SAFARI
Na
WATU wa kale walituachia misemo
mingi, ambayo
Moja ya misemo ya kale ambayo imebaki kuwa na mafundisho makubwa hata katika maisha ya sasa ni ule usemao: “Tembea uone”.
Ngwe yangu ilikuwa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa, yaani Tabora, Shinyanga na Mwanza pamoja na sehemu kadhaa za mkoa wa Morogoro.
SAFARI INAANZA
Ilikuwa safari nzuri, kwani
Kesho yake, yaani Oktoba 7, tulianza safari yetu kwenda Tabora kupitia barabara ya Manyoni na Itigi. Ni barabara ya vumbi, lakini inayopitika katika kipindi chote cha mwaka. Imo katika mkakati wa kuijenga kwa kiwango cha lami.
Tulifika mjini Tabora majira ya jioni na
kisha kumsubiri mgombea wa CCM, Kikwete ambaye alikuwa anafika kesho yake kwa
ndege akitokea jijini
Kimsingi, tulimaliza kampeni za mikoa ya Tabora na Shinyanga kwa mafanikio makubwa, na kisha kuingia mkoani Mwanza.
Kikwete alianza kampeni za mkoa huo kwa
kuhutubia jimbo la Sumve, baada ya kupokewa eneo la Malya mkoani Shinyanga, na
kisha kwenda Kwimba, jimbo atokalo
Baada ya kumaliza mkutano wa
kampeni katika jimbo
Asubuhi, msafara uendelea hadi Busega, jimbo linalowaniwa na Dk. Raphael Chegeni, ambako Kikwete alifanya mkutano wa kampeni. Baada ya hapo tukwenda Geita kupitia kivuko cha Busisi na Sengerema.
Kivukoni hapo, tulikuta maandamano makubwa ya vijana
waliokuwa kwenye mitumbwi
Mitumbwi hiyo ilikuwa ikienda sambamba na pantoni iliyokuwa imembeba Kikwete na msafara wa wake hadi ng’ambo ya pili, ambako pia tulikuta umati mkubwa wa wananchi ukimsubiri.
Baada ya kuwasalimia, msafara huo ulielekea moja kwa moja Geita bila kusimama Sengerema. Tulikwenda hadi uwanja wa michezo ambako tulikuta umati wa watu ukisubiri, ambako alihutubia. Hiyo ilikuwa Oktoba 14.
SAFARI YA
Alipomaliza mkutano wa kampeni hapo, tulilala na kesho yake asubuhi, tulianza safari ya kwenda Mwanza mjini kupitia Sengerema ambako Kikwete alifanya mkutano.
Mkutano huo ulipomalizika, ndipo safari ya kuelekea Mwanza ilipoanza kupitia kivuko cha Busisi hadi njia panda ya Busagara katika barabara kuu itokayo Shinyanga, tulikokuta umati mkubwa wa wananchi ukitusubiri hapo.
Mbali na mamia ya wananchi waliokuwepo hapo kumlaki Kikwete, pia kulikuwa na zaidi ya magari 100, pikipiki na baiskeli lukuki.
Tuliondoka njia panda ya Busagara saa 6.30 mchana na kupita katika vitongoji vya Buhongwa, Nyegezi, Mkuyuni, Igogo hadi Soko Kuu la mjini Mwanza na kisha kuingia barabara ya Nyerere ambako kulikuwa na maelfu kwa maelfu ya wananchi wakimshangilia Kikwete.
Msafara uliondoka eneo
TUNAINGIA
Nje ya uwanja wa CCM Kirumba kulikuwa na watu ambao idadi yake si rahisi kuielezea, ambao bila shaka, hao walishindwa kuingia ndani kutokana na uwanja huo wakati huo kuwa umejaa pomoni.
Tulipoingia ndani ya uwanja huo, ndipo nilipoelewa nguvu ya Chama cha Mapinduzi na mgombea wake wa nafasi ya Urais. Umati ule ndani ya uwanja huo ni ushahidi tosha kwamba uteuzi wa CCM ulikuwa sahihi.
Umati wa watu uliokuwemo ndani ya uwanja huo wa CCM Kirumba ulikuwa mkubwa kupita kiasi, kwani kwenye maeneo ya kukaa, hakukuwa hata na nafasi ya mtu kutema mate!
