Ilani ya CCM Habari Mpya Historia ya TANU na ASP Kutoka Magazetini Hotuba

 

 

 

 

 

 

 

 

 

JARIDA LA MKEREKETWA

CCM yatoa kadi mpya kwa wanachama wake
  • Mtindo wa ‘papo kwa papo’ sasa basi
Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM iliamua mwaka 2002 kwamba ufanyike utaratibu wa uchapishaji upya wa Kadi za CCM kwa ajili ya wanachama wake wote (wazamani na wapya) nchini.
Madhumuni ya uamuzi huo ni kuongeza ubora na udhibiti wa kadi za CCM ili zisiweze kuingia katika mikono ya watu wasiohusika.
Katibu Mipango wa CCM Taifa, Ndugu Jackson Msome ameliambia jarida la Mkereketwa kwamba Sekretarieti ya Halmahauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) imeanza kutekeleza zoezi hilo na hadi sasa jumla ya kadi mpya 470,000 zimekwisha chapishwa na baadhi yake zimefikishwa mikoani.
“Lengo letu ni kuchapisha kadi mpya zaidi ya milioni tatu (3,000,00) ili wanachama wetu wote wa zamani na wale watakaojiunga na CCM waweze kupewa kadi hizo ambazo zimetengenezwa kitaalamu na zina alama maalum za siri”, aisema.
Katibu Mipango amewakumbusha Makatibu wa CCM wa Mikoa kuzingatia utaratibu uliowekwa wa usambazaji wa kadi hizo ili kudhibiti uchukuaji, ugawaji na mawasilisho ya fedha
.
           
     
         
Katibu Mipango CCM Taifa, Ndg. Jackson Msome
   
Alieleza kwamba ili kufanikisha vizuri zoezi hili, Kamati Kuu ya CCM imeagiza mambo yafuatayo yazingatiwe:-
Kadi mpya zichukuliwe kutoka Ofisi za CCM za Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar na Makatibu wa CCM wa Mikoa wenyewe. Mtu mwingine hatapatiwa kadi katika ofisi hizo mpaka awe na kibali cha maandishi cha Katibu wa CCM wa Mkoa anakotoka.
Makatibu wa CCM wa Mikoa wahakikishe kwamba wanatuma mawasilisho ya fedha zinazohusika Makao Makuu ya CCM bila kuchelewa. Sekretarieti ya NEC itakuwa karibu sana na Mikoa ili kuratibu suala la uchukuaji wa kadi na mawasilisho ya fedha kila mwezi.
Matawi ya CCM yaelekezwe kurejesha utaratibu wa Katiba ya CCM ya kuwapokea wanachama wapya badala ya mtindo wa “papo kwa papo”.
Ndugu Msome amewakumbusha Makatibu wa CCM wa Mikoa kutekeleza agizo la Chama la kuanzisha “Mfuko wa Vifaa” katika kila ngazi ya Chama ili itumike kununulia kadi za CCM na kuendeshea shughuli nyingine za Chama.
Watendaji wa CCM wa ngazi zote wanatakiwa kuliendesha zoezi hili muhimu kwa uangalifu na uadilifu wa hali ya juu bila kuleta usumbufu kwa wanachama wa CCM.
Mangula aelezea utekelezaji wa ‘Muafaka’ ingereza
  • Aiwakilisha CCM kwenye Mkutano wa Labour Party
Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Philip Mangula hivi karibuni alialikwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Laour Party cha Uingereza, David Triensman kuhudhuria Mkuano Mkuu wa chama chao uliofanyika kwenye kituo cha kitaifa cha Bournemouth kuanzia Septemba hadi Oktoba 2, mwaka huu.
Aidha, Katibu Mkuu wa CCM pia alialikwa na Serikali ya Uingereza kutembelea sehemu mbalimbali za nchi hiyo kwa muda wa wiki mbili.
Katika ziara hiyo, kiongozi huyo wa CCM alitumia fursa hiyo kuwaeleza wenyeji wake kuhusu utekelezaji wa Muafaka wa CCM na CUF, hali ya kisiasa nchini na maandalizi ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa Serikali wa mwaka 2005.
   
       
Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Mangula akimsikiliza Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili BBC, Ndugu Dunstan Tido Mhando alipotembelea Studio za BBC London. Kushoto
ni Jumbe Omar Jumbe wa BBC.
 

Akiwa Uingereza, Ndugu Mangula alikutana na watu kadhaa mashuhuri wakiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Bwana Donald Mac Kinnon; Mkurugenzi Mkuu wa Westminster Foundation for Democracy, Bwana David French na Mkrugenzi wa Jamuiya ya Afrika (Royal African Soceity), Bwana Richard Dowden
Katibu Mkuu wa CCM alifanya mazungumzo na Watanzania wanaoishi huko pamoja na wafanyakazi wa Ubalozi wetu ambao aliwaeleza jinsi hali ya kisiasa ilivyo nchini Ta-nzania na mae-ndeleo ya kuuje-nga uchumi wa Tanzania pamoja na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2000.
Aidha, alifanya mahojiano na Shirika la Habari la BBC kwa lugha zote mbili za Kiswahili na Kiingereza ambapo alizugumzia mambo mengi kuhusu hali ya kisiasa nchini, Itikadi ya CCM, Mwelekeo wa Sera za CCM na mafanikio yaliyopatikana na Serikali zote mbili za CCM za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM.