Lipumba: Mgombea urais wa
CUF aliyejaa majisifu ya usomi
KAMPENI kwa
ajili ya uchaguzi mkuu wa
Oktoba, mwaka huu zimepamba moto.
Vyombo mbalimbali vya habari haviko
nyuma katika kufuatilia habari hizo za kampeni
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi CUF Profesa Ibrahim Lipumba amemaliza awamu ya kwanza ya ziara ndefu iliyomchukua siku kumi katika mikoa ya Kusini, akifanya kampeni za kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao wa mwezi Oktoba.
Juzi alilala
Ziara hiyo ya mikoa ya Kusini, ambayo mimi niliifuatilia nyuma nyuma kutokana na kunyimwa usafiri katika kanvoi yake, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kukosekana kwa nafasi ndani ya magari, niliungana nayo mkoani Mbeya na kwa muda wa siku kumi zilizofuata tulitembelea mikoa ya Ruvuma, Mtwara na Lindi.
Nadhani nilinyimwa lifti katika magari ya kanvoi ya Lipumba si kwa sababu hakukuwa na nafasi, bali bila shaka ni kwa sababu nilitokea katika magazeti ya Uhuru, magazeti ambayo yanaonekana kama ni chombo cha upinzani, na kwa imani yao haliwezi kuandika habari zozote nzuri za CUF.
Nilisafiri kwa kurukia mabasi kutoka basi
moja na kuendelea
na basi lingine
katika msafara mzima kutoka Mbeya
na katika mikoa ya
Nini kilichojiri katika ziara hiyo?
Katika kampeni zo zote za kisiasa ili upate kura ni lazima unadi sera kwa kuwaeleza wananchi nini unachotarajia kufanya iwapo utachaguliwa katika nafasi unayoiomba.
Nchi hii
Lipumba ana nne, Kikwete ana moja ndio wimbo mkubwa wa wapambe wa kiongozi huyo kila walipopita wakiomba kura, wakiwa na maana kwamba Lipumba ana digrii nne wakati Kikwete ana digrii moja, na kwa maana hiyo yeye ni msomi mwenye uwezo na kustahili kuwa rais.
Niliianza ziara
na kikosi
cha Lipumba chenye magari manne. Wakiwa
ndani ya magari
Nilijaribu kuwahoji wapambe wake kila nilipopata nafasi waniambie nini kilikuwa kinafuata. Kwa mfano, niliuliza baada ya mkutano huu mwenyekiti anaelekea wapi? Hatuna hakika, tutakuwa na kikao jioni saa mbili baada ya hapo ndipo tutajua mwelekeo. Wewe usiwe na wasiwasi, tutakupigia simu kukuarifu, ndio majibu ambayo kila wakati nilikuwa nikipatiwa, bila shaka kwa nia ya kunikwepa na kunipotezea dira na mwelekeo wa msafara.
Lakini hoja
ya usomi, uprofesa, na
kuwa na digrii
nyingi ndiyo vigezo pekee au sifa ya kumfanya
mtu aweze kuwa rais wa
nchi?
Kilichonichosha katika ziara ya
Lipumba ni
kwamba maneno anayozungumza ni
Mkutano utaanza kwa mmoja wa wapambe wake kupanda jukwaani na kutoa wasifu wa Lipumba, vyuo alivyosoma hapa nchini, Marekani na shahada alizopata. Baada ya hapo atapanda Lipumba na kuanza kwa kuponda sera za CCM katika maeneo ya uchumi na elimu, na kisha ataeleza kile atakachofanya.
Ukienda ndani ya analosema utakuta anarejea kauli za CCM na sera zake katika kukuza uchumi, huduma bora za afya, ajira ya vijana na kupanua elimu ya msingi Sasa ni kipi kipya Lipumba anachojaribu kuwaeleza Watanzania?
Pengine kutoa chakula cha mchana anachodai kwamba CUF ikiingia madarakani itahakikisha kinatolewa kwa wanafunzi katika shule zote za msingi, kitu ambacho hakuna hata serikali moja duniani iliyofanikiwa kufanya kwa ukamilifu.
Katika maeneo mengine nilikopata nafasi ya kuzungumza na kuwahoji wananchi, wengi walionekana kuwa na hamu ya kumuona Lipumba anafananaje, kuliko kuvutiwa na sera zake. Wengi, na hasa kinamama, walifika kwenye mikutano yake kwa nia ya kutaka kumwona Lipumba ni nani, na baada ya hapo kubeba watoto wao na kuelekea majumbani kwao.
Lakini hata wanaume nao waliofika mikutanoni na niliopata nafasi ya kuhojiana nao, wengi walisema walitarajia kusikia kitu kipya, lakini waligundua hakuna jipya zaidi ya majigambo ya Lipumba na kurejea sera za CCM.