Katikati ya uwanja kulikuwa na
umati mwingine mkubwa wa watu, ambao idadi
Hata hivyo, msafara wa Kikwete baada ya kuzunguka uwanjani huku akiwapungia wananchi, hatimaye ulifika jukwaani ambapo alishuka na kwenda kukaa kwenye jukwaa kubwa, shughuli za burudani zilianza kwa vikundi mbalimbali kuburudisha wananchi.
Walioanza kutoa burudani uwanjani hapo lilikuwa kundi la
Wanaume (TMK Wanaume) chini ya kiongozi wao,
Baada ya tukio
Miongoni mwa waliosalimia ni pamoja
na
Kataraia pia aliwatambulisha viongozi wengine wa CCM, wakiwemo wajumbe wa
Baadaye ndipo lilipofuata tendo la mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Kikwete kutawazwa kuwa Chifu wa Wasukuma.
Kikwete alishuka kutoka katika jukwaa kubwa alipokuwa ameketi na kwenda katikati ya uwanja ambako kulikuwa kumejengwa majukwaa mengine mawili, moja kwa shughuli hiyo ya kumtawaza na lingine kwa ajili ya kuhutubia.
Wakati akitoka jukwaani kwenda kwenye majukwaa hayo, Kikwete
alifuatana na baadhi ya viongozi wa Chama, ambapo huko
aliwakuta baadhi ya wazee wa Kisukuma waliomtawaza kuwa Chifu wa kabila
Kikwete alipandishwa jukwaani na kuketishwa kwenye kigoda. Wakati shughuli hiyo ikiendelea, ndipo kijana aliyekuwa amevalia mgolole mweusi, alipomvamia Kikwete na kuukumbatia mguu wake wa kulia akitaka kumdondosha chini kutoka jukwaani alipokuwa ameketi kwenye kigoda!
Kutokana na ushupavu wake, Kikwete aliweza kujinasua kutoka mikononi mwa yule kijana, na wakati huo huo ndipo kijana huyo ‘aliposhukiwa’ na kundi la zaidi ya askari 30 waliokuwa wamezunguka jukwaa alilokuwepo Kikwete.
Kusema kweli, kitendo hicho kilitokea katika muda wa sekunde chache, kiasi kwamba wapo baadhi ya watu waliokuwemo uwanjani humo hawakujua nini kilichokuwa kimetendeka.
Kutokana na jinsi kijana yule alivyokuwa amevalia, haikuwa rahisi kwa wanausalama au kwa mtu yeyote kumshuku kwamba alikuwa amedhamiria kuleta fadhaa ile pale uwanjani.
Kijana yule, mbali na kupewa mkong’oto wa nguvu, alizolewa na kuchukuliwa juu kwa juu na askari polisi walimpakia kwenye karandinga na kumpeleka kituo kikuu cha polisi mjini Mwanza anakoendelea kuhojiwa zaidi.
Hata hivyo, baada ya tukio
SAFARI YA MAHENGE
Baada ya Kikwete kumaliza kuhutubia mkutano huo wa kampeni ambao rekodi yake haijawahi kutokea katika mikutano yake hapa nchini, sisi waandishi tulitakiwa kuondoka mjini Mwanza jioni ile kuelekea Mahenge wilayani Ulanga.
Kimsingi, Kikwete alikuwa hajamaliza ziara yake ya mkoa huo,
kwani kesho yake asubuhi alikuwa amepangiwa kwenda wilayani Ukerewe ambako
alikuwa na mkutano mwingine wa kampeni. Jimbo
Tuligawanywa katika makundi mawili. Moja ni la waandishi ambao wangeandamana na mgombea kwenda Ukerewe na wengine kuelekea Mahenge, ili kumpokea keshokutwa yake, yaani Oktoba 17, ambako angemalizia ‘kiporo’ cha wilaya za Ulanga na Ifakara, mkoani Morogoro.
