UHURU 23.11.2005
Kikwete
asema CUF isubiri kipigo Des.
14
Asema baada ya kushindwa
Na Rashid Zahoro, Kibiti
MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya
Muungano wa
amesema hivi sasa CUF imechanganyikiwa na kwamba isubiri kipigo cha dhoruba
ifikapo Desemba 14.
"CUF imechanganyikiwa, baada ya kushindwa
kikubwa na cha dhoruba nzito katika uchaguzi mkuu wa Desemba 14.
"Desema 14 ikifika hakuna cha Lipumba wala cha Mbowe, mimi ndiye nitakayeibuka
mshindi baada ya uchaguzi wa siku hiyo... safarini tupo wengi, lakini wengine
wananisindikiza mimi," alisema.
Kikwete aliyasema hayo jana alipoanza kampeni zake wakati aliposimama kuwasalimia
wananchi wa vijiji vya Jaribu Mpakani, Bungu na Hanga, akiwa njiani kwenda
kuhutubia mikutano ya kampeni katika maeneo ya Nyamisati na Kibiti mkoani Pwani.
Kuhusu wanasiasa wanaotumia nyumba za ibada kuendesha kampeni, Kikwete alisema
wanasiasa wa namna hiyo wamefilisika kisiasa na kwamba kamwe wasichaguliwe.
"Hawa watu hawana kitu ndio maana wanakimbilia misikitini… misikiti ni sehemu ya
kusali na kumwabudu Mungu siyo siasa. Anayekimbilia huko siasa imemshinda,
amefilisika, hana mbele wala nyuma," alisema Kikwete.
Akizungumzia bei ya korosho, mgombea urais huyo wa CCM, aliwaahidi wakazi wa
vijiji vya Bungu na Hanga kuwa
atahakikisha bei ya zao
waweze kufaidika na zao
Kikwete alisema serikali ya awamu ya nne imepania kuinua kilimo na kukuza uchumi
wa Tanzaania na pia kupanua masoko ya mazao ili wakulima wawajue wanunuzi.
"Sio leo anakuja Fidha Hussein kesho Mohamed Enterprises... tunataka mkulima awe
na soko la uhakika na amjue mnunuzi wake," alisema Kikwete.
Kikwete alikiri kufahamu kuwepo kwa wanunuzi wa korosho ambao huwapunja wakulima
kwa kushusha bei za zao
Kuhusu vijana wa vijiji hivyo, Kikwete aliahidi kuwatatulia tatizo la ajira kwa
kuwapatia mitaji kwa njia ya mikopo ili waweze kujiajiri wenyewe.
Kikwete katika msafara huo pia alizungumza na wananchi katika vijiji vya
Nyamtonga, Minjeti na Nachiga kabla ya kufanya mkutano mikubwa Nyamisati na
Kibiti.
Katika mikutano hiyo, Kikwete alimtambulisha pia mke wake, Mama Salma Kikwete na
kwenye mkutano wa Kibiti alimnadi
Mgombea ubunge wa jimbo
'Upinzani kuiona
Ikulu kwa mialiko ya dhifa'
Dk. Sheni asema bado havina hadhi
Na Dunstan Bahai, Tanga
VYAMA vya upinzani bado havijafikia hadhi ya kwenda Ikulu na badala yake wataiona
kwa mialiko maalumu watakayopewa kwa ajili ya kuhudhuria dhifa za kitaifa.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mgombea Mwenza wa Urais wa CCM, Dk. Ali Mohamed Sheni
wakati akihutubia mikutano miwili tofauti katika wilaya za Mkinga tarafa ya
Maramba na Pangani katika ziara ya mkoani hapa inayomalika leo.
Leo anaendelea na ziara yake mkoani Arusha, lakini akiwa njiani kuelekea huko,
kila wilaya atakayopita atasimama kidogo kuwasalimia wananchi.
"Kutokana na kutokuwa na uwezo
kwa vyama vya upinzani, Ikulu watafika
waalikwa wa shughuli maalum
kitaifa," alisema Dk. Sheni huku akishangiliwa na maelfu ya mashabiki, wanachama
na wafurukutwa wa CCM.
Alisema vyama vya upinzani bado ni wachanga, havina uwezo, havina uzoefu, havina
ujuzi, "hata ubwabwa wa shingo haujawatoka," aliongeza.
