CHAGUA CCM, CHAGUA KIKWETE CHAGUA
MAENDELEO YA WANAWAKE TANZANIA
Wanawake ni watu wenye mchango mkubwa sana kwa
maendeleo ya jamii ya Watanzania. Wanawake ni wazazi na walezi msingi wa vizazi
vyote. Katika Tanzania, wanawake watakumbukwa kwa ushiriki wao katika harakati
za kutafuta uhuru. Aidha, wamekuwa mstari wa mbele katika harakati za kuinua
uchumi na mageuzi ya kisiasa. Sauti za wanawake ziko juu sana katika kuleta
mabadiliko ya kijamii, hususan kupambana na mila na desturi potofu mathalani
ukeketaji; ambazo zimekuwa zikileta athari kubwa kwa ustawi wa wanawake wenyewe
na jamii kwa ujumla.wa kutambuliwa na kuthaminiwa na usiopimika kwa maendeleo
ya taifa.
Ni wanawake wa Tanzania ambao wamekuwa wapiga kura waaminifu, na hivyo
kuipa CCM ushindi wa kishindo katika chaguzi zote zilizopita tangu nchi yetu
ipate uhuru. Ni katika kuwatambua, kuwaheshimu, kuwathamini wanawake hawa, CCM
katika Ilani yake ya Uchaguzi imetoa kipaumbele kwa masuala yatakayowaletea
wanawake na jamii maendeleo endelevu. CCM inatambua kwamba, wanawake
wakiwezeshwa kisiasa, kiuchumi, kielimu na kijamii, taifa zima litakuwa
limeinuliwa, hatimaye, kuwa na maisha bora kwa kila Mtanzania.
Hata hivyo, ni muhimu kwa wanawake wote kuzingatia kwamba, waipe CCM kura
zote za ndio, ili wanawake waweze kunufaika na Sera nzuri za CCM na zinazojali
maslahi ya watu wote pasipo ubaguzi katika msingi wowote kama jinsia, dini,
rangi, elimu, na mikoa. Wanawake watambue kuwa hawatapoteza kura zao kwa kuamua
kuchagua CCM. Kura zao zitakuwa ni mtaji ambao watakuwa wamewekeza katika kisima
cha maendeleo kinachopata uhimili wa Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya kuelekea
katika Tanzania yenye neema tele.
Tunasema hivi, kwani CCM ni Chama ambacho kimefanya mengi sana kwa
maendeleo ya wanawake ambayo wanawake na jamii wanajivunia. Mifano iko mingi
sana. Kisiasa, CCM imezingatia na kuinua ushiriki wa wanawake katika vyombo vya
maamuzi. Idadi ya wanawake Bungeni imeongezeka kutoka wanawake 8 sawasawa na
asilimia 10, katika kipindi cha 1961 hadi 1965, na idadi ya wanawake kufikia
zaidi ya asilimia 20 Julai 2005. Ongezeko kama hili limekuwa pia katika
ushiriki wa wanawake kwenye vyombo vya maamuzi mashina, matawi, kata, tarafa,
wilaya, mikoa hadi taifa. Idadi ya wanawake imeongezeka pia katika nyanja
mbalimbali za utumishi na ajira serikalini na sekta binafsi. Wanawake wengi
sana wamepata mwamko mkubwa wa kujihusisha kwenye ajira binafsi isiyo rasmi.
Kielimu wanawake wamepewa kipaumbele. Kumekuwa na ufadhili maalum kwa mfano
Carnegie mahususi kuinua kiwango cha sifa za msingi za kujiunga na Chuo Kikuu
Dar es Salaam. Ipo mifuko mingine mingi, inayotoa ufadhili kwa wanawake ili
kuwawezesha kupata elimu katika vyuo mbalimbali vya elimu ya Juu hapa nchini,
na hata nje ya nchi.
Wanawake na wananchi wote kwa ujumla wanakubaliana na ukweli usiofichika
kwamba, mweleko unaonesha wazi kuwa Ndugu yetu Jakaya Kikwete atashinda kwa
kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa 2005. Kwa maneno mengine, wanawake
wanachohitaji kufikiria, ni kwa namna gani watashirikiana na Kikwete ili
kufanikisha azma ya CCM na ahadi nzuri za ndugu Kikwete za kuwatumikia wanawake
wa Tanzania ili wawe na maisha bora. Wanawake andaeni mbinu na mkakati wa
kutekeleza kwa vitendo mema yote ambayo CCM imekusudia kuwafanyia, kwa Ari
Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya.
Wanawake watambue kuwa ndugu Kikwete hajifunzi kuongoza. Anao uzoefu wa
muda mrefu alioupata kwa muda mrefu akiwa Waziri katika wizara mbalimbali.