Msafara wa magari yaliyokuwa
yamepangwa kwa safari ya Mahenge yalikuwa saba, yakiwemo manne yaliyokuwa
yamewabeba waandishi wa habari na wapigapicha. Safari ilianza
Kwa mujibu wa mkuu wa msafara,
Ilikuwa safari ngumu, iliyohitaji uvumilivu wa hali ya juu, kwani tukiwa Nzega usiku huo wapo walioamua kutolala kabisa kwa kuhofia kwamba iwapo wangejilaza tu, basi ingekuwa vigumu kuamka!
Hata hivyo, kwa wale waliolala
ilikuwa
Kulipopambazuka tu, safari ilianza na msafara ulianza kwa ari, nguvu na kasi mpya hadi Singida ambapo watu walipata chai ya asubuhi kabla ya kujipakia tena na kuendelea na safari hadi njia panda ya Kilosa eneo la Dumila tulipofika saa 11.00 hivi.
Mkuu wa msafara aliamuru kwamba
safari inaendelea kwenda Mikumi kupitia njia panda hiyo, ambayo kusema kweli
japokuwa barabara ilikuwa siyo mbaya, lakini kutokana na uchovu, na kwamba
barabara ilikuwa ya vumbi tulijikuta tunafika Mikumi
Watu walipata chakula cha jioni hapo Mikumi na kisha kuendelea na safari hadi Ifakara, ambako tulifika saa 7.00 usiku. Ilikuwa safari ngumu, lakini yenye hamasa kubwa, huku ikifungua milango zaidi ya fahamu na jiografia.
Tuliendelea na safari hadi
kivukoni, ambako tulivuka Mto Kilombero kwa pantoni saa 7.30 usiku na kisha
kuelekea Mahenge, umbali wa zaidi ya Kilometa 100.
Hata hivyo, safari ilikuwa kwenda kwenye kijiji cha Mwaya,
ambako kuna uwanja mdogo wa ndege katika Hifadhi ya
Taifa ya Selous, ambako Kikwete angewasili asubuhi yake akitokea Musoma mkoani
Mara kupitia
Kadri muda ulivyokuwa ukienda ndipo wananchi wa kijiji hicho walivyokuwa wakimiminika uwanjani hapo, huku vikundi mbalimbali vya kwaya na ngoma za Umoja wa Vijana wa CCM vikiburudisha wananchi waliofika uwanjani.
Tulikaa hapo mpaka karibu saa sita mchana, ndipo ndege ndogo iliyombeba Kikwete ilipotua katika uwanja huo na shamrashamra za wananchi na wana-CCM zilipopamba moto na kisha msafara wa kuelekea Mahenge katika mji wa Ulanga zilipoanza.
Tulifika Ulanga kama saa nane hivi mchana ambako alihutubia mkutano mkubwa wa kampeni ikiwa ni pamoja na kumnadi mgombea wa jimbo hilo la Ulanga Mashariki, Celina Kombani na baadaye Ulanga Magharibi kwa Dk. Juma Ngasongwa katika mji wa Lupiro.
Baadaye tulirudi Ifakara kupitia kivukoni ambako nako
alifanya mkutano wa kampeni na kumnadi mgombea wake,
Castory Ligalama na baada ya hapo tukarudi Kidatu tulipoingia majira ya
Hiyo ndiyo safari ya waandishi wa
habari za kampeni za mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Kwa maneno mengine, unaweza kusema tulisafiri usiku, mchana, usiku, mchana bila kulala! Hata hivyo, ni safari niliyojifunza mengi, na kwa kweli mambo niliyoyaona sitayasahau kamwe maishani mwangu.
Pia, safari hiyo imepanua mno jiografia yangu kwa kufika maeneo na sehemu ambazo, nisingeweza kuota
kuzifika katika maisha yangu,
Lakini kubwa zaidi, nimeshuhudia jinsi Chama cha Mapinduzi kilivyojichimbia na kuweka mizizi hadi katika maeneo ya vijijini kabisa. Ni wapi utakwenda nchini hapa ukose kuona bendera ya CCM ikiwa inapepea?
Hii inadhihirisha pia kwamba
IDD Azzan: Mgombea ubunge wa jimbo la Kinondoni anayefananishwa na Kikwete
Wengi jimboni waonyesha kuwa na imani naye
ARI mpya, Nguvu mpya na Kasi Mpya
ni kaulimbinu iliyoasisiwa na
IDD Azzan si jina geni masikioni mwa wakazi wa Kinondoni, kwani limekuwa likivuma zaidi kwa wale wafuatiliaji wa karibu wa masuala ya michezo.
