Kwa nini Watanzania wanajiandaa kuipa CCM ushindi wa kishindo?
Sera zake za maendeleo zimejionyesha kwa yaliyotekelezwa, hata wapinzani wanakiri
VYAMA  vya upinzani vinaomba Urais  vitawale sawasawa na CCM inayoomba kuendelea na Utawala huo. Lakini mpaka sasa wananchi wanatambua kwamba vyama vya Upinzani havichaguliki.  Makala hii ya Mwandishi wetu LAUDEN MWAMBONA inatoa ufafanuzi  zaidi  ni kwa nini CCM inaomba kuendelea kushirikiana na wananchi katika kusukuma gurudumu la maendeleo.
WAGOMBEA tisa wa Urais kupitia Vyama vya upinzani  bado wanaendelea na kazi ya kuomba kura ili wapate nafasi hiyo. Pamoja na kutokwa jasho jingi katika harakati hizo bado vyama hivyo vinajikongoja kusaka Urais
Vyama vyenye wagombea ni SAU ambacho mgombea wake ni Paul Kyara,  NLD ambacho mgombea wake ni Emmanuel Makaidi,  DP chenye mgombea wake Christopher Mtikila na chama cha TLP ambacho kama kawaida Mwenyekiti wake, Augustine Mrema anawania Urais kwa mara ya tatu.
Kiongozi mwingine wa chama cha upinzani anayewania kwa mara ya tatu tangu 1995 akisaka  Urais ni Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF ambaye wanachama wake tayari wamempa somo kwamba akishindwa mara ya tatu  basi ashike lake.
Wengine ni  Anna Senkoro wa chama cha PPT Maendeleo, Freeman Mbowe wa CHADEMA, Sengondo Mvungi wa  NCCR-MAGEUZI  na Profesa Leonard Shayo wa chama cha  Demokrasia Makini.
KWA NINI WANAGOMBEA?  
Watu wengi wanajiuliza sana swali hili na wanashindwa kupata jimbo. Baadhi ya vyama vinavyoshiriki vinadai vinataka kuwasaidia wananchi. Wanasema vinataka kuwapatia utajiri Watanzania na kuwaondoa kwenye umaskini. Lakini wanashindwa kutoa mbinu za kutekeleza hayo.
Lakini  maelezo wanayotoa kwenye mikutano ya kampeni ni ya kukashifu na kuipinga CCM tu na wala siyo kueleza watafanya nini.
Taarifa zinazopatikana kutoka kila mikutano yao wagombea wote wananukuliwa kupinga CCM tu.   Ni mara chache Mgombea wa Urais wa TLP , Mrema alirukia pia kwa vyama vingine vya upinzani akieleza kwamba havifai.
Mfano ni pale alipokuwa Shinyanga ambapo Mrema kwa kinywa chake aliwaambia wakazi wa huko kwamba Profesa Lipumba wa CUF hafai kuwania Urais kwa vile hajawahi kuwa hata katibu kata.
Mrema pia alinukuliwa  akiwa Mwanza, akisema, Lipumba hafai kwa vile aliwahi kuteuliwa kuwa mshauri wa masuala ya uchumi  wa Rais Ali Hassan Mwinyi na kusababisha uchumi kuporomoka kuliko kawaida.
 Kipindi cha Lipumba serikali ilizembea kukusanya kodi, huduma za jamii zilizorota, mishahara ya wafanyakazi wa serikali haikupatikana. Kwa ujumla kipindi hicho wafanyakazi walidharauliwa. Na dhuluma ilijaa kwenye vyombo vya dola na mahakama kutokana na vitendo vya rushwa kushamiri.
Lakini pia Mrema alivitaja vyama vya upinzani kuwa havina ushirikiano hata kidogo na kufafanua kwamba CUF ilishindwa kutoa kura kwa vyama vya upinzani mwaka 1996 huko Zanzibar badala yake kura zilipigwa kwa maruhani baada ya wagombea wake kuenguliwa mahakamani.
Nasema ni Mrema pekee ambaye kidogo ameshambulia vyama vingine vya upinzani, kwa vile ndiye aliyesikika, lakini ukweli ni kwamba vyama vingine vyote vinatembeza magari yao kwa kuikashifu CCM bila kunadi sera.
Pamoja na CUF  kuonyesha ilani yake ya uchaguzi lakini mpaka sasa kinashindwa kuifafanua ilani hiyo ni kwa vipi watatekeleza majukumu  kwa vile  chama chenyewe hakijawahi kuwa na mipango ya maendeleo.
Kwa kawaida ilani , inaandaliwa kwa kuzingatia mipango ya maendeleo iliyoandaliwa na serikali katika vijiji, kata, tarafa, wilaya, mikoa, Wizara  na hatimaye Taifa  jambo ambalo halijafanywa na CUF.
Hivyo ni vigumu kwa wananchi kuelewa sababu za CUF na vyama vingine vya upinzani kutaka vitawale Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
KWA NINI CCM INAOMBA KUENDELERA KUONGOZA
Sababu zipo nyingi, lakini kwa LEO nitaeleza mambo yatakayofanyika kwa sekta ya afya ikiwa CCM itachaguliwa 
Sekta ya afya ni muhimu kwa Watanzania wote. Watanzania wanahitaji kuona hospitali zinatoa huduma safi za tiba na kinga kwa magonjwa. Pia lazima mazingira yawe safi katika maeneo yote ya Hospitali, vituo vya Afya na  Zahanati.
Waziri wa Afya Anna Abdallah ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya CCM alisema hivi karibuni kwamba  mipango ya maendeleo  katika serikali ya CCM   inatarajiwa kugharimu zaidi ya sh. bilioni 90.8
Fedha hizo zitatumika kwa kazi ya kuendeleza ukarabati wa  Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ili iweze kutoa huduma bora na safi kwa wagonjwa.  Ukarabati huo utafanyika katika wodi, maabara, chumba cha upasuaji na  kujenga wodi ya watoto wagonjwa Muhimbili.
