CCM IMEONESHA UMAHIRI NA UWEZO MKUBWA WA KUPAMBANA NA UMASIKINI

Kabla ya kuchagua chama gani ukipe madaraka ya kuongoza nchi kwanza fikiria uwezo wa chama hicho kitaasisi.Chama cha mapinduzi (CCM) ni miongoni vyama vichache duniani ambavyo vimejitengenezea muundo bora wa kitaasisi kwa ajili ya kuongoza nchi. Vyama vya aina hii huwa na viongozi wenye uwezo mkubwa wa kuongoza nchi bila kutetereka na kujenga imani kwa wananchi kwa kuwa na uhakika wa kuishi na kujiendeleza kwa usalama na bila woga wowote.Kwa hali hiyo CCM ni chama ambacho watu wengi wamekuwa wakija  Kutoka  nchi mbalimbali kupenda kujifunza kutoka Tanzania ni jinsi gani kimeweza kuongoza nchi kwa ustadi shrikishi na kwa mafanikio makubwa.

Tangia uhuru CCM ilitamka rasmi kazi kubwa iliyopo mbele ya Taifa letu ni kupambana maadui wakuu watatu wakiwemo Umasikini, Ujinga na Maradhi.Maadui hawa ni maeneo nyeti ambayo CCM iliyaona kuwa tukifanikiwa hapa maisha ya mwananchi yatakuwa bora zaidi. Serikali imetoa kipaumbele katika vita dhidi ya umaskini. Katika kufanya hivyo, inatekeleza malengo ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025, na vilevile mpango wa kimataifa wenye dhamira ya kutokomeza umaskini kwa nusu ya kiwango cha sasa ifikapo mwaka 2015 na kuutokomeza kabisa ifikapo mwaka 2025. Serikali kwa kushirikiana na wadau wengine, iliandaa Mkakati wa Taifa wa Kusimamia Utekelezaji wa Sera za Kuondoa Umaskini

Kwa mujibu wa ujibu wa ilani na nyaraka mbali mbali za CCM, Masuala makuu yaliyobainishwa katika kupiga vita umaskini na Serikali ni pamoja naKukuza uchumi unaoshirikisha watu wengi kuzingatia shughuli zinazofanywa na wadau mbalimbali kama vile wakulima wadogo wafanyabiashara wadogo, viwanda vidogo na vya kati, Kuendeleza huduma muhimu za kijamii na kiuchumi, Kuweka mazingira mazuri ya umilikaji wa uchumi yanayovutia wawekezaji; Kuwa na usimamizi mzuri wa hifadhi ya mazingira kwa maendeleo endelevu; Kuimarisha miundombinu hasa barabara na mawasiliano; Utawala bora  kuwa hasa vita dhidi ya rushwa, uzingatiaji wa utawala wa sheria, demokrasia, uwazi, uwajibikaji na ushirikishwajiwa wadau na
Kuwa na mfumo imara wa ufuatiliaji.

Kwa watanzania ambao walikuwa bado hawajui hadi leo, ni kwmaba Serikali ya CCM imeonyesha kasi kubwa kuibadili Tanzania  na imewezesha nchi kusamehewa baadhi ya madeni yake chini ya Mpango wa Msamaha wa Madeni na Mkakati wa Kupunguza Umaskini. Pia Serikali imeandaa Mkakati wa Misaada wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaolenga kuboresha usimamizi wa misaada ya wafadhili, ili kuielekeza misaada hiyo katika maeneo ya kipaumbele yaliyoainishwa katika kupunguza umaskini. Katika kuhakikisha kuwa jamii maskini zinapata huduma za msingi kwa gharama zinazolingana na uwezo wao kiuchumi, hatua mbalimbali zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kufuta ada zote katika shule za msingi na kupunguza ada katika shule za sekondari za Serikali, kutoa ruzuku kwa shule za sekondari za binafsi, kutoa ruzuku ya mbolea na kuondoa kodi katika pembejeo na zana muhimu za kilimo na mifugo na kuondoa kodi ya makisio kabla ya kuanza biashara. Hatua hizo zimesaidia kupunguza kero zinazowakabili wananchi.

Ili kuongesa kasi kuushinda Umasikini, Serikali ya CCM  ilianzisha Idara ya kuondoa Umaskini ili kuimarisha shughuli za uratibu na utekelezaji wa mipango ya kuondoa umaskini. Idara hiyo ina kazi kuu ya kuratibu na kusimamia jitihada za kupunguza umaskini nchini. Vita dhidi ya umaskini inachukuliwa kama agenda kuu ya Taifa na hivyo kuchukua hatua za kuongeza bajeti ya fedha zinazotengwa katika sekta za kipaumbele. Kwa mujibu wa Uchambuzi wa utafiti uliofanyika mwaka 2000/001, umeonyesha kuwa idadi ya watu wanaoishi katika umaskini imepungua kutoka asilimia 38.6 mwaka 1991/92 kufikia asilimia 35.3 mwaka 2000/2001. Uchambuzi huo unabainisha kuwa idadi ya watu wanaoishi katika umaskini uliokithiri, imepungua kutoka asilimia 21.6 mwaka 1991/92 kufikia asilimia 17.7 mwaka 2000/01.