Lakini baada ya kuwika na kwa kweli
kusaidia
Anawania ubunge katika jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwa kwa upande mmoja ameiva katika kushughulikia matataizo ya wananchi, kwa kuwa inasadikiwa kuwa michezoni ni pahala ambako ni lazima mtu awe shupafu ndiyo anaweza kumudu kuiendeleza michezo.
Licha ya kuwa kiongozi wa Soka, Azzan pia ni diwani wa kata ya Magomeni ambapo wakazi wengi wa kata hiyo, wamepata maendeleo makubwa kwa kuweza kutatua matatizo yaliyokuwa yakiikabili kata hiyo.
Kukubalika kwa Azzan kunatokana na ucheshi wake alionao miongoni mwa jamii inayomzunguka, pia ni kiongozi asiye na ‘majigambo’ machoni mwa watu.
Kubwa zaidi hivi karibuni alitambulishwa kwa
wananchi wa jimbo la Kinondoni katika mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye
uwanja wa
‘KIKWETE’ JUNIOR
Wakati akipanda jukwaani wananchi wengi walimshangilia kwa ‘mbwembwe’ na nyimbo mbalimbali huku wengi wakimuita ‘Kikwete junior’ kutokana na mvuto alionao kwa kufananishwa naye.
Pamoja na kumtambulishwa machoni
mwa maelfu ya wananchi waliokusanyika katika mkutano huo,
”Ndugu wana CCM wenzangu, nachukua nafasi hii kumtambulisha
kwenu mdogo wangu, rafiki yangu wa siku nyingi,
“Azzan ninamfahamu kwa muda mrefu
hata
Hata hivyo, katika mikutano yake ya hivi karibu aliyofanya katika maeneo mbalimbali ya Kinondoni, Azzan alisema kwamba atahakikisha wananchi wanapata maisha bora kwa kuboresha miundo mbinu iliyopo kwa kuzingatia Ilani ya CCM.
Ushindi kwa
Pamoja na hayo, Azzan anasema
kwamba tatizo la maji kwa baadhi ya maeneo ya Kinondoni yatakwishwa ambapo hadi
sasa Serikali ya
Hali hiyo inatokana kuwepo kwa maisha bora kwa kila Mtanzania ambayo mgombea ameahidi kukamilisha. Azzan amekuwa na nyota ya kupendwa na watu wa kila rika si kwa vijana tu bali pia wazee pamoja na kina mama kutoka maeneo mbalimbali ya Kinondoni.
UONGOZI WAKE
Suala la uongozi kwa Azzan halina mjadala kwa kuwa watu wengi wanamfahamu tangu akichochea maendeleo ya soka, hadi kuchaguliwa kuwa diwani katika kata ya Magomeni.
Mgombea huyu amekuwa mstari wa mbele katika kufanikisha mandeleo kwa wakazi wake na hii inatokana kuwepo kwa misingi bora na imara ya uongozi.
Miaka mitatu iliyopita Azzan alipitishwa kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi alipokuwa nje ya nchi kwa shughuli zake. Hii inaonyesha ni jinsi gani anavyokubalika.
Azzan pamoja na mambo mengine, ameahidi kufanya mambo mengi makubwa ya maendeleo kwa wananchi ikiwemo uboreshaji wa zahanati, vituo vya afya, elimu na mifereji ambalo ni tatizo kubwa kwa wakazi wa Kinondoni wakati wa mvua.
Kuhusu michezo Azzan anasema atahakikisha vijana wapenda soka wanapatiwa vifaa bora vya michezo katika kuendeleza soka la ‘bongo’ ambalo litakua katika chati ndani na nje ya nchi.
“Kwa nini
Akinguruma kwenye mkutano wa
kampeni uliofanyika hivi karibuni katika tawi la Kwa Biyuda, kata ya
Mgombea huyu wa CCM pia, ni mwanzilishi wa timu ya Veterani (Tanzania Stars), ambayo iliiwakilisha nchi katika mashindano makubwa ya Kombe la Washindi barani Afrika kwa miaka miwilimfululizo 1997 hadi 1998.