Dk. Sheni alisema kutokana na amani na utulivu na mafanikio katika huduma za
kijamii kuboreka, hasa katika kipindi cha miaka kumi iliyopita, ili yaendelee
kuboreshwa, wananchi wanaaswa kuichagua CCM.
"CCM itashinda watake wasitake, kwa nguvu ya wananchi. Ushahidi halisi ni katika
uchaguzi wa
kutokana na wananchi kuwa na imani nayo," alisema na kukebehi sera za baadhi ya
vyama vya upinzani kuwa ni za vitisho na kunoa mapanga hali yenye lengo la
kuwagawa Watanzania.
Mgombea mwenza huyo ambaye pia ni Makamu wa Rais, alisema wapinzani wanapanga
mipango mingi kwa kutumia sera za Chama Cha Mapinduzi. "Domo utindi maziwa kwa
mwenye ng'ombe," alitoa msemo huo ambao uliangua vicheko kwa mashabiki
waliohudhuria mkutano uliofanyika Maramba.
Akiwa wilayani Pangani, Dk. Sheni alisema serikali ya awamu ya nne inakusudia
kuwaondolea kero zinazowakabili Watanzania na kwa upande wa wilaya ya Pangani
alibainisha kero kubwa kuwa ni barabara na kivuko.
Dk. Sheni alisema kwa upande wa kivuko, serikali yake itatoa ufumbuzi wa muda
mfupi kwa kununua kivuko kipya na kwamba ufumbuzi wa kudumu utafuatia kwa kujenga
daraja linalounganisha Pangani mjini na kijiji cha Bweni wakati upande wa barabara
alisema upo mradi unaojenga barabara ya kutoka Saadani Bagamyo kupitia Pangani
hadi Horohoro.
Alisema pia kuwa kitajengwa chuo cha ufundi stadi (VETA) ili kuwaandaa vijana
wanaomaliza shule ili waweze kujitegemea.
Mgombea mwenza alisikitishwa na vitendo vya fujo vinavyofanywa na vyama vya
upinzani na kufafanua kuwa kuwepo kwa vyama vingi si fujo bali ni kushindanisha
hoja ambazo zitawashawishi wananchi kujiunga na chama wanachokipenda kulingana na
sera zake.
Akiwa Maramba, Dk. sheni alipokea wanachama 526 kutoka vyama vya upinzani ambao
wamejiunga na CCM. Wanachama hao ni kutoka CUF (405), TLP (56), CHADEMA (30) na
NCCR-Mageuzi (35) wakati Pangani aliwapokea 502 kutoka CUF (380), TLP (62),
NCCR-Mageuzi (48) na CHADEMA (12).
Wanachama hao walifananishwa na mwana mpotevu aliyepotea njia na baada ya kugundua
hali hiyo alirudi haraka nyumbani kwa baba yake.
Rais Mkapa awataka
Majaji, Mahakimu kupiga vita rushwa
Na Mwandishi Wetu
RAIS Benjamin Mkapa
RAIS Benjamin Mkapa amewataka mahakimu na majaji kujenga imani kwa wananchi kwa
kupiga vita rushwa na kukubali kuwajibika kwao.
Hayo yamo kwenye hotuba ya Rais Mkapa aliyoitoa jana kwenye uzinduzi wa majengo ya
'Uwanja wa Haki Iringa' katika hafla iliyofanyika mkoani Iringa na hotuba yake
kupatikana mjini
"
kuwajibika kwao na mpige vita rushwa kwa nguvu zenu zote.
"Si kwamba mahakama ina ukiritimba wa rushwa, la hasha. Lakini rushwa ikijipenyeza
kwenye mahakama ubaya wake unakuwa maradufu maana juhudi za wengine wote kupiga
vita rushwa zitakwama zikifika mahakamani," alisema Rais Mkapa katika hotuba yake.
Rais Mkapa alisema kuna haja ya kuwa waangalifu kwa siku zijazo ili kuwezesha
Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani ziweze kufikiwa na watu wengi kwa maana ya
umbali na gharama.
Alisema kuwa matarajio yake ni kwamba kuwe na Mahakama Kuu katika kila mkoa ili
kuwezesha kila mwananchi kuweza kuitumia huduma ya mahakama hiyo.
Rais Mkapa pia alisema katika mahakama hizo kuna tatizo la gharama ya kutafuta
haki na kuongeza kuwa iwapo gharama hizo itakuwa nje ya uwezo wa mwananchi wa
kawaida basi hataweza kupata haki yake.
