USHINDI WA CCM UKO
WAZI WAZI
Hakukosea hata kidoga mgombea urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
tiketi ya Chama Cha Mapinduzi ndugu Jakaya Mrisho Kikwete aliposema kwamba
ushindi kwa CCM ni wa asilimia 90. Ni dhahiri ndugu Kikwete alikuwa na sababu
za msingi aliposema maneno hayo mbele ya umati mkubwa wa wananchi wa mjini Sikonge
mkoa wa Tabora tarehe 9/10/2005. Na ni dhahiri kuwa watanzania walio wengi
wanaamini ya kwamba CCM ndicho chama bora kuliko vyama vingine vyote vya siasa.
Kielezo kimoja wapo cha nguvu na umakini wa Chama Cha Mapinduzi ni wingi na
ubora wa makada wake. Chama Cha Mapinduzi kina kila sababu ya kujivunia ubora
wa mtaji huu. Tunapokiongelea Chama Cha Mapinduzi tunaongelea itikadi, malengo
na sababu sahihi za Chama kikubwa na chenye historia inayotukuka. Na kamwe sio nasaba na umaarufu wa mtu mmoja
mmoja ndani ya chama kama vilivyo vyama vya upinzani hapa nchini. Tunaamini ya
kwamba hakuna hata mwananchi mmoja mwenye uelewa wakutosha atakayethubutu
kukipa kura ya ndiyo chama ambacho muhimili wake ni mtu mmoja kwani kwa kufanya
hivyo atakuwa ameiweka nchi yetu rehani na katika hatari ya kupelekwa katika
kiza kinene cha mapungufu ya mtu huyo. Kwa mantiki hiyo basi tuna hakika ya ushindi
wa asilimia 90 na pengine hata zaidi. Aidha, Chama Cha Mapinduzi kimesheheni
wagombea wenye kutambua na kuyajali matatizo ya wananchi. Na kwa kuwa itikadi
na malengo ya CCM vinalenga katika kuwaletea maendeleo ya kweli wananchi wa
Tanzania ndio maana CCM ina kila sababu za kujiamini.
Wagombea udiwani, ubunge na urais wa Chama Cha Mapinduzi hata uwaamshe saa
nane usiku watakuambia historia, madhumuni, itikadi, malengo, na hata mwelekeo
wa Ilani ya Chama chao. Uelewa na umakini huu wa Makada wa CCM ni jambo nadra kulikuta
kwa wagombea wa vyama vya upinzani. Udhaifu na mapungufu haya kwa viongozi wa
vyama vya upinzani, utatufanya tuwe na mashaka kuhusu mwelekeo wa vyama hivyo.
Ndiyo maana tunakila sababu ya kuamini kuwa vyama vya upinzani vinalenga kuitumbukiza
nchi yetu katika machafuko.makubwa. Mapungufu haya ya viongozi wa vyama vya
upinzani ya kushindwa hata kuelewa vema vyama vyao, haiyumkini ndiyo sababu ya
viongozi hao kushindwa kuweka mipaka kati ya siasa zinazolinda maslahi ya
Tanzania za amani, utulivu, na maendeleo na saiasa za chuki na vurugu. Imekuwa
ni tabia kwa wapinzani kutumia hamasa hasi za wafuasi wao kuendesha kampeni kwa
njia ya vitisho, vurugu na kusababisha maafa.
Haingii akilini hata kidogo kwa ngombea uraisi katika nchi yenye misingi
imara ya amani na utulivu kama Tanzania kunukuliwa na waandishi wa vyombo vya
habari kuwa ameacha kugombea ubunge kwa sababu hapendi namna mawaziri wanavyojibu
maswali ndani ya bunge. Je mtu huyo akiwa rais si tunaweza kusikia siku moja
amewaondoa pasipo kufuata mantiki ya hoja na sheria mawaziri wake kwenye kikao
kwa sababu wametofautiana hoja? Hii itasababisha uvunjifu wa amani na kujenga
hofu kwa mawaziri na hata watendaji wengine wa serikali. Watanzania tupo tayari
kuilinda amani ya nchi yetu hivyo ni dhahiri kuwa hatutamchagua mtu anayeongozwa
na utashi binafsi kuwa rais. Ndiyo maana tunaamini kuwa CCM itashinda kwa
kishindo.
