UCHAGUZI WA VIONGOZI WA VITONGOJI, MITAA NA SERIKALI ZA
VIJIJI, TANZANIA BARA, 2004
(Mada iliyowasilishwa na Mhe. Brig. Jen. (Mstaafu) Hassan Ngwilizi (Mbunge, Naibu Katibu Mkuu,
CCM, kwenye Semina ya Wajumbe wa NEC, Wenyeviti na Makatibu wa Mikoa na Wilaya iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Chimwaga Dodoma, tarehe 24/8/2004)
UTANGULIZI:
1. Mwaka
huu utafanyika Uchaguzi katika ngazi za vijiji, mitaa na vitongoji. Kama ilivyokuwa kwa chaguzi zilizotangulia
za mwaka 1993 na 1999, uchaguzi wa mwaka
huu utafanyika kwa kuzingatia mfumo wetu wa demokrasia ya vyama vingi
vya siasa ambao unazingatia mambo yafuatayo:
·
Ushindani wa
kidemodrasia wa vyama vya siasa;
·
Utawala wa kikatiba na
kisheria;
·
Misingi ya kijamii
ambapo wananchi ndio msingi wa mamlaka yote ya Serikali;
·
Ustawi wa wananchi;
·
Uwajibikaji wa Serikali
kwa wananchi; na
·
Ushirikishwaji wa
wananchi katika shughuli za Serikali.
·
Kuanzishwa kwa Mfumo wa
Vyama vingi vya siasa;
·
Kutungwa sheria za
kusimamia uendeshaji wa vyama vingi vya
siasa;
·
Kutungwa sheria na/au
kurekebishwa kwa sheria zilizopo kusimamia uchaguzi chini ya mfumo wa vyama
vingi vya siasa;
·
Kuwa na utaratibu
unaotoa haki kwa kila raia kushiriki katika kupiga kura na katika kuchaguliwa
katika nafasi za uongozi.
4. Mabadiliko
hayo yaliweka mazingira mazuri ya kuendesha uchaguzi wa ngazi mbalimbali ikiwa
ni pamoja na ngazi za vijiji, mtaa na vitongoji. Uchaguzi katika ngazi ya
vijiji, mitaa chini ya mfumo wa vyama vingi vya siasa ulifanyika kwa mara ya
kwanza mwaka 1993 na kurudiwa mwaka 1999.
Chaguzi zote 2 yaani uchaguzi
wa mwaka 1993 na uchaguzi wa mwaka 1999 uliendeshwa kwa mafanikio ya kuridhisha
kwa vile ulitoa fursa kwa vyama vya siasa kushiriki kwa
haki; uhuru na demokrasia licha ya kutokuwepo kwa
uzoefu wa kutosha.
5. Sheria
zinazoongoza uchaguzi wa Serikali za Mitaa zimegawanyika katika makundi mawili
makubwa. Kundi la kwanza, ni Sheria ya
Uchaguzi katika Serikali za Mitaa The Local Authoririties Election Act. No.
4 of 1979 ambayo inahusika na uchaguzi wa Madiwani. Uchaguzi wa kundi hili utafanyika mwaka kesho 2005 pamoja na Uchaguzi
Mkuu wa Rais na Wabunge. Kundi la pili,
ni Sheria za Serikali za Mitaa yaani sheria na. 7 na 8 za 1982, ambazo
zinaongoza uchaguzi katika ngazi ya vijiji, mitaa na vitongoji. Uchaguzi wa kundi hii ndio utafanyika mwezi
Novemba mwaka huu.
6. Chini
ya Sheria za Serikali za Mitaa na 7 na 8 za 1982, Waziri Mwenye Dhamana na
Serikali za Mitaa amepewa madaraka ya kutunga kanuni zitakazoongoza uchaguzi
katika ngazi ya kijiji, mtaa na kitongoji.
7. Maandalizi
muhimu kwa uchaguzi wa mwaka huu yameanza na yanaendelea vizuri. Kanuni za uchaguzi za mwaka 1999 zimefanyiwa
mapitio na kanuni mpya zitakazoongoza uchaguzi wa mwaka huu zimeandaliwa. Rasimu za kanuni hizo zimetangazwa kwenye
magazeti na kutolewa maoni na mapendekezo katika mikutano ya wadau wafuatao:
·
Vyama Vyote vya Siasa
Vyenye Usajili wa Kudumu.
·
Wakuu wa Mikoa na
Makatibu Tawala wa Mikoa.
·
Wakuu wa Wilaya na
Makatibu Tawala wa Wilaya.
·
Jumuiya ya Tawala za
Serikali za Mistaa, Tanzania - ALAT.
·
Halmashauri zote,
Tanzania Bara.
·
Wananchi kwa ujumla.
8.
Maoni na mapendekezo
yaliyotolewa yamegawanyika katika mafungu mawili makubwa:
Moja ni maoni na mapendekezo yanayolenga kuziboresha
kanuni. Mbili ni maoni na mapendekezo
ambayo yakikubaliwa itabidi uchaguzi uahirishwe hadi hapo mabadiliko yatakapofanyika
katika Katiba na Sheria mbalimbali.
9. Kanuni
zimefanyiwa marekebisho mbalimbali yanayozingatia maoni na mapendekezo
yaliyotolewa.Maoni na mapendekezo yanayohitaji marekebisho ya katiba na sheria
yamepokelewa na yatafanyiwa kazi kwa utaratibu tofauti. Zogo linaloendelea kutoka kwa wapinzani
linatokana na madai ya kutaka mapendekezo yao ya kurekebisha katiba na sheria
mbalimbali yatekelezwe kwanza kabla ya uchaguzi wa mwaka huu kufanyika, jambo
ambalo halikubaliki kwa vile litavuruga ratiba ya uchaguzi mkuu wa Rais,
Wabunge na Madiwani.
