mafunzo kwa mujibu wa
maagizo ya Mkutano Mkuu wa Sita wa Oktoba 2002.
Mpaka sasa zimekwishafanywa semina ngazi za Kamati
Kuu ya CCM, Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC)
na Halmashauri Kuu za CCM za Mikoa. Mafunzo pia yametolewa
kwa Wakufunzi (Makada) wa Kitaifa na Makada wa Mikoa.
Baadaye mafunzo yatafika Wilayani na kuhuka hadi ngazi
ya Kata na Tawi. Lengo kuu ni kujenga itikadi moja
ndani ya Chama.
|
|
|
|
|