Wapinzani bado ni dhaifu mno na wakati mwingine huwa hawatambui cha
kuwafanyia watanzania. Ndio maana hata katika kampeni zao badala ya kuelezea
sera zao, hutumia muda mwingi kukikashfu Chama Cha Mapinduzi, na hata
kuwadanganya wananchi kwa kuwapa taarifa za uongo. Mfano, yuko mgombea ambaye
aliwaeleza wananchi kuwa Baba wa Taifa ndiye alitoa wosia kwa CCM kwamba
watanzania wasipewe elimu wala fursa za kujiendeleza kiuchumi, kwamba itakuwa
ni vigumu kwa CCM kutawala wasomi na matajiri. Mgombea huyu kamwe hana hofu ya
Mungu. Anasahauu kuwa wananchi wanajua fika kuwa CCM imekuwa na sera nzuri na
zinazotekelezeka kuhusu elimu na uwezeshwaji kiuchumi wa mtu mmoja mmoja tangu
vyama asisi vya TANU/AFRO-SHIRAZ. Na kiashiria kikubwa cha kukubalika na
kuaminika kwa CCM hata kabla ya uchaguzi tayari ina Wagombea wasiopungua 8 wa
ubunge na madiwani wanaozidi 120 wa CCM wamekosa upinzani. Kadiri tunavyoelekea
ukikongoni, vyama vya upinzani watazidi kuingia mitini. Hakika CCM itashinda
kwa kishindo 2005.
Ushindi wa kishindo wa Chama Cha Mapinduzi unathibitishwa zaidi na matokeo ya
uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika Novemba 2004 ambapo CCM ilionesha
kuwa ni maji ya kina kirefu ambacho hakipimwi kwa miguuu miwili. Katika
uchaguzi huo Chama cha Mapinduzi kilijizolea ushindi wa siyo chini asilimia 96
na kuwaacha wapinzani wakiwa hoi bin taaban. Kwa kuwa ni wananchi walewale ndio
watakopiga kura kuchagua rais, wabunge na madiwani, hapana shaka ushndi kwa CCM
ni utakuwa katika kiwango cha uwiano kama hicho cha Serikali za Mitaa.
Wagombea wa CCM wanafahamu kuwa maendeleo kwa watanzania kamwe hayataletwa
kwa miujiza kama ambavyo ahadi za wapinzani zinavyosema. Ndiyo maana siko zote
CCM, imeweka bayana kuwa, wananchi wakukubali kuwa kujitegemea kwa kufanya kazi
kwaa bidiii na maarifa ndio msingi wa maendeleo na kutokomeza umasikini. Kila
mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anawajibu wa kufanya kazi na kushirikiana na
serikali kubuni na kutekeleza mbinu bora zaidi za uwezeshaji wananchi. Aidha, mtaji
wa masikini ni ari, nguvu, kasi na akili zake mwenyewe. Uwezeshaji ni njia ya
kumuunga mkono.
Kwa vyama vya upinzani, kuwaahidi wananchi kuwa vitawaletea maendeleo bila
ya kuunganisha nguvu zao katika kufanya kazi ni uongo na unafiki mkubwa
unaopaswa kupigwa vita. Wapinzani walitarajia kukiona Chama cha Mapinduzi
kikiwaletea watanzania maendeleo kwa njia ya “akadabla(mazingaombwe), hili ni
jambo lisilowezekana: Hata wayunani wakale walisema, “Impossibilium nullaest
obligation” yaani hakuna mwenye kupaswa kutenda lisilo wezekana: Tuna imani na
wananchi wa Tanzania kuwa ni watu wenye uwezo wa kuzitambua pumba na kuziweka
mbali na mchele.
Wapinzani hawaelewi watanzania wanataka nini ndio maana mara nyingi
wamekuwa wakitumia kampeni za vitisho na wakati mwingine wafuasi wao
wakihatarisha amani na utulivu uliojengeka miongoni mwa watanzania. Watanzania
hawahitaji vitisho, watanzania, haawahitaji kuona damu ya raia wema ikimwagika.