Misingi
ya kisheria ya kutunga Kanuni za Uchaguzi katika ngazi ya Kijiji, Mtaa na
Kitongoji:
10. Sheria za Serikali za Mitaa na. 7 na 8 za
mwaka 1982 kama zilivyorekebishwa ndizo zinazohusika na uanzishaji na uendeshaji
wa vyombo vya Serikali za Mitaa katika vitongoji na vijiji katika maeneo
ya vijijini na katika mitaa katika
maeneo ya mijini. Katika hali hiyo,
kifungu cha 30 (4) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) Na. 7 ya
mwaka 1982 kinaelekeza kuwa kila kitongoji kitakuwa na Mwenyekiti ambaye atachaguliwa na Mkutano wa
wakazi wa Kitongoji. Kifungu cha 14 (4)
cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Na. 8 ya mwaka 1982
kinaelekeza kuwa kila Mtaa utakuwa na Mwenyekiti na Kamati yenye wajumbe
wasiozidi 6 na wajumbe wasiopungua wawili ni lazima wawe wanawake. Mwenyekiti na wajumbe wa Kamati ya Mtaa
watachaguliwa na Mkutano wa Wakazi wa Mtaa.
11.
Kwa
upande wa Kijiji, Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) katika
kifungu cha 25 inaelekeza kuwa kila kijiji kitakuwa na Halmashauri ya Kijiji.
Kifungu cha 56 (1) kinaelekeza kuwa Halmashauri ya Kijiji itakuwa na wajumbe
wasiopungua 15 na wasiozidi 25 kama ifuatavyo:
(a)
Mwenyekiti
wa kijiiji atakayechaguliwa na Mkutano Mkuu wa Kijiji.
(b)
Wenyeviti
wa Vitongoji katika Kijiji.
(c)
Wajumbe
wengine watakaochaguliwa na Mkutano Mkuu wa Kijiji wakiwemo wanawake ambao
idadi yao haitapungua robo ya wajumbe wote wa Halmashauri ya Kijiji.
12. Sheria imempa Waziri Mwenye Dhamana ya
Serikali za Mitaa jukumu la kuandaa Kanuni zitakazofuatwa katika kuwachagua
viongozi wa Vitongoji, Mitaa na Serikali za Vijiji. Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kitongoji zimetungwa chini ya
kifungu cha 30 (4) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) Na. 7 ya
mwaka 1982. Kanuni za Uchaguzi wa
Mwenyekiti na Kamati ya Mtaa zimetungwa chini ya kifungu cha 70 (c) cha Sheria
ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) Na. 8 ya mwaka 1982. Kanuni za Uchaguzi wa Halmashauri ya Kijiji
zimetungwa chini ya kifungu cha 56 (3) cha Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka
za Wilaya) Na. 7 ya mwaka 1982.
Misingi iliyozingatiwa Katika
Kutunga Kanuni:
13. Ipo misingi ya Kikatiba, Kisheria na
Kiutawala ambayo imezingatiwa katika kutunga Kanuni hizi. Misingi hiyo ni pamoja na:
·
Kutumia
demokrasia katika kuwapata viongozi ambao kweli ni wawakilishi wa wananchi;
·
Kutoa
fursa kwa kila mwananchi kushiriki katika kuchaguliwa kuwa kiongozi na pia
katika kuchagua viongozi;
·
Kurahisisha
utaratibu wa uchaguzi;
·
Kuepuka
gharama zisizo za lazima.
·
Kuwa
na utaratibu wa uchaguzi ulio wazi na wa haki wenye kumwezesha mgombea kukata
rufaa ikiwa atakuwa na malalamiko dhidi ya mwenendo wa uchaguzi.
·
Kuhakikisha
uchaguzi unakuwa huru na wa haki.
·
Kuhakikisha
kwamba kwa kutumia demokrasia tunampata kiongozi mwadilifu na anayezingatia
maadili ya utawala bora.
14. Vile vile ipo misingi iliyozingatiwa ili
kuhakikisha kuwa uchaguzi katika ngazi ya Vijiji, Mitaa na Vitongoji unakuwa wa
haki, huru na wa kidemokrasia. Misingi
hiyo ni pamoja na:
·
Kuwepo
kwa mfumo madhubuti wa uandikishaji wa wapiga kura, kama ibara ya 5 ya Katiba
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyoelekeza. Misingi hiyo ni pamoja na kuhakikisha uandikishaji wa wapiga
kura, kuwepo kwa taratibu rahisi za uandikishaji n.k.
·
Kuwepo
kwa utaratibu mzuri wa uandikishaji wa vyama vya siasa na wagombea, ambapo
vyama vinakuwa na uhuru wa kuteua wagombea kwa kuzingatia katiba za vyama vyao.
·
Kuwepo
kwa uhuru wa vyama na wagombea kufanya mikutano ya kampeni ambayo inaendeshwa
bila vitisho, fujo, woga na njia nyingine za vitisho.