Ili kuleta unafuu wa maisha Serikali ya CCM pia imeweza kusimamia mfumko wa bei na kupata  mafanikio makubwa ya kupungua kwa kiwango cha mfumko wa bei kutoka asilimia 27.1 mwaka 1995 hadi asilimia 4.1 mwezi Novemba, 2004. Mafanikio hayo yametokana na utekelezaji makini wa sera za kudhibiti ongezeko la ujazi wa fedha na karadha; kuongezeka kwa makusanyo ya mapato ya Serikali; mkakati na mfumo wa kudhibiti matumizi ya Serikali; juhudi za wananchi katika kuongeza uzalishaji kwenye baadhi ya mazao ya chakula; na upatikanaji na usambazaji mzuri wa bidhaa muhimu za matumizi ya kawaida. Lengo la Serikali ni kuendeleza sera hizo ili kiwango cha mfumko wa bei kiendelee kushuka na kilingane na cha nchi tunazofanya nazo biashara kwa wingi. Mwenendo wa kupungua kwa Mfumko wa Bei umeonyeshwa katika

Ili kuongeza kasi ya kukuza uchumi na kuonge ajira Serikali ya CCM imefanya juhudi kubwa ya kuvutia wawekezaji wa ndani na nje kwa kuweka mazingira mazuri ya kibiashara. Kwa mujibu wa ripoti mbali mbali kuanzia mwaka 1995 hadi Desemba 2004, Kituo cha Uwekezaji (TIC) kimeidhinisha jumla ya miradi 2,321 inayokadiriwa kutoa nafasi za ajira 447,290. Kati ya miradi hiyo, 1,598 ilikuwa mipya na miradi 723 ni ya zamani. Miradi 1,003 sawa na asilimia 43.2 inamilikiwa na wawekezaji wa ndani, miradi 610 sawa na asilimia 26.3 na wawekezaji wa nje na miradi 708 sawa na asilimia 30.5 ni ya ubia kati ya wawekezaji wa ndani na wa nje. Thamani ya uwekezaji katika miradi yote hiyo ni Shilingi 7,587,078 milioni.

Kwa kuongeza nguvu na kasi na ushiriki wa kila mwananchi  Serikali ya CCM ilianzisha Mkakati wa Kupunguza Umaskini Awamu ya Pili ujulikanao kama Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania (MKUKUTA) wa mwaka 2004. Mkakati utatekelezwa na Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa miaka mitano kuanzia mwaka 2005/06 hadi 2009/10.

Pia Serikali kwa kutambua tatizo la ajira nchini, ilianzisha mradi wa kutoa mikopo midogo uliotokana na mkopo wa Dola za Marekani 10.7 milioni kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika. Utekelezaji wa mradi huo ulianza kwa majaribio katika mikoa sita iliyobainika kuwa nyuma kimaendeleo. Mikoa hiyo ni Mtwara, Lindi, Pwani, Morogoro, Dodoma na Singida. Kati ya mwaka 2000 na 2004, Mradi umeweza kutoa mikopo ya Shilingi bilioni 3.7 ambayo ni asilimia 42 ya fedha za mkopo zinazokusudiwa kutolewa kwa wananchi. Fedha zilizotolewa chini ya mradi huo, zimewafikia walengwa 17,404 ambao ni asilimia 53 ya walengwa waliokusudiwa. Asilimia 61 ya walengwa waliofikiwa ni wanawake. Mikopo hiyo imewafikia wananchi kupitia asasi 73 za kifedha ambazo asilimia 68 ni Vyama vya Ushirika vya Akiba na Mikopo.

Serikali ilianzisha Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) kwa lengo la kuboresha huduma za jamii ikiwa ni hatua mojawapo ya kupambana na umaskini kwa kusaidia shughuli za wananchi katika sekta za afya, elimu, maji, miundombinu, mazingira na mafunzo.vile vile Katika kutekeleza mwelekeo wa sera za CCM na Ilani za Uchaguzi, Serikali imechukua hatua kadhaa ili kuhakikisha kwamba wananchi wa Tanzania wanakuwa na uwezo zaidi wa kushiriki katika uchumi wa nchi yao. Katika kuboresha zaidi mazingira ya uwezeshaji wa wananchi hususan kwa kutumia rasilimali zilizopo, Serikali imefanya maandalizi ya Programu Maalum ya Kurasimisha Rasilimali za Sekta isiyo Rasmi kuwa sekta rasmi (MKURABITA) kwa nia ya kuwawezesha wananchi kutumia mali walizonazo kama dhamana ya kukopa fedha kutoka benki kwa ajili ya kukuza shughuli zao za kiuchumi na hivyo kupunguza umaskini.

Inawezekana bado kuna watu hawaamini mafanikio haya.Kwa mujibu wa waraka uliotolewa na shirika la masuala ya Uchumi duniani 
 ”World Economic Forum (WEF)’’ Tanzania imepanda kwa kasi na kuruka nafasi  11  ikilinganishwa na mchakato wa mwaka jana ambapo kwanza ilikuwa chini ya Kenya na Uganda. kwa mujibu wa waraka huo Tanzania ilikuwa nchi ya  71  kati ya nchi  117  zilizofanyiwa tathnini hiyo.nchi ya Uganda ilikuwa ya 87 na Kenya ilikuwa ya  92.Awali Tanzania ilikuwa ya 82 wakati Kenya ilikuwa ya 78 naUganda 79.  
katika mchakato huo vitu vitatu viliangaliwa pia  uimara wa uchumi, ubora wa taasisi za umma na utayari wa kiteknologia..Tanzania ilioneshwa kuwa na uimara mkubwa wa taasisi za umma  na kuwa na nafasi ya 60, wakati uimara wa Uchumi ilikuwa ya 72 na utayari wa kiteknologia..ilikuwa nchi ya 86

Kwa maana hiyo una sababu za kuichagua CCM katika kiti cha Urais, Ubunge na Udiwani.Kidumu chama  cha Mapinduzi.

 

Nguvu ya Hoja,

Abiyani Chuo Kikuu.