Hospitali kuu za jiji nazo zitakarabatiwa ikiwa ni pamoja na kukarabati wodi za wagonjwa  hospitali ya Ocean Road, kujenga maabara ya kudhibiti ubora na kununua vifaa vya maabara Dar es salaam na Mwanza.
CCM inaomba kura kwa sababu  inataka serikali yake ikarabati na kuboresha vituo vya utafiti wa magonjwa ya binadamu huko  Amani, Gonja, Mwanza, Tukuyu, na ofisi za Makao Makuu ya Wizara ya Afya.
 Vyuo vyote 35 vya afya navyo vitakarabatiwa na kununua vifaa zaidi vya hospitali za rufani za Mbeya, Mirembe, Buhando na KCMC. Hospitali za mikoa, wilaya na hospitali teule nazo kuangaliwa kwa karibu zaidi.
Jambo lingine ambalo CCM inaomba kura kwa wananchi ili serikali yake ifanye kazi ni kuendeleza mipango ya kudhibiti malaria, kifua kikuu na ukoma,  na kusimamia kikamilifu mpango wa kudhibiti ukimwi ili waathirika wengi zaidi wapate dawa za kurefusha maisha bila ya malipo
CCM inasema wajawazito  na watoto wataendelea kupata huduma za tiba bila malipo. Na kwamba huduma za chanjo za kinga zitaimarishwa zaidi.
Suala la kupatikana dawa kwenye vituo vya afya na zahanati ni jambo ambalo limeahidiwa  kuimarishwa zaidi katika mipango ya maendeleo ya serikali ya CCM.
CCM ilitaja  Zahanati zitakazoongezwa katika kupata dawa kuanzia mwaka huu wa fedha baada ya kuchaguliwa kuwa ni Olkerieni , Ngyani,Terrati na Kipendenkovele zote za halmashauri ya Arumeru wakati  kituo cha afya cha Themi manispaa ya Arusha nacho kitapata dawa za kutosha .
Zahanati na vituo vingine vitakavyopata dawa kwa mkoa wa Arusha Matale, Meserani, Aya-labe, Lambo, Oldeani, Esere, Oloipiri na Magaiduru  wakati kwa upande wa mkoa wa Dar es Salaam zahanati zitakazopata  dawa ni  Ukonga, Msewe, Mlalakuwa na  Makongo juu.
Zahanati za mkoa wa  Dodoma zinazoongezwa katika mpango safi wa kupata dawa  ni Ntuba, Zuzu, Chahwa, Michese, Ntyuka, Gawaye, Ndembwe, Mpamatwa, Chinyangutu, Tambi, Matonya, Chitemo, Ikuyu, Kiboriani, Kimagai, Mtamba, Kidenge,  Ndurungumi Ihanda, Chiwe, Chamkoroma, Pigalame, na Lenjulu.
CCM inasema serikali yake itapeleka dawa zahanati mbalimbali za mkoa wa Iringa zikiwemo za Masisiswe, Ndegenda, Ngongwa,  Ibanda, Ilungu, Ukange, Kipagalo, Muhinga, Igombavanu, Kilolo, Mhula na vituo vya afya vya Makoka, Sadani, Mgololo na Kimande.
Huko Kagera dawa zitakwenda zahanati za Bulembo, Kibirizi, Buzi, Nyakato na Bulembo wakati huko Kigoma  zahanati zitakazopata ni Kanazi, Mugera, Kajana, Nyamugali, Risaba, na Kituo cha afya cha Janga.
Ahadi kama hizo pia  zinatolewa mkoa wa Kilimanjaro ambako zahanati zitakazoingizwa kwenye mpango wa kupata dawa za kutosha ni Mdawi, Mahoma, Kindi, Kimangara, Marangu Kiraracha,  Mdawi, Karamba, Bwambo na Mhezi.
Huko mkoa wa Lindi , dawa zitaongezeka katika  Zahanati za Namalongo, Kihuwe, Nkaloji na Kituo cha Afya Marando.
Zahanati za mkoa wa Manyara zitakazoongezwa kwenye orodha ya zahanati zinazopata dawa nyingi ni  Endasaki, Manyara, Simbai, Gahandu, Ngorat, Hasama, Tsawa, Onyomat, Dohoni, Dabir, Mayoka, Minjingu, Lemukuna, Chokaa, Narakau,  na vituo vya afya vya Gallapo na Mererani.
Mkoa wa Mara utaongezewa dawa  kwenye zahanati za Kunzungu, Wariku, Mirwa, Bwitegi, Ochuna, Kibuyu wakati mkoa wa Mbeya utaongezewa dawa kwenye zahanati za Saza, Mbogani, Soweto, Ifuko, Maoga, Nsalanga, Iwambi, Iwowo, Kapele, Namwanga, Mpapa Itumbi wakati vituo vya afya vitakavyofaidika ni Mwakaleli.
Huko Morogoro , CCM imeahidi  kwamba serikali yake itaongeza dawa kwenye  zahanati za Mabula, Majawanga, Mzaganza, Masenge, Dakawa na Kituo cha Afya cha Kidete.
Ahadi kama hizo pia zimetolewa kwa zahanati kadhaa za mikoa ya Mtwara, Mwanza, Pwani, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Singida, Tabora na Tanga.
Kwa hali hiyo, CCM inayo sababu kubwa ya kuomba wananchi waichague ili itekeleze kazi hiyo kwa sekta ya Afya kwani wagombea wengine hawajui hali halisi ya huduma zitolewazo kwenye zahanati hizo.