·
Kuwa
na utaratibu mzuri wa kupiga kura na kutangaza matokeo ya uchaguzi. Chini ya utaratibu huu lazima kuwepo na
mahali pa kufaa pa kupigia kura ambapo panafikika na wapiga kura wote. Vile vile utaratibu wa kupiga kura lazima uhakikishe
kwamba kura zinahesabiwa na kutangazwa katika mikutano ya uchaguzi na hati za
matokeo zimetolewa na kuthibitishwa na wasimamizi wa uchaguzi mbele ya wagombea
au wawakilishi wao.
·
Kuwepo
kwa uhuru wa wagombea na vyama vya siasa na vyombo vya habari wa kujieleza;
·
Kuwepo
kwa uhuru wa kupata taarifa kuhusu uchaguzi na uendeshaji wake ikiwa ni pamoja
na kanuni na taratibu zinazotumika.
·
Kuwepo
uhuru wa kuuliza na kupeleka malalamiko na haki ya kukata rufaa endapo taratibu
hazikufuatwa.
MAPITIO YA KANUNI ZA UCHAGUZI KATIKA NGAZI YA KIJIJI,
MTAA NA KITONGOJI
Uandikishaji Wapiga
Kura:
15. Kama ilivyo kawaida ya uchaguzi wowote inafaa kuwa na kumbukumbu
za wapiga kura katika kila Kitongoji, Kijiji na Mitaa. Rasimu za kanuni zinaweka utaratibu wa
kuandaa orodha ya wapiga kura katika uchaguzi wa viongozi wa umri wa miaka 18
au zaidi na wenye sifa za kupiga kura.
Utaratibu utakaotumika wa kuandaa orodha hiyo ya wapiga kura ni tofauti
na ule unaotumika katika uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani.
16. Chini ya kanuni hizi uandaaji wa orodha
ya wakazi wa vijiji, mtaa na vitongoji itafanywa na Maafisa Watendaji wa Kata
na Vijiji. Utaratibu utakaotumika sio
wa wakazi kwenda katika vituo kujiandikisha kama ilivyo kwa uchaguzi wa Rais,
Wabunge na Madiwani bali ni kwa maafisa husika kuwaandikisha wapiga kura
(compilation) kutoka katika Daftari la Wakazi wa Kijiji, Mtaa au Kitongoji na
kutoa fursa kwa pingamizi endapo kuna mkazi hakuandikishwa au asiyestahili
ameandikishwa.
17. Yapo mapendekezo na madai kwamba uchaguzi
wa vijiji, mitaa na vitongoji uahirishwe ili utaratibu wa Daftari la Kudumu la
Wapiga Kura ndio utumike badala ya utaratibu uliofafanuliwa. Zipo sababu za kimsingi za kuendelea kutumia
utaratibu tulioufafanua. Kwanza
uchaguzi katika ngazi ya kijiji, mtaa na kitongoji unafanyika katika mikutano
ya wakazi hivyo wananchi wote wanajuana.
Pili, kumbukumbu za kudumu za wakazi husika zipo katika madaftari ya
wakazi wa vijiji, mitaa na vitongoji, ambayo ndio yatatoa orodha ya wapiga
kura. Tatu, wakazi wa maeneo husika
watapata fursa ya kutoa pingamizi ili kuhakikisha kwamba watakaopiga kura ni
wale tu wenye sifa na wanaostahili.
Mwisho, endapo uchaguzi utaahirishwa ili kusubiri Daftari la Wapiga Kura
utakuwa na athari kubwa katika ratiba
ya uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani
Mipaka ya Vijiji, Mitaa na
Vitongoji:
18 Jukumu la kuandikisha wakazi wa vijiji,
mitaa na vitongoji ili washiriki katika mikutano ya uchaguzi linakwenda
sambamba na suala la kuweka na kutangaza majina na mipaka ya maeneo husika.
Kila Mkurugenzi anapaswa kutangaza majina na mipaka husika ili itambulike sio
tu kwa wasimamizi bali pia kwa wakazi wa kawaida wa vijiji, mitaa na
vitongoji. Jukumu la kuweka mipaka hii
ni la Halmashauri husika. Kabla ya
kuandikisha vijiji na kuweka mgawanyo wa vitongoji na kugawa kata za mijini
katika mitaa, Halmashauri husika inapaswa kuweka na kutunza kumbukumbu ya
mipaka ya maeneo husika. Kanuni
zinawaelekeza Wakurugenzi kutangaza kwa majina, mipaka na maeneo ya vijiji,
mitaa na vitongoji wakati wa uchaguzi ili iweze kufahamika kwa wasimamizi,
wagombea na wakazi wa maeneo husika.
HATUA ZA AWALI YA UCHAGUZI:
19. Waziri
Mwenye Dhamana ya Serikali za Mitaa atatoa tangazo la uchaguzi kwa umma
katika magazeti ya Kiswahili na Kiingereza siku 90 kabla ya siku ya uchaguzi.
Maelekezo
ya Uchaguzi:
20. Baada
ya Tangazo la Waziri, Mkurugenzi wa Halmashauri atatoa maelekezo kuhusu
uchaguzi siku 28 kabla ya siku ya uchaguzi itakayotaja masuala yafuatayo;-
(a)
Tarehe ya kufanyika
mikutano ya uchaguzi;
(b)
Tarehe, muda na mahali
pa kufanyika mikutano ya uchaguzi (ambayo itafanyika muda wowote kati ya saa
2.00 asubuhi na saa 10 jioni).
(c)
Kuwataka wakazi wote
wenye sifa za kupiga kura wahudhurie mkutano wa uchaguzi siku ya uchaguzi;
(d)
Kuwataka wakazi wenye
umri wa miaka 21 au zaidi
wanaotaka kugombea nafasi za uongozi
katika kijiji, mtaa na kitongoji wajaze fomu za kugombea zinazopatikana kwenye
ofisi za msimamizi msaidizi wa uchaguzi.