Kimuundo na kiutendaji, Waziri ni mwakilishi wa Rais katika wizara husika. Zaidi,
ndugu Kikwete anao uzoefu wa ujenzi wa Amani na Utulivu. Ameshiriki kwa ari na
uwezo mkubwa katika harakati za kuleta amani kwa njia ya mazungumzo, katika
nchi za Maziwa Makuu. Wanawake wanatambua kwamba uvunjifu wowote wa Amani na
Utulivu, huathiri wanawake na watoto zaidi. Tunaye Kikwete, Nyota ya Amani,
wanawake mpeni kura zote za ndio.
Kwa upande wa elimu CCM, itahakikisha kuwa inatoa elimu ya awali na msingi
kwa wasichana wote na na watu wa jinsia zote, shule za sekondari kwa kila kata,
itaimarisha ubora wa vifaa,majengo na walimu, itaimarisha elimu ya kujiendeleza
kwa wanawake na elimu ya watu wazima, itaimarisha elimu ya UKIMWI na magojwa
mengine na kuhamasisha wanafunzi wa kike kuchukua masomo ya sayansi ili
kuhakikisha kuwa wanawake wanashika madaraka katika nyanja za juu na kushiriki
katika maamuzi ya kitaifa.
Katika sekta ya afya CCM kupitia ilani yake ya 2005/2010 itahakikisha kuwa
kuna huduma bora ya afya ya msingi kwa wanawake na watoto wote, kupunguza vifo
vya watoto wachanga na watoto chini ya umri wa miaka mitano,kuinua kiwango cha
muda wa kuishi kwa wanawake, kuboresha huduma za kiliniki kwa kina mama na
watoto kuwa bora na karibu na wananchi, kutoa huduma bure kwa wanawake
wasiojiweza na kuimarisha vita dhidi ya UKIMWI.
Pia kwenye sekta ya kilimo katika Ilani yake CCM itahakikisha kuwa kilimo cha
kisasa ndio msingi wa uchumi wa kisasa, itatoa elimu kwa wanawake juu ya
matumizi bora ya ardhi, kushawishi na kueneza kwa wanawake elimu ya
utengenezaji na upatikanaji wa mikokoteni ya kuvutwa na wanyama na vinu vya
kisasa vya kukobolea na kusagia nafaka. Aidha CCM itahakikisha upatikanaji wa
mbegu bora mbolea na pembejeo kwa wanawake, kutoa elimu kwa wanawake kuhusu
uvunaji wa maji ya mvua,kuchimba mabwawa na kuimarisha kilimo cha umwagiliaji.
CCM itazingatia kuundwa na kuendeleza mifuko ya mikopo kwa ajili ya wanawake
wakulima wadogo wadogo vijijini, na utoaji wa elimu kwa wanawake ya usindikiji
na ufungashaji wa mazao ili kuvutia soko na kupunguza uharibikaji wa mazao.
CCM itaratibu kuboresha upatikanaji wa masoko ya uhakika kwa mazao, kutoa
elimu kwa wanawake juu ya njia rahisi ya kuhifadhi mazao, kushawishi wanawake, kuanzisha
na kukuza kilimo cha maua,matunda,mboga na mazao ya viungo vya chakula. CCM
itahakikisha upatikanaji wa elimu kwa wanawake juu ya matumizi bora ya mazao ya
kilimo ili kuinua lishe na kujenga afya ya familia na jamii. CCM pia itaendeleza
kilimo na kukifanya kiwe cha kisasa ili kuweza kutoa ajira kwa wanawake na
vijana na kutoa vivutio, zawadi na tuzo kwa wakulima wanawake watakaoongeza
maradufu kiasi cha mazao yanaovunwa kwa eka.
Katika nyanja ya ufugaji na uvuvi,CCM itafanya yafuatayo; kuboresha
mazingira ya ufugaji na uvuvi ili kuinua kiwango cha ushiriki wa wanawake na
vijana, kutoa elimu kwa wanawake itakayosaidia kuinua kiwango cha mazao
yatokanao na ufugaji na uvuvi, kutoa elimu kwa wanawake juu ya usindikaji na
ufungishaji wa mazao yatokano na uvuvi na ufugaji ili kuvutia soko na kuzuia
kuharibika kwa mazao hayo. Aidha CCM itaendeleza ufugaji na uvuvu na kuufanya
uwe wa kisasa ili kuweza kutoa ajira kwa wanawake na vijana, pia kuhamasisha
wanawake wafugaji na wavuvi kuanzisha na kujiunga na SACCOS na kutumia
kuwapatia mikopo.