Watanzania tumezoa Amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa. Hivyo wapinzani
wanaotumia kampeni za vitisho wasitegemee kupata kura za watanzania:
Wakati kampeni za uchaguzi za 2005 zinaanza wapinzani walikuwa wanafanana
na mvuvi anayeng’ang’ania kuwawakilisha wakulima au mwalimu anayetaka kuwa
mwakilishi wa daktari. Kadiri siku zinavyokwenda wapinzani wanachukua sura ya mbabaishaji
anayeng’ang’ania kuwa mweka hazina wa umoja wa raia wema. Watu hawa wakifanikiwa
kutimiza azma yao, maisha na rasilmali za raia hawa wema vitakuwa mashakani.Wapinzani
wajiandae kushindwa kwa kishindo 2005.
Kwa muda mrefu majukumu ya wapinzani yamekuwa ni kudai ruzuku kutoka
serikalini kwa nguvu zote, kuudanganya umma wa watanzania kwa kutoa ahadi
zisizotekelezeka, kuwatishia wananchi wanaonekana kuwa na msimamo na imani na Chama
Cha Mapinduzi na kulalamika bila ya sababu za msingi. Hivi kamwe havitoi mvuto
kwa watanzania wa kuvikuchagua vyama hivi vya upinzani.
Wapinzani bado ni wachanga mno katika ulingo wa siasa. Kuwa wachanga sio
kosa. Kosa kubwa la wapinzani ni kwamba hawataki kukua. Kama vyama vya upinzani
vingekuwa tayari kukua na kukomaa kisiasa basi viongozi na wafuasi wa vyama
hivyo wangekuwa tayari kujifunza kutoka hata kwa mtoto mdogo wa miaka miwili:
Watoto wadogo huwa wanaangalia na kujali hali halisi, huwa hawaendishwi na yale
ambayo hawawezi kupambana nayo. Kama
wapinzani wamejifunza hili, wangekubaliana na hali halisi ya kutokukubalika
kwao mbele ya wananchi waliyo wengi na hivyo wasingepoteza nguvu na muda mwingi
katika kupambanana na mkongwe Chama cha Mapinduzi kwa kuwadanganya watanzania
na kutumia mkakati na mbinu duni kama vitisho ili kutafuta ridhaa za
watanzania.
Ni jambo la kushangaza kwa mtanzania mwenye akili zake timamu kung’ang’ania
kuingia katika kinyang’anyiro ambacho amekuwa akitupwa nje kwa kipindi cha
miaka kumi na mitano bila kuona aibu. Hivi mtu huyu anatarajia malaika washuke
kutoka mbinguni waje kumwambia kuwa hakubaliki kwa watanzania ndio afike
kikomo? Na inakuaje kuwa mtu mwingine ambaye anatembea na ofisi za chama chake
kwenye kikapu, kuomba kura ili aingie ikulu?Hivi watu kama hawa kama hawana
lengo la kuwachekesha watanzania wana malengo gani? Na inakuwaje kwa mtu
anayejiita mpinzani kuacha kupanga mikakati ya kampeni na badala yake kwenda
kwenda mahakamani kudai ruzuku kwa ajili ya chama chake ambacho hakijui hata
rangi za bendera ya taifa letu? Hiii sio aina ya wapinzani tuliyoikusudia
tulipo ridhia kuingia katika mfumo wa vyama vingi.
Kwa kuwa wanatambua wazi kuwa hawakubaliki kwa watazania waliyo wengi hivyo
hawataingia Ikulu wala bungeni, lakini bado wanang’ang’ania kuzunguka huku na
kule kujinadi. Tunashawishika kuamini kuwa wengi wao hawapo kwa ajili ya maslahi
ya watanzania. Pengine hiki ndicho kinachowafanya wengi wao watumie nguvu
nyingi sana katika kudai ruzuku kuliko kupanga mikakati ya kuwaletea watanzania
maendeleo. Hii imewafanya wapinzani wengi kukosa mwelekeo sahihi hata kama
inapotokea baadhi yao kuingia bungeni, huwa si jambo la ajabu kwao kusahau
kilichowapeleka bungeni na badala yake kufanya mambo ya kihuni ambayo hupelekea
baadhi yao kutimuliwa bungeni. Tunaimani na wananchi wa Tanzania hawataharibu
kura zao kwa kuwapa watu hawa badala yake watakichagua Chama cha Mapinduzi kwa
kura nyinngi iwezekanavyo hivyo kupelekea kupatikana kwa Ushindi wa Kishindo,
kwa maisha bora ya kila Mtanzania.
Nguvu ya Hoja
Abiyani Chuo Kikuu.