(e)
Tarehe na muda wa
kuchukua na kurudisha fomu za maombi ya
kugombea uongozi kwa msimamizi wa uchaguzi na kuagiza kwamba muda wa kuchukua
na kurudisha fomu za kugombea hautazidi siku (7).
(f)
Siku ambayo uteuzi
utafanyika na mahali pa matangazo ambapo fomu za wagombea zitabandikwa ili
wapiga kura wazione;
(g)
Muda wa kutoa pingamizi
dhidi ya uteuzi na kusikilizwa kwa pingamizi;
(h)
Tarehe ya kusikiliza
rufaa dhidi ya uamuzi wa msimamizi msaidizi wa uchaguzi;
(i)
Kipindi cha kuendesha
mikutano ya kampeni za uchaguzi ambacho hakitazidi siku saba na masuala
mengineyo yanayohusiana na uchaguzi.
Sifa
za Wapiga Kura:
21. Watu
watakaoruhusiwa kushiriki katika uchaguzi wa viongozi wa vijiji, mitaa na vitongoji ni wale tu wenye sifa
zifuatazo:
(a) Raia wa
Tanzania;
(b)
Wakazi wa kawaida wa
eneo linalohusika (kitongoji/mtaa/kijiji);
(c)
Wenye umri wa miaka 18
au zaidi;
(d)
Wasio na ugonjwa wa
akili.
Sifa
za Wagombea:
22. Wagombea
wa nafazi zote za uongozi katika kitongoji, mtaa na kijiji wanatakiwa kuwa na
sifa zifuatazo:
(a)
Wawe raia wa Tanzania;
(b)
Wawe wametimiza umri wa
miaka 21 au zaidi;
(c)
Wawe na kipato halali
cha kuwawezesha kuishi;
(d)
Wawe na uwezo wa
kuandika na kusoma Kiswahili au Kiingereza;
(e)
Wawe wanachama na
wadhaminiwa wa vyama vya siasa vilivyosajiliwa kwa mujibu wa sheria;
(f)
Wawe wakazi wa kawaida
wa maeneo yanayohusika (kitongoji/mtaa/kijiji);
(g)
Wasiwe wanadaiwa kodi
yoyote ya Serikali Kuu au Serikali za Mitaa;
(h)
Wasiwe wamehukumiwa na
Mahakama yoyote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kupewa adhabu ya kifo
au kifungo cha miezi 6 au zaidi kwa makosa ya jinai.
(i)
Wasiwe na ugonjwa wa akili.
23. Pengine itakuwa vema kutoa ufafanuzi wa
kisheria ya
baadhi ya sifa za wagombea na wapiga kura:
(i)
Raia wa Tanzania: Ibara ya 5 ya Katiba ya jamhuri ya Muungano
wa Tanzania inaelekeza kwamba raia yeyote wa Tanzania anaweza kushiriki katika
uchaguzi wowote kama mpiga kura au
mgombea wa nafasi ya uongozi. Ili mtu
yeyote aweze kuipata haki ya kikatiba ni sharti awe raia wa Tanzania kwa mujibu
wa Sheria ya Uraia, (The Citizenship Act No. 6 of 1995).
Sheria ya Uraia The Tanzania Citizenship Act. No.
6 of 1995 inatambua aina zifuatazo za kupata uraia wa Tanzania:
(a)
Raia wa Tanzania kwa
Kuzaliwa:
Sheria ya Uraia kifungu cha 5 inaelekea kwamba mtu
yeyote aliyezaliwa Tanzania siku ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar atakuwa
raia wa Tanzania endapo wazazi au mojawapo wa wazazi wake ni raia wa Tanzania.
(b)
Uraia wa Tanzania
kwa tajinsi (nasturalization)
Kwa mujibu wa kifungu cha 9(1)
cha Sheria ya Uraia, raia wote wa kigeni wanaoishi nchini wanaweza kuomba
kutangazwa kuwa raia wa Tanzania.
(c)
Uraia
kwa kuandikishwa:
Sheria ya auraia inatambua vile
vile kupata uraia kwa kuomba kuandikishwa.
(ii)
Mkazi
wa kawaida wa eneo husika:
Neno mkazi wa kawaida limefafanuliwa
kisheria katika kanuni hizi. Aya ya
ufafanuzi inaelekeza kwamba mkazi ni raia wa Tanzania mwenye kaya au anayeishi
katika kaya iliyopo katika eneo husika.
Hata hivyo kwa madhumuni ya kanuni
hizi mkazi yeyote atakuwa na haki ya kugombea nafasi ya uongozi au kupiga kura
katika Kijiji, Mtaa au Kigongoji kimoja tu.
24. Utaratibu wa uteuzi:
Kanuni za uchaguzi katika ngazi ya
Kijiji, Mtaa na Kitongoji zinaelekeza utaratibu ufuatao wa uteuzi:-
·
Siku
ya uteuzi:- Msimamizi wa uchaguzi
atafanya uteuzi wa wagombea siku
zisizopungua kumi na tano (15) kabla ya tarehe ya uchaguzi.
·
Uteuzi
utafanywa kutokana na fomu zilizowasilishwa;
·
Baada
ya uteuzi msimamizi wa uchaguzi atabandika mahali pa matanagazo majina ya wagombea wenye sifa na wasio na
sifa za kugombea nafasi za uongozi katika ngazi ya kijiji, mtaa na kitongoji.
