ADHMA YA KIKWETE KUIMARISHA MIUNDO MBINU INAGUSA MATARAJIO YA MAENDELEO NA UKOMBOZI WA DHATI WA MTANZANIA

 

Tunapenda kukipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa jitihada zake za muda mrefu katika harakati za kulikomboa taifa kutoka kwenye makucha wa maadui watatu wa maendeleo na ustawi wa jamii ya watanzania; umasikini, ujinga na maradhi. Katika awmu mbalimbali za utawala wake, serikali ya Chama Cha Mapinduzi; kwa nguvu zote imekuwa mstari wa mbele kutokomeza kabisa kustawi kwa maadui hao kwa kupanga na kutekeleza mipango mbalimbali ambayo ilihakikisha faraja na ustawi mkubwa wa ke unapatikana.

 

Sera ya ujamaa na kujitegemea ni mfano mdogo tu ambao umeipa Tanzania heshima kubwa ndania na nje ya nchi na kuwa mfano bora kwa mataifa ya Afrika na ulimwengu wa nchi za kusini kwani umewajengea Watanzania utamaduni wa kuishi pamoja kwa amani, upendo na mshikamano, jambo ambalo kwetu sisi Watanzania ni heshima na faraja kubwa. Kwa watanzania wapenda maendeleona wenye mapenzi mema kw nchi yao tutakuwa wachoyo wa fadhila kama hatuataliona hili kuwa jambo jema kwetu na nchi na bila shaka tuatungana na wenzetu “Chama Cha Mapinduzi” katika kuwaenzi waasisi wa chama hicho, kukipongeza chama na viongozi wake wa wa awamu zote jwa kuheshimu ustawi wa watu wake na kuifanya Tanzania sehemu salama ya kuishi nakimbilio la wageni. Hongera Chama Cha Mapinduzi kwa kutufikisha hapa tulipo.

 

Tunaungana na wenzetu ambao kwa wakati tofauti hasa katila lipindi hiki cha uchaguzi wamekuwa wakiandika na wanaendelea kuandika makala mbalimbali yanayohusu mafanikio ya Chama Cha Mapinduzi na sera zake katika awamu mbalimbali. Sisi tunapenda kutumia fursa hii kuelekeza maoni na hisia zetu katika hotubanaahadi za matumaini makubwa aliyonayo mgonbea wa Chama Cha Mapinduzi, kwa tiketi ya uraisi, chama na serikali yake kwa watanzania.

 

Katika hotuba zake za kampeni ya kuelekea ikulu mgombea huyo meongelea mambo mengi na yamsing kwa maendeleo ya Mtanzania. Tunapenda leo kutoa mchango hasa katika mpango kabambe wa chama chake wa kuwakomboa watanzania katika kuimarisha miundo mbinu mbalimbali, ukiwemo ujenzi wa barabara kuu zinazoubganisha mikoa kwa kiwango cha lami, mpango ambao ni sehemu ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi na serikali ya Chama Cha Mapinduzi umeshaanza kutekeleza na watanzania wote tu mashahidi katika hili.

 

Mpamgo huu wa kuimarisha miundo mbinu hususan ujenzi wa barabara kuu zinazounganisha mikoa unagusa na kuvutia watanzania wengi. Tunaipongeza serikali yua awamu ya tatu ya CCM maana kwa kufanya hivyo, imetambua umuhimu wa miundo mbinu hasa usafiri wa barabara katika maendeleo ya nchi, jambo ambalo katika enzi hii ya utandawazi ambapo dunia sasa ni kama kijiji linatakiwa kupewa kipaumbele katika mipango ya maendeleo ya nchi kwani barabara kama nyenzo muimu ya usafiri wa umma ni daraja muhimu la kuivusha nchi katika maendeleo ya ulimwengu wa utandawazi na umasikini.

 

Adhma hiyo ya Chama Cha Mapinduzi kuleta ukombozi na maendeleo thabiti ya mtanzania kwa kuinganisha miundo mbinu katika pembe zote za nchi inaongeza matumaini na imani ya wananchi kwa Chama Cha mapinduzi na kukijengea uhakika wa kuliongoza taifa katika kipindi kingine cha miaka kumi ijayo ya utawala wa Jakaya Kikwete; kipenzi cha watanzania amabao wengi wao ni wakulima na wafanyakazi

 

Serikali ya Chama Cha mapinduzi katika mipango yake ya awamu ijayo pia imepanga kuzalisha umeme wa kutosha kukidhi uzalishaji viwandani na kwa matumizi ya nyumbani. Baadhi tu ya miradi ambayo itashughulikiwiwa kufikia lengo hilo ni kuzalisha umeme kutokana na makaa ya mawe Mchuchuma, umeme wa gesi ya Mnazi bay kwa ajili ya mikoa ya Lindi na Mtwara, kufikisha umeme katika makao makuu ya wilaya zikiwemo Kibondo, Kasulu, Mbinga, Tunduru, Likombe, Simanjiro na kikadi na kuunganisha mikoa ya Kigoma na Ruvuma na Gridi ya taifa.