Aliongeza kuwa mawakili nao gharama zao zimekuwa kubwa na kuhoji iwapo kuna
wananchi wengi wanaoweza kumudu gharama za mawakili ambazo ni mamilioni ya fedha.
Rais Mkapa alisema katika siku zijazo kuna haja ya kuchangia mawazo ya namna ya
kuwasaidia wananchi ambao wanakosa haki kwa sababu ya unyonge wao na uduni wa
mapato
Kuhusu masuala ya amani, alisema kuwa utawala wa sheria ni jukumu la kila
serikali, kila jamii, kila mtu na kila asasi na kwamba penye utawala wa sheria
hakuna ruhusa kuhalalisha au kufumbia macho uhalifu unaofanywa na vyama vya siasa.
Hakuna uchunguzi
kuhusu uchaguzi Z'bar-SMZ
Na Khatib Suleiman,
Serikali ya Mapinduzi ya
hakuna mwenye uhalali na mamlaka ya kudai kufanyika uchunguzi juu ya uchaguzi huo.
Kauli hiyo ilitolewa hapa jana na Naibu Waziri Kiongozi, na Waziri wa Habari,
Utamaduni na Michezo, Ali Juma Shamuhuna. Alikuwa akizungumza alipokuwa
akimkabidhi ofisi Waziri mpya wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Amina Salum Ali.
Alisema Katiba na sheria za
uchaguzi za
cho chote kuhoji ama kutaka uchunguzi ufanywe juu ya matokeo ya uchaguzi wa Rais.
Alisema Tume ya Uchaguzi ya
urais wa
uwezo wa kuhoji
kimataifa zinavyotaka.
Shamuhuna alisema kitendo cha kudai kufanyika kwa uchunguzi kwenye suala
hakikubaliki.
Alisema kupitiwa tena matokeo ya urais baada ya kutangazwa rasmi na Tume ya
Uchaguzi kwa nafasi za urais, udiwani, na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi,
hakukubaliki.
"Katiba ya
urais wa Zanzbar baada ya kutangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzbar," alisema.
Chama cha CUF ambacho kilishindwa katika uchaguzi mkuu wa
mwaka huu, kimepinga ushindi wa Chama cha Mapinduzi, na kukataa kumtambua rais
halali aliyepo madarakani, Amani Abeid Karume.
Chama hicho kikisaidiwa na baadhi ya nchi na taasisi za nje ya nchi zimekuwa
zikitoa madai ya kutaka kufanyika kwa uhakiki wa kura zilizopigwa katika uchaguzi
mkuu huo, kikidai ili kuondoa 'utata' wa matokeo ya uchaguzi huo.
Shamuhuna alisema matokeo yaliyotangazwa na ZEC ni halali ambapo rais
aliyetangazwa amekwishakula kiapo na kuunda serikali, hatua ambayo inakamilisha
muhimili mmoja wapo wa dola ambao ni serikali.
Alisema kitendo cha Rais Karume kuteuwa baraza la mawaziri, ni kitendo
kinachoashiria kuwepo madarakani na
kutekeleza majukumu yake
inavyoelekeza baada ya kupata ushindi mkubwa.
Shamuhuna alisema Rais Karume ameunda Baraza la Mawaziri zito ambalo limezingatia
uwiano wa uwakilishi mkubwa wa wanawake kwa kuteuwa mawaziri wanne wanawake
akiwemo Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi nchini Zainab Omar ambaye anakuwa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi Maalumu.
Mapema, Waziri Amina Salum Ali aliwataka wafanyakazi na watendaji wa Wizara hiyo
kumpa kila aina ya ushirikiano ambao utafanikisha kutekeleza pamoja na kusimamia
majukumu yake muhimu ya ujenzi wa taifa.
"Ninachokitaka kwenu ni kupata ushirikiano wa kufanikisha majukumu tuliyokabidhiwa
yaliyomo katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi," alisema Amina ambaye
pia ni Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake nchini UWT.
Shahidi adai aliunguzwa matako kwa kuangushwa kwenye sufuria la supu
Na Mwandishi Wetu
SHAHIDI Mariamu Sadick (30), jana alidai mbele ya mahakama ya wilaya ya Ilala kuwa
alipigwa na kuangushwa kwenye sufuria lenye supu ya moto na kuungua matako, paja
na goti.