·
Ikiwa
hakuna mwombaji hata mmoja aliyejitokeza au waombaji wote waliojitokeza au
kumetokea kifo au sababu nyingine yoyote basi utaratibu wa uteuzi
utarudiwa; ambapo msimamizi wa uchaguzi
atatengua uteuzi na kupanga tarehe nyingine ya uchaguzi ambayo sio zaidi ya
siku 10 tangu tarehe ya kutengua uteuzi uliofanyika.
·
Pingamizi
dhidi ya uteuzi: Pingamizi kwa
kuteuliwa au kutoteuliwa mgombea litawasilishwa kwa msimamizi msaidizi wa
uchaguzi masaa 24 tangu uteuzi ulipofanyika ili kumtaka akangalie upya uamuzi
wake na kutoa uamuzi katika muda wa siku 2 tangu siku ya kupokea pingamizi;
Kamati ya Rufaa:
25. Kanuni zinaelekeza kwamba kutakuwepo na
kamati ya rufaa ambayo jukumu lake ni kusikiliza malalamiko ya uteuzi wa
uchaguzi katika kila Halmashauri.
Kamati hii ya Rufaa itateuliwa na kupewa maelekezo na Katibu Tawala wa
Mkoa na itajumuisha wajumbe wafuatao:-
(i)
Katibu
Tawala wa Wilaya ambaye atakuwa Mwenayekiti;
(ii)
Viongozi
wawili (2) wa dini kutoka madhehebu tofauti ambao watateuliwa na Katibu Tawala
wa Mkoa baada ya kupokea mapendekezo kutoka madhehebu yaliyomo katika eneo la
Halmashauri.
(iii)
Afisa wa umma kutoka
eneo la Halmashauri husika atakayeteuliwa na Katibu Tawala Mkoa.
(iv)
Katibu ambaye
atateuliwa na Katibu Tawala Mkoa kutokana na maafisa wa umma waliopo katika
eneo la Halmashauri husika.
Utaratibu
wa Kampeni za Uchaguzi:
26. Mgombea au mtu yeyote aliyeruhusiwa na
mgombea au Chama cha Siasa cha mgombea anaruhusiwa kuitisha na kuhutubia
mikutano ya kampeni itakayofuata ratiba zilizoratibiwa katika utaratibu
ufuatao:
·
Kampeni zitaanza siku
moja baada ya siku ya uteuzi wa wagombea na zitamalizika siku moja kabla ya
siku ya uchaguzi.
·
Mgombea , chama cha
siasa, au mwakilishi wa mgombea wataandaa na kuwasilisha kwa msimamizi wa
uchaguzi ratiba ya kampeni za uchaguzi.
·
Ratiba za mikutano ya
kampeni ambayo imeratibiwa na msimamizi wa uchaguzi, zitakuwa taarifa rasmi za
mikutano ya kampeni na zitawasilishwa kwa Jeshi la Polisi ili kuhakikisha
ulinzi na usalama katika mikutano hiyo ya kampeni za uchaguzi.
Siku ya Uchaguzi:
27.
Kazi
ya kwanza ya mkutano wa uchaguzi itakuwa ni kumchagua mjumbe mmoja ambaye siyo
mgombea wa nafasi yoyote, kuwa Mwenyekiti wa muda wa mkutano huo. Baada ya kuchagua Mwenyekiti mpangilio wa
uchaguzi utaendelea kwa utaratibu ufuatao:
(a)
Kwanza utafanyika
uchaguzi wa Wajumbe wa Kamati ya Mtaa/Halmashauri ya Kijiji kutokana na kundi
la wagombea wote, wanawake na wanaume.
(b)
Kura zitahesabiwa ili
wagombea wanawake ambao hawatapita waweze kuingia katika uchaguzi wa kundi la
viti maalum;
(c)
Utafanyika uchaguzi wa
viti maalum vya wajumbe wanawake.
(d)
Mwisho utafanyika
uchaguzi wa Mwenyekiti wa Mtaa/Kijiji.
Kwa upande wa uchaguzi wa kitongoji utafanyika
uchaguzi wa Mwenyekiti wa kitongoji tu.
Utaratibu
wa Uchaguzi:
28. Uchaguzi wa Mwenyekiti utakuwa kama
ifuatavyo:-
·
Iwapo mgombea wa nafasi
ya Mwenyekiti wa Kitongoji, Mtaa au Kijiji ni mmoja tu, basi atapigiwa kura za
siri za NDIYO au HAPANA na ikiwa kura za NDIYO zitakuwa zaidi ya nusu ya
kura zilizopigwa basi atatangazwa kuwa Mwenyekiti.
·
Ikiwa kura za NDIYO
zitakuwa chini ya nusu ya kura zilizopigwa basi utaratibu wa uchaguzi utaanza
upya (yaani kutangaza tarehe mpya ya uchaguzi, kujaza fomu, kufanya uteuzi
n.k.).
·
Endapo hakuna mgombea
hata mmoja aliyejitokeza au kama wagombea wote waliojitokeza hawana sifa
zinazostahili kugombea utaratibu wote wa uchaguzi utaanza upya.
·
Endapo baada ya kupiga
kura wagombea wawili au zaidi watakuwa wanaongoza kwa kura sawa, kura zitapigwa
tena kwa wale wagombea ambao kura zao zitakuwa zimefungana.