 

Katika kipindi cha 205 – 2010, Chama Cha Mapinduzi pia kimepanga mipango ya kukarabati barabara zote kazi ambayo inaendelea na ujenzi wa kiwango cha lami amabo umeshaanza ikiwemo barabara ya Manyoni – Singida na Shelui Kigoma – Biharamulo – Lusamoja na kuwanza ujenzi wa kiwango cha lami barabara za Minjinga – Babati – Singida, Arusha – Namanga na kuzifanyia upanuzi barabara za Mtwara – Masasi – Songea  - Mbamba bay, Maganzo – Maswa – Bariadi – Mpulawandi; Babati – Dodoma – Iringa. Hili si jambo dogo kwetu sisi na kwa maendeleo ya nchi hivyo tunaipongeza sana CCM kwa kuonesha upeo mkubwa wa maendeleo ya watanzania katika kipindi chake cha utawala wa awamu inayofuata na vipindi vingine vya utawala wake.

 

Mpango wao kabambe wa uimarishaji miundo mbinu unatoa Changamoto kubwa ya maendeleo kwa wananchi unaoonesha ni  kwa jinsi gani serikali ya awamu ya nne ya Chama Cha Mapinduzi imepania kuona kuwa wananchi wake wanajengewa mazingira mazuri ya maendeleo kwani kwani kuimarika kwa mawasiliano katiak sekta hiyo muhimu ikiwemo usafir wa barabarautaimarish mawasiliano  mazuri ya biashara kati ya mikoa ya Tanzania na nchi jirani  pia kutafungua milango ya uwekezaji kwa makampuni na watu binafsi kuwekeza katiaka sekta  nyingine zikiwemo utalii, kilimo, misitu na viwanda.

 

Kwa upande wa mikoa ya kusini mwa nchi, mpago wa ujenzi wa barabara na uimarishaji wa miundo mbinu mingine si tu utajenga mazingira mazuri ya uchumi kwa mikoa husika itakavyokuwa katika sehemu nyingine ya nchi bali pia utaleta maendeleo amabayo yanaondoa dhana ya siku nyingi  ambayo imejengengeka miongoni mwa watanzania kwamba kusini siyo sehemu ya kuishi. Kwa mantiki hiyo basiTanzania na Kusini ya awamu ya nne ya utawala wa CCM …wa Tanzania ni neema, kuleta mapinduzi ya uchumi mfano mzuri ni mapinduzi ya viwanda katika nchi za ulaya na za bara la Amerika. Na kwa sasa ambapo serikali zetu zinajaribu kuimarish jumuiya ya Afrika ya Mashariki suala la miundo mbinu litachangia kujenga mazingira mazuri kwa nchi za Kenya na Uganda kuimarisha mazingira mazuri ya kiuchumi na Tanzania hivyo wananchi wote watafaidika na masualal ya jumuiya hiyo.

 

Wahenga walisema siku njema huonekana mapema na Chanda chema huvishwa pete. Watanzania tazama CCM, tazama  wagombea wake wapinzani wasiwadanganye mkaacha kuchagua CCM. Tukichagua CCM tutachagua maendeleo endelevu. Dhamira na ishara ya Chama Cha Mapinduzi kuleta maemdeleo inaonekana mapema kwa kuangalia ilani yake ya uchaguzi, kauli za …. Za wagombea waketunatoa mwito kwa watanzania kuangalia mustakabali wao maendeleo na kuwakumbusha kuwa kitu kilichi chema hutuzwa. Tuituze CCM, Tuwatuze wagombea wake kwa kuwapa kura za ndiyo na kwa chama ushindi wa kishindo siku ya uchaguzi ambayo ni tarehe 30 Oktoba na ustawi

 

Hayo tu ni baadhi ya manufaa ambayo watanzania tunapaswa kuyaona ndani ya busara na ukweli wa kuchagua CCM kama chama chao kwa maendeleo  ukiondoa faida ya ajira kwa watanzania kutokanan na kuimarishwa kwa biashara, uwekezaji katika sekta mbalimbali na kuwepo shughuli za utalii kwa sehemu yenye vifutio hivyo.

 

Tunawashauri watanzania watafakari hilo na kufanya maamuzi sahihi siku ya uchaguzi hapo Octoba tarehe 30, 2005 kwani kosa dogo katika zoezi la kupiga kura kuwa lina athari kubwa kwa maendeleo ya jamii hasa pale mwananchi anapodanganyika na kuamua kuchagua chama chenye programu amabayo haitekelezeki. Tumeona ni kwa jinsi gani programu za chama tawala zinavyolenga maendeleo ya watu, miundo mbinu hususan ujenzi wa barabara ikiwa tu sehemu ya mengi mema ambayo CCM imedhamiria kwa ukombozi wa watu wake.

Watanzania tukumbuke kwamba suala la miundo mbinu si dogo kwa maendeleo ya nchi kwani histosia inatuonyesha kuwa ujenzi wa miundo mbinu umechangia sana. Hongera CCM, kura zote kwa CCM kwa maendeleo na ustawi wa watanzania.

 

 

 

Kevin Ngonyani na Rehema Longo

Nguvu ya Hoja,

Abiyani Chuo Kikuu cha Dar es Salaam