Mariamu alitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu wa Wilaya Agnes Mchome, katika kesi
inayomkabili mshitakiwa Zena Seleman (41) na Rehema Said (25) wakazi wa Dar es
Salaam.
Alidai washitakiwa walikwenda katika banda la chakula maeneo ya Buguruni na
kurusha matusi ya nguoni kuwa aliiba sahani ya udongo.
Pia, Mariamu alidai washitakiwa walitoa matusi hayo ambapo mmoja wao alimvamia na
kumpiga kisha kumuangusha kwenye sufuria lenye supu ya moto.
"Mheshimiwa walinichangia wote kisha wakaniangusha kwenye sufuria la moto, kweli
niliungua matako, paja la kulia na kwenye goti," alidai Mariamu.
Aliongeza kuwa baada ya kuangushwa kwenye sufuria alitolewa na rafiki yake
aliyemtaja kwa jina la Amina na alikwenda kituo cha Polisi Buguruni.
Mariamu aliongeza kuwa baada ya kufika kituo hapo alipewa cheti cha polisi ambapo
alikwenda kutibiwa katika hospitali
ya Amana,
Washitakiwa hao wanadaiwa Mei 4 mwaka huu, saa tano asubuhi, katika maeneo ya
Buguruni relini, walimuunguza Mariamu katika sufuria lenye supu ya moto na
kumsababishia majeraha katika matako, paja na goti.
Washitakiwa walikana shitaka na wapo nje kwa dhamana hadi Januari 5 mwaka huu
ambapo kesi hiyo itaendelea kusikilizwa.
'Mashina yaunde
vikundi vya kupambana na umaskini'
Na Furaha Omary
MGOMBEA udiwani wa kata ya Dovya, wilayani Temeke amesema mashina ya wakereketwa
wa CCM yatumike kuunganisha vijana katika masuala ya siasa na kuunda vikundi vya
kupambana na umaskini.
Mgombea udiwani huyo alisema hayo wakati wa hafla ya uzinduzi wa shina la
wakereketwa la vijana wa kata hiyo.
Alisema mashina ya wakereketwa wa CCM pamoja na kuhamasisha masuala ya siasa
lazima yawe na mipango ya maendeleo ili kujikwamua katika umaskini.
Aliongeza kuwa mashina hayo pia yawe ya vijana wenye itikadi
wasaidie kuimarisha chama na kupambana na wanasiasa uchara bila kuyumbishwa.
Mgombea huyo wa udiwani, alisema maneno yanayotolewa na wanasiasa 'uchwara' ni ya
uongo na lengo
"Sikatai uchaguzi wa 2000 niliahidi kukamilisha ujenzi wa barabara, ikiwa ni moja
ya mambo niliyoyaahidi, lakini bado nina uwezo wa kukamilisha ujenzi huo katika
kipindi kijacho," alisema Mwakasindile
Katika hafla hiyo, vijana wa kata hiyo walimuhakikishia ushindi wa 'kishindo' na
kumtaka awe mlezi wa shina
Shina
wanajishughulisha na masuala mbalimbali ikiwemo muziki.
Mwakasindile aliwahakikishia vijana hao kuwawezesha kimuziki kwa kukiuza uchumi wa
nchi kutokana na shughuli zao katika kikundi hicho.
Ujumbe wa Chama cha Kikomunisti
Na Mwandishi Wetu
UJUMBE wa watu 48 kutoka Chama cha
Kikomunisti cha
nchini jana usiku kwa ziara ya siku mbili ambapo pamoja na mambo mengine leo
utakuwa na mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula, yatakayofanyika
hoteli ya Movenpick.
Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya
Katibu Mkuu wa CCM jijini
jioni, ilisema ujumbe huo unaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Kamati ya
Siasa ya Chama , Li Changchum.
Mazungumzo kati ya ujumbe huo na Katibu Mkuu wa CCM, Mangula, yanatarajiwa kuanza
saa tatu asubuhi.
Viongozi waandamizi wa CCM , Makamisaa wa CCM ndani ya serikali na baadhi nya
maofisa na makada wa CCM wamealikwa kwenye mazungumzo hayo.