29. Uchaguzi
wa nafasi za Wajumbe:
·
Kama idadi ya wagombea
wa nafasi za ujumbe wa Halmashauri ya kijiji au Kamati ya Mtaa itakuwa chache
kuliko au italingana na nafasi zinazohitaji kujazwa, basi wagombea watatangazwa
kuwa wamechaguliwa.
·
Ikiwa idadi ya wagombea
itakuwa kubwa kuliko nafasi zinazohitaji kujazwa, kura za siri zitapigwa na
watakaopata kura nyingi watatangazwa kuwa wajumbe wa kamati ya Mtaa/Halmashauri
ya Kijiji.
30. Kuhesabu kura na kutangaza matokeo:
Kura zitahesabiwa na Msimamizi wa Uchaguzi mbele ya
wagombea au wawakilishi wao ikiwa watataka kushuhudia zoezi hilo, na matokeo ya
uchaguzi yatatangazwa mkutanoni kwa kuanza na wajumbe wa Kamati ya Mtaa
/Halmashauari ya Kijiji na kumalizia na Mwenyekiti wa Kamati ya Mtaa/Mwenyekiti
wa Kijiji.
31. Malalamiko ya uendeshaji wa uchaguzi:
Mgombea yeyote ambaye hakuridhika na uendeshaji wa
uchaguzi atakuwa na haki ya kupeleka malalamiko yake mahakama ya wilaya katika
muda wa siku 30 baada ya siku ya kutangaza matokeo ya uchaguzi.
32. Kiapo
na uwajibikaji wa wasimamizi wa uchaguzi:
Wasimamizi wa uchaguzi watatakiwa kula kiapo cha
uaminifu na kutunza siri kabla ya kuanza kutekeleza majukumu yao. Kanuni zinaelekeza pia kwamba msimamizi
atakayekiuka kanuni za uchaguzi atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatia
atapewa adhabu ya faini ya shs. 50,000/= au kifungo cha miezi 12 au vyote faini
na kifungo.
33. Watizamaji
wa Ndani:
Kanuni zinatoa fursa kwa watizamaji wa ndani ili
kuhakikisha kwamba uchaguzi ni wa haki, huru na kidemokrasia.
34. Makosa
ya Uchaguzi:
Kanuni zinaorodhesha makosa
yafuatayo ya uchaguzi. Adhabu ya kila kosa itakuwa faini ya shs. 50,000/= au
kifungu kwa muda usiozidi miezi kumi na mbili (12).
·
Kuharibu orodha ya
wapiga kura;
·
Kutoa taarifa za uongo
kuhusu makazi;
·
Kuharibu karatasi ya
wagombea;
·
Kugushi karatasi za
uteuzi;
·
Kupiga kura mara mbili;
·
Kutishia wapiga kura au
wagombea ili kuvuruga uchaguzi;
·
Kuonyesha ishara au
mavazi yanayoashiria kumtambulisha mgombea na chama chake cha siasa siku ya
uchaguzi;
·
Kumzuia msimamizi wa
uchaguzi kutekeleza majukumu yake;
·
Kukiuka masharti ya
kiapo;
·
Kutenda jambo lolote
linalokiuka kanuni hizi.
35. Uchaguzi
Mdogo:
Nafasi za uongozi huwa wazi kutokana
na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kifo, kujiuzulu, kukosa sifa za
kuendelea kuwa kiongozi n.k. Mara tu zitokeapo nafasi hizi ni lazima zijazwe
ili kuendeleza haki ya uwakilishi ya wakazi wa eneo husika. Kanuni zinaelekeza kwamba Mkurugenzi
atatangaza kutokea kwa nafasi wazi baada ya kupokea taarifa kutoka kwa
Halmashauri ya Kijiji au Kamati ya Mtaa.
Baada ya tangazo la Mkurugenzi nafasi wazi itajazwa katika muda wa siku
60 tangu kutangazwa. Uchaguzi mdogo
utaendeshwa kwa utaratibu unaotumika kwa uchaguzi wa kawaida.
HOJA ZILIZOJITOKEZA KATIKA KUJADILI RASIMU ZA KANUNI ZA UCHAGUZI
KATIKA NGAZI YA KIJIJI, MTAA NA KITONGOJI:
36. Hoja, maoni na mapendekezo yafuatayo
yalijitokeza katika kujadili Rasimu ya Kanuni hizi:
(a)
Uandikishaji
wa wapiga kura katika uchaguzi wa vijiji, mitaa na vitongoji uzingatie Daftari
la Kudumu la Wapiga Kura
37. Daftari la Kudumu la Wapiga Kura
litakaloandaliwa na Tume ya Uchaguzi halitatumika kwa ajili ya Uchaguzi katika
ngazi ya Vijiji, Mitaa na Vitongoji kwa sababu zifuatazo.
·
Daftari la Kudumu la
Wapiga Kura linatumika kwa kuzingatia masharti ya Katiba na Sheria ya Uchaguzi
na 1 ya 1985 na 4 ya 1979 ambazo zinaelekeza kwamba daftari hilo litatumika
kuandikisha wapiga kura kwenye uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani na sio
katika uchaguzi wa viongozi wa vijiji, mitaa na vitongoji.
·
Uchaguzi wa viongozi wa
mitaa, vitongoji na vijiji husimamiwa na Serikali za Mitaa nazo zina Daftari la
kumbukumbu muhimu kuhusu maeneo hayo ya vijiji, mitaa na vitongoji. Daftari hilo ndilo litatumika kupata orodha
ya wapiga kura katika uchaguzi wa viongozi wa vitongoji, mitaa na vijiji.