Maji pia ni kati ya mambo yaliyopewa kipaumbele kwenye ilani ya CCM
2005/2010. Chamacha Mapinduzi kitahakikisha kuwa kinawawezesha wanawake wa
mijini na vijijini kupata maji safi, salama yakutosha na yaliyokaribu na sehemu
wanzoishi. CCM itaendeleza ujenzi wa malambo na mabwawa, pia kuunda na
kuendeleza ushiriki wa wanawake katika kamati ya maji na mifuko ya maji ya
wananchi. CCM itaratibu utoaji elimu kwa wanawake juu ya njia nyepesi na rahisi
ya kukinga na kuhifadhi maji ya mvua, na
elimu kwa wanawake juu ya kuvitambua, kuvithamini na kuvutunza vyanzo vya maji.
Katika miradi midogomidogo CCM itatoa elimu na kuinua kiwango cha ushiriki
kwa wanawake na vijana katika kuanzisha na kuendeleza miradi midogo midogo. CCM
itatoa elimu kwa wanawake juu ya ubora wa bdhaa ili kuvutia masoko ya ndani na
ya nje ya nchi, na elimu kwa wanawake juu ya utunzaji wa mahesabu na kujenga
ubunifu utakaosaidia kuendeleza miradi, kuanzisha vikundi vidogo vidogo vya
ushirika vya wanawake, upatikanaji kwa wanwanke wa mikopo yenye masharti nafuu.
CCM itatoa elimu kwa wanawake juu ya afya na kinga juu ya UKIMWI.
Aidha kwenye sekta ya Nishati CCM katika ilani yake ya 2005/2010 itawarahisishia
wanawake upatikanaji wa nishaiti na uhifadhi wa mazingia. CCM itatoa kwa
wanawake elimu juu ya matumizi ya njia rahisi na za kisasa za nishati
inayopatikana katika mazingira yao, pia kutoa elimu kwa wanawake juu ya kupunguza
matumizi ya kuni na mkaa. CCM itatoa elimu kwa wanawake juu ya upandaji miti
inayokuwa kwa haraka. CCM itasimamia kuharakisha upatikanaji na usambazaji wa
umeme karibu na wananchi. Muhimu pia, CCM
itachochea na kuendeleza vipaji na ubunifu wa wanawake na vijana kuhusu
majiko yanayotumia nishati kidogo,na kuimarisha na kuendeleza usambazaji wa
huduma ya umeme kwa bei nafuu.
Tukiangalia takwimu ya idadi ya watu, Tanzania ni nchi yenye watu wapatao
milioni thelethini na nne, ambapo wanaume ni asilimia 49 na wanawake ni
asilimia 51. Kutokana na idadi hiyo wanawake wana idadi kubwa kuliko wanaume.
Wanawake wote Tanzania ni wajibu wao kujitokeza kupigia kura CCM ili iweze
kushinda kwa kishindo. Tuchague chama CCM ambacho kina “sera zilizotulia”,.
Maana yake zinazoeleweka, zinazokubalika, zinazotekelezeka, zinazojengwa juu ya
misingi ya historia ya Uhuru, na Utaifa wetu na maslahi ya Tanzania inayokwenda
na wakati. Aidha, Sera za CCM zimelenga kuinua viwango vya maisha ya kila
Mtanzania pasipo ubaguzi wa aina yoyote. bila kupingwa na zinafaa Tanzania
Tunatoa pongezi nyingi kwa Chama Cha Mapinduzi kwa kumkabidhi ndugu Kikwete
dhamana ya kupeperusha bendera ya CCM na hatimaye afikie kubeba dhama kubwa
zaidi ya kubeba bendera ya taifa. Wanawake wote wa Tanzania wanayo imani kuwa
sana kwa CCM na ndugu Kikwete. Wanawake wote wanajiandaa tena kwa uaminifu
kumpigia kura zao zote za ndiyo ndugu Jakaya Kikwete hapo ifikapo tarehe
30/10/2005. Wanawake wanaijua vema CCM. Hakutakuwa na kubabaika na kufanya
majaribio ya sera kama vyama vingine ambavyo havijawahi kushika uongozi wa
nchi. CCM Awamu ya Nne itakuwa inaendeleza juu ya yale mema mengi ambayo
yameasisiwa na Awamu zilizopita. Ukweli huu unawapa wanawake matumaini makubwa
sana ya kusonga mbele kimaendeleo kwa Ari Mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya, katika
Tanzania itakayoongozwa na ndugu Kikwete. Ndiyo maana tunasema CHAGUA CCM,
CHAGUA KIKWETE KWA MAENDELEO YA WANAWAKE TANZANIA.
Nguvu ya Hoja,
Abiyani Chuo Kikuu.