Sh. milioni 500 kukamilisha barabara ya Dabiri
Na Serafina Sungusia, Babati
SHILINGI milioni 500 zinahitajika kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa barabara ya
mlima Dabiri kwenda Bashnet wakati sh. milioni 290 zimetumika kuunganisha nishati
ya umeme kata ya Bashnet wilayani Babati mkoani hapa.
Akizungumza na wakazi wa Dareda, kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Jumamosi
eneo la Seloto, mgombea ubunge jimbo la Babati vijijini kwa tiketi ya CCM, Damas
Nakei, alisema fedha hizo zinahitajika ili kuunganisha eneo dogo lililobaki kutoka
mlimani hapo hadi Bashnet mjini.
Alisema fedha hizo zitatoka kwenye Mfuko wa Barabara katika bajeti ya mwaka wa
fedha 2006-2007 na zitamalizia kazi hiyo zitakapotolewa.
Eneo la mlima huo lenye urefu wa kilomita saba, limekuwa korofi kwa muda mrefu na
tayari lilishafanyiwa matengenezo ya awamu ya kwanza yaliyogharimu sh. milioni
120. Lami hiyo ilidumu kwa miaka miwili kutokana na magari ya tani zaidi ya 10
kuitumia.
Agosti mwaka huu ukarabati wa barabara hiyo ulianza tena kwa kiwango cha juu zaidi
ili kukidhi matumizi ya magari ya mizigo na ya abiria na unategemea kukamilika
mwezxi ujao ambapo utagharimu sh. milioni 480.
Nakei alisema matengenezo ya awamu zote mbili zinaishia eneo
ndio sababu kabla hajanga'atuka kwenye bunge aliiomba serikali kuongeza fungu kwa
ajili ya kuunganisha barabara hiyo hadi Bashneti mjini na kuepuka uharibifu.
Ukarabati wa eneo la mlima huo unafanywa na kampuni mbili moja ikiwa ya ushauri
Crowtech Consaltant na kampuni ya ukandarasi MECCO zote za jijini Dar es salaam na
utawawezesha wanaosafirisha abiria na magari ya mzigo kutumia dakika 30 badala ya
saa tatu na nusu katika eneo
Wakazi wa eneo
unaotarajiwa kuwashwa wakati wowote kuanzia sasa uliogharimu sh.milioni 290
kuvutwa kutoka Dareda hadi kwenye transfoma iliyopo Bashnet umbali wa kilomita 13.
Wakazi hao waliema kuwa watanufaika na huduma hiyo muhimu na wataweza kumudu
gharama ya kuendesha viwanda vyao vidogovidogo ambapo awali walikuwa wanatumia
jenereta na kujikuta wakipata hasara kwenye biashara zao.
Cheyo ahojiwa na polisi kwa maneno ya uchochezi
MWENYEKITI wa Chama cha United Democratic Party (UDP), John Cheyo, anahojiwa na
polisi mjini hapa akituhumiwa kushawishi maasi dhidi ya serikali.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi mkoani
hapa, Abdallah Mssika, alisema mwenyekiti huyo anahojiwa kufuatia kutoa kauli
kadhaa ambazo zinaweza kuchochea ghasia katika jamii. Cheyo anawania ubunge
Bariadi Mashariki.
Alitaja baadhi ya kauli hizo ni ‘polisi kukiona cha moto Desemba 14, wakiyagusa
masanduku ya kura’ na kundi la 'Tela 9', linalodaiwa kuwa limeandaliwa kwa
madhumuni ya kutekeleza azma hiyo ya 'watakiona cha moto'.
Pia, anatakiwa kueleza ni lini alifanya mazungumzo na Inspekta Jenerali wa Polisi
nchini (IGP), Omar Mahita,
nchini (siyo Uhuru).
Kamanda Mssika alisema polisi inahitaji ufafanuzi na mfano hai ni lini imeshiriki
kuiba kura kwa lengo la kukilinda CCM, na kuvigandamiza vyama vya upinzani.
Kwa mujibu wa Kamanda Mssika, kwenye mahojiano ya awali yaliyofanyika kati yake na
Cheyo, juzi, alizikana kauli hizo akidai kuwa vyombo vya habari vimepotosha kwa
kumnukuu tofauti na kauli zake halisi.
Katika tukio la msingi, Kamanda Mssika alisema Cheyo anadaiwa kutamka hadharani
kauli hizo za uchochezi kwenye mkutano wa kampeni za ubunge, za mgombea wa
Shinyanga Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo- CHADEMA, Bob
Makani, Novemba 20, mwaka huu.