·
Uchaguzi wa viongozi wa
mitaa, vijiji na vitongoji inafanyika katika mikutano ya wakazi wa maeneo
husika. Wakazi wa maeneo hayo wanajuana
hivyo utaratibu uliowekwa kwenye kanuni wa kuandaa orodha ya wapiga kura kwa
kushirikisha wananchi unafaa na utaepusha migogoro isiyo ya lazima.
·
Daftari la kudumu la
wapiga kura bado halijakamilika na endapo litatumika athari yake ni kuahirisha
uchaguzi, jambo ambalo litavuruga ratiba ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na
Madiwani unaotarajiwa kufanyika mwaka 2005.
(b)
Uchaguzi wa
Viongozi wa Vijiji, Mitaa na Vitongoji Kusimamiwa na Tume Huru ya Uchaguzi
Badala ya Usimamizi Chini ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa.
38. Uchaguzi
wa viongozi wa mitaa, vitongoji na vijiji husimamiwa na mamlaka za Serikali za
Mitaa husika yaani Mkurugenzi wa
Halmashauri ambamo uchaguzi huo unafanyika akisaidiwa na Watendaji wa kata au
kijiji wala siyo watumishi wa Makao
Makuu ya OR-TAMISEMI. Utaratibu huu
umewekwa ili kukidhi matakwa ya ibara ya 146 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano
inayotoa jukumu kwa Vyombo Vya Serikali za Mitaa kusimamia demokrasia katika
eneo lake. Ibara hiyo inaelekza kama ifuatavyo:
146. (1) Madhumuni ya kuwapo Serikali za Mitaa ni
kupeleka madaraka kwa wananchi. Vyombo vya Serikali za Mitaa vitakuwa na
haki na mamlaka ya kushiriki na kuwashirikisha wananchi katika mipango na
shughuli za utekelezaji wa maendeleo katika sehemu zao na nchini kote kwa jumla.
(2) Bila ya kuathiri
maelezo ya jumla yaliyomo katika ibara ndogo (i) ya ibara hii, hiki chombo cha
Serikali za Mitaa, kwa kuzingatia masharti ya sheria iliyokianzisha, kitahusika
na shughuli zifuatazo:
(a)
Kutekeleza
kazi za Serikali za Mitaa katika eneo lake;
(b)
Kuhakikisha
utekelezaji wa sheria na ulinzi wa wananchi; na
(c)
Kuimarisha
demokrasi katika eneo lake na kuitumia demokrasi kuharakisha maendeleo ya
wananchi.
39. Jukumu hili
la kusimamia uchaguzi ni la kiutendaji. Kazi ya
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa ambayo ina Dhamana ya Serikali za Mitaa, kwa mujibu wa Sheria
za Serikali za Mitaa ni kuweka tu Kanuni ya namna uchaguzi huo utakavyoendeshwa
na si vinginevyo.
40. Sambamba na hoja hiyo, ipo minongono
kwamba Wakurugenzi wa Halmashauri wana utii kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa
na Serikali za Mitaa, kwa kuwa ndiyo inayowateua. Uteuzi wa Wakurugenzi sio wa kisiasa bali unafanywa kwa misingi
ya stahili (meritiocracy) kama sera ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma
inavyoelekeza.
41. Uchaguzi huu hausimamiwi na Tume ya
Uchaguzi kutokana sababu zifuatazo.
·
Uchaguzi
huu unafanyika kwenye ngazi ya mtaa, kijiji au kitongoji. Katika kitongoji wakazi wote waliopo
wanafahamiana. Hii ni tofauti na
uchaguzi wa kitaifa ambapo wagombea wanaweza kupigiwa kura kutoka kwenye maeneo
ambayo hawakuzaliwa na hawaishi na hawafahamiki. Ni kwa sababu hii kwamba katika ngazi ya kitaifa wanahitaji
chombo maalum kitakacho hakikisha kwamba haki zao zinalindwa.
·
Kikatiba,
jukumu la Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni kusimamia uchaguzi wa Rais, Wabunge na
Madiwani, na jukumu la kusimamia uchaguzi katika vijiji, vitongoji na mitaa
limepewa vyombo vya Serikali za Mitaa katika ngazi hizo husika.
·
Sababu
nyingine ni ile haja ya kuzingatia uwezo wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kufanya
jukumu hili kwa ufanisi. Kwa mfano, kwa
uchaguzi wa Wenyeviti wa Vijiji, vitongoji na mitaa, idadi ya wagombea kutoka
vyama vya siasa kumi na sita vyenye usajili wa kudumu kama vitasimamisha
mgombea mmoja mmoja tu kutoka kila chama kutakuwa na wagombea karibu 1,500,000
ambao kwa uchache husimamiwa na watumishi 12,721 wa Serikali za
Mitaa. Watumishi hawa wamepatiwa
mafunzo, wana utendaji wenye maadili ya Serikali na wanaweza kuwajibishwa. Kwa kuzingatia hali kama hii, ni dhahiri
kuwa huu utakuwa ni mzigo mkubwa kwa Tume kuweza kuuhimili. Kinachotakiwa ni kuwepo kwa utaratibu utakaowezesha
uchaguzi kufanyika kwa haraka, kwa urahisi na wenye kuzingatia demokrasia na
haki.
