| Mwalimu Julius K. Nyerere na
wanachama na viongizi wa TANU na ASP walio wengi walikuwa
na matarijo makubwa kwa Chama kimoja cha Mapinduzi.
Miongoni mwa matarajio hayo ni kukamilisha Muungano
wa Tanzania; kuleta maendeleo ya pamoja na haraka kwa
nchi yetu; kumkomboa Mtanzaina na Mwafrika kifikra,
kisiasa, kiuchumi na kijamii; na kusaidia kuharakisha
kufikia lengo la kujenga nchi inayofuata siasa ya Ujamaa
na Kujitegemea.
Aidha, Chama kimoja cha Mapinduzi kilitarajiwa kushiriki
kwa ukamilifu katika kutokomeza ukoloni katika Bara
la Afrika na kwingineko duniani na kuendeleza siasa
ya kutofungamana na upande wowote hasa kwa kuzingatia
kwamba katika miaka ya 1970 na 1980 dunia ilikuwa bado
imegawanyika kisiasa, kiuchumi na kiulinzi katika kambai
mbili zenye uhasama.
Kambi hizo ni ya Magharibi ikiongozwa na Marekani na
ile ya Mashariki ikiongozwa na Umoja wa Kisovieti. Waasisi
wa TANU na ASP walitambua kwamba kuwepo kwa vyama viwili
katika mazingira ya siasa ya chama kimoja kulipunguza
upeo, nguvu na umoja wao katika kuendeleza mapambano
ya kujenga Ujamaa nchini na kushiriki kwa pamoja na
kwa ukamilifu katika harakati za mapinduzi ya Tanzania,
Afrika na dunia kwa jumla.
TANU na ASP toka mwanzo vilikuwa ni
vyama vya ukombozi vilivyojengeka kwenye msingi wa demokrasia.
Kwa mfano, pendekezo la Mwalimu Julius K. Nyerere la
kuunganisha vyama lilipitishwa na TANU na ASP kwa njia
ya kidemokrasia.
TANU na ASP walipeleka suala zima la kuunganisha vyama
kwa wanachama wenyewe kwani ndio wenye vyama.
Wanachama hao katika matawi yao walitakiwa wajadili
nakutoa maoni yao kuhusu suala la kuunganisha TANU na
ASP ili kiundwa Chama kimoja cha Mapinduzi.
Kazi hiyo ilifanyika kwa ufanisi kama ilivyoagizwa
na Halmashauri Kuu za Taifa za TANU na ASP. Licha ya
wanachama kujadili na kutoa maoni yao, kwa Zanzibar
viongozi wa ASP walipwewa nafasi ya kujadili na kutoa
maoni yao katika vikao vyote vya Chama.
Wanachama walijadili na kutoa maoni yao kwanza ndipo
wakafuata viongozi katika Halmashauri za vikao mbalmblai
vya ASP. Angalia majedwali na. 1 na 2 ambayo yanaonyesha
matokeo ya maoni ya wanachama wa TANU na ASP kuhusu
kuunganishwa vyama. Matokeo ya Maoni ya Wnachama wa
TANU kuhusu kuunganishwa TANU na ASP
Matawi |
Idadi |
Asilimia |
| Idadi ya Matawi ya TANU |
6,639 |
100 |
| yaliyokutana |
6,427 |
96.81 |
| yaliyokutana |
212 |
3.19 |
| yaliyokubali |
6,424 |
99.95 |
| yaliyokataa |
3 |
0.05 |
| Idadi ya matawi madogo
ya TANU |
38 |
100. |
| Matawi Madogo yaliyokutana
|
38 |
100 |
| Matawi Madogo yaliyokubali |
38 |
100 |
| Matawi Madogo yaliyokataa |
Hakuna |
0.00 |
Chanzo: Chuo cha CCM Kivukoni (1981) Historia ya Chama
cha TANU 1954 hadi 1977, (Dar es Salaam : Mpiga Chapa
wa Serikali)
|