Mssika alisema endapo atashindwa kutoa ufafanuzi wa kuridhisha wa kauli hizo zenye
mwelekeo wa kuleta vurugu katika uchaguzi mkuu wa Desemba 14, atafikishwa
mahakamani kukabiliana na sheria za uchochezi.
Wazazi wenye watoto
walemavu waaswa kutowaficha
Na Pendo Mangala,
WAZAZI wenye watoto walemavu wameshauriwa kuacha kuwaficha na kuona aibu
kuwapeleka watoto wao katika vituo vya kulelea watoto hao.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa
Mkoa wa
alipozungumza na wazazi wenye watoto walemavu, walioshiriki katika mashindano ya
michezo mkoani hapa na Marekani. Hafla hiyo ilifanyika ofisi ya mkuu wa mkoa mjini
hapa.
Alisema watoto walemavu wana haki sawa ya kupata huduma
muhimu za kijamii
walivyo watoto wasio na ulemavu.
Nkhangaa alisema baadhi ya wazazi ambao wana watoto wenye ulemavu wamekuwa wakiona
aibu na kuwaficha watoto wao, na mbaya zaidi hushindwa kuwapeleka katika vituo
maalum vya kuwalea na kuwakosesha mahitaji muhimu ya kijamii.
Aliwataka wazazi hao kuwapeleka watoto wao katika vituo hivyo ili wapate haki zao
za msingi.
Mkuu huyo wa mkoa alisema kumficha mtoto mwenye ulemavu ni sawa na kumpinga
Mwenyezi Mungu, kwani yeye ndiye anayepanga mipango mbalimbali, hivyo waridhike na
hali ya ulemavu waliyonayo watoto wao.
Alisema baadhi ya watoto wenye ulemavu ambao wamekuwa wakiwapeleka watoto wao
wenye ulemavu katika vituo hivyo hupatiwa huduma muhimu za kijamii ambazo ni
elimu, chakula pamoja na mavazi
ambapo baadhi
kutokana na malezi wanayoyapata vituoni humo.
Hata hivyo, alisema serikali itakuwa bega kwa bega na watoto wenye ulemavu
mbalimbali ili kuweza kuhakikisha wanapata huduma hizo muhimu za kijamii.
Jumla ya watoto wapatao 10 wenye ulemavu toka katika vituo vya Miyuji Cheshire,
Mlezi pamoja na Chinangali
vilivyopo Mkoani
dhahabu, fedha,
CBE sasa kufungua
tawi jipya mkoani Mwanza
Na Mwandishi Wetu
CHUO cha Elimu ya Biashara nchini (CBE) kinatarajia kufungua tawi jipya mkoani
Mwanza ili kupanua utoaji elimu kwa wanafunzi wanaopenda masomo ya biashara.
Hayo yalielezwa jana na Mkuu wa Chuo hicho, Serivanus Hyera alipokuwa akizungumza
na waandishi wa habari ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40 tangu kuanzishwa
kwa chuo hicho.
Hyera alisema idadi ya wanafunzi wanaojiunga na masomo ya biashara imekuwa
ikiongezeka kila mwaka hivyo uongozi umeona kuna umuhimu wa kufungua tawi lingine
mjini Mwanza ili kusaidia wanafunzi wa eneo la Kanda ya Ziwa.
Mbali ya hatua hiyo, Hyera alisema katika kuimarisha chuo hicho, mwishoni mwa wiki
hii wanatarajia kupata kompyuta mpya 150.
Kuhusu matatizo yanayowakabili, Hyera alisema ni pamoja na uhaba wa majengo kwa
ajili ya madarasa ya wanafunzi.
Hata hivyo, alisema chuo kina mpango wa kujenga madarasa mengine juu ya majengo
yaliyopo sasa ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na uhaba wa madarasa.
Alisema lingine linalosababisha usumbufu kwa wanafunzi ni ukosefu wa mabweni na
kuwa kutokana na wingi wa madarasa inakuwa vigumu kuwapatia wanafunzi wote sehemu
za kulala.
Madhimisho ya miaka 40 ya CBE yanaendelea leo kwa semina kuhusu mambo mbalimbali
ya biashara katika viwanja vya
Karimjee jijini
Jumamosi ijayo wakati wa mahafali ya 40 ya wanafunzi wa chuo hicho.