Mwisho:
42. Viongozi
wa vitongoji, mitaa na serikali za vijiji ni muhimu sana katika mfumo wa
utawala wa nchi yetu. Utawala bora
umejengwa katika ngazi hii. Jambo
lingine ambalo pia ni muhimu ni kwamba uongozi madhubuti katika ngazi hii ndio
utakaosaidia katika kudumisha umoja na mshikamano wa Taifa letu na hivyo
kutuwezesha kuwa na maendeleo ya kweli na yenye kudumu.
KIAMBATISHO A
KAZI ZA MWENYEKITI WA KITONGOJI KWA
MUJIBU WA TARATIBU ZILIZOTUNGWA CHINI YA KIFUNGU CHA 112 CHA SHERIA YA SERIKALI
ZA MITAA (MAMLAKA ZA WILAYA) NA. 7 YA MWAKA 1982
(i)
Kuitunza rejesta ya Wakazi wa
Kitongoji na habari nyingine muhimu zinazohusu maendeleo ya Kitongoji kwa Jumla
ikiwa ni pamoja na kumbukumbu za vizazi na vifo.
(ii)
Kusimamia ulinzi na usalama wa
watu na mali za wanaoishi katika eneo lote la Kitongoji.
(iii)
Kuhamasisha ulipai wa Kodi na
ushuru mbali mbali, kama utakavyoamuliwa na kuwekwa mara kwa mara na
Halmashauri ya Wilaya.
(iv)
Kusimamia katika eneo lake suala
zima la Hifadhi ya Mazingira hususan vyanzo vya maji n.k.
(v)
Kusimamia suala zima la Afya
katika eneo lake ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Kampeni za afya za Kitaifa,
Kimkoa au Kiwilaya dhidi ya magonjwa ya kuambukiza.
(vi)
Kusimamia utekelezaji wa Taratibu
za Kilimo na Ufugaji bora ili kuinua hali ya lishe na uchumi wa wakazi wa
Kitongoji.
(vii)
Kufuatilia na kuhakikisha kuwa
kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule anapoatiwa nafasi, na kushirikiana na
viongozi wa shule katika kudhibiti utoro shuleni.
(viii)
Kuhamasisha Elimu ya Watu Wazima.
(ix)
Kusimamia na kuwahamasisha wakzi
wa Kitongoji katika kutekeleza shughuli za kujitegemea.
(x)
Kusuluhisha migogoro midogo
isiyostahili kushughulikiwa na Mabaraza ya Kata au Mahakama.
(xi)
Kuwakilisha Kitongoji katika
Serikali za Kijiji.
(xii)
Kuwaongoza na kuwahamasisha wakazi
wa Kitongoji washiriki katika Sherehe za Taifa na mikutano ya hadhara
itakayoandaliwa na kuitwa na Serikali au Halmashauri.
(xiii) Kutekeleza kazi nyingine atakazopangiwa na Halmashauri ya Wilaya.
KIAMBATISHO B
KAZI ZA MWENYEKITI
WA KITONGOJI KWA MUJIBU WA TARATIBU ZILIZOTUNGWA CHINI YA KIFUNGU CHA 56 CHA
SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA MIJI) NA. 8 YA MWAKA 1982
(i)
Kutunza rejesta ya wakazi wote wa
Mtaa na habari nyingine muhimu
zinazohusu maendeleo ya Mtaa kwa Jumla ikiwa ni pamoja na kumbukumbu za
vizazi na vifo.
(ii)
Kusimamia ulinzi na usalama wa
watu na mali za wanaoishi katika eneo
la Mtaa.
(iii)
Kusuluhisha migogoro midogo
isiyostahili kushughulikia na Mabaraza ya
Kata au Mahakama.
(iv)
Kuhamisha ulipaji wa kodi na
ushuru mbalimbali kama utakavyoamuliwa na kuwekwa mara kwa mara na Halmashauri
ya Mji, Manispaa au Jiji.
(v)
Kusimamia suala zima la Afya
katika eneo lake ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Kampeni za afya za Kitaifa,
Kimkoa au Kiwilaya dhidi ya magonjwa ya kuambukizwa.
(vi)
Kusimamia uwekaji wa eneo la Mtaa
katika hali ya usafi.
(vii)
Kushirikiana na Halmashauri ya
Mji, Manispaa au iji kudhibiti
bughudha.
(viii)
Kufuatilia na kuhakikisha kuwa
kila mtoto mwenye unri wa kwenda shule anapata nafasi ya kushirikiana na
viongozi wa shule katika kudhibiti utoro.
(ix)
Kuhamaisha elimu ya watu wazima.
(x)
Kusimamia na kuhamasisha wakazi wa
Mtaa katika shughuli za kujitegemea.
(xi)
Kuwaongoza na kuwahamasisha wakazi
washiriki katika sherehe za Taifa na mikutano ya hadhara itakayoandaliwa na
Serikali au na Halmashauri.
(xii)
Kuwakilisha Mtaa kwenye Kamati ya
Maendeleo ya Kata.
(xiii)
Kutekeleza kazi nyingine
atakazopangiwa na Halmashauri ya Mji, Manispaa au Jiji.
KIAMBATISHO C
DAFTARI LA ORODHA A WAKAZI WENYE UMRI WA MIAKA 18 NA KUENDELEA
KITONGOJI/MTAA
KIJIJI
KATA
|
NA. |
JINA LA MKAZI |
JINSIA (KE/ME) |
UMRI |
TAREHE YA KUANDIKI-SHWA |
SAHIHI YA ANAYEANDI-KISHWA |
SAHIHI YA MWANDI-KISHAJI |
|
|
|
|
|
|
|
|
KE =
Mwanamke
ME = Mwanamme