MAPAMBANO DHIDI YA UMASIKINI NI NDOTO KAMA TUTACHAGUA OVYO

Katika wiki hizi chache  zilizobakia kufikia tarehe ya kupiga kura ya Rais wabunge na madiwani, wapo wananchi ambao hadi sasa bado hawajafanya uamuzi juu ya nani watakayempigia kura ifikapo tarehe therathini mwezi huu kwa madai kwamba mambo yatajiipa huko huko kituoni. Katika kipindi chote kilichopita cha wagombe kujinadi ,juu ya kipi kitakachofanyika baada ya vyama hivyo kushinda na kuingia madarakani , kila mtu anmatumaini mabubwa kwa wapiga kura wake kwamba wamemwelewa vilivyo na mategemeo makubwa kwa kila anayeingia katika uwanja wa mashindano ni kupata ushindi ,uwe wa kishindo, wa tsunami ,ushindi ni ushindi tu.Ushindi unaotarajiwa kwa kila chama ni kuona wagombea wake wanakubalika katika kila daraja , nikiwa na maana ya ushindi wa kiti cha urais, kiti cha ubunge, na kiti cha udiwani.

 

Wapo baadhi ya wapiga kura ambao tayari wameshafanya uamuzi wa Rais wao mtarajiwa , lakini bado wana kigugumizi cha Mbunge yupi atakayewafaa, na kwa upande wa Diwani ndio kabisaa hawajui wamchague yupi.Kigugumizi hiki kinatoka wapi basi? Ninaamini kuwa kila chama kumefanya maamuzi makini na  sahihi katika kuchagua wagombea wa viti vyote  vinavyotakiwa kupigiwa kura na watanzania siku ya siku itakapowadia.

 

Vipo vyama ambavyo sera zake zinaonekana kuwa makini sana , na  baadhi ya sera hizo zimekwishaonyesha matokeo mazuri kwa watanzania na kilichobakia ni kuendelezwa na kuboreshwa zaidi kinachotakiwa ni kuhakikisha kuwa kura yako inalenga kwa wagombea watakaokuwa wamepitishwa wa chama kimoja  ili kuonyesha ukomavu wa fikra, na utumiaji wa uhuru wako wa kuchagua chama kinachofaa kuiongoza nchi yetu kwa kipindi 2005-2010 Tunapochagua Rais tuchague  na wasaidizi wake watakaomwezesha kufanya maamuzi sahihi katika kutekeleza  ilani ya chama kilichomweka madarakani.  Kwa kuwa kila chama kin ayo ilani yake ya uchaguzi na mwelekeo wake baada ya kuingia madarakani Na kwa upande wa CCM sina shaka kwamba kwa mtindo huu wa viongozi hao watatu  nchi yetu imefanya mambo mengi ya kuiweka nchi hii katika sura ya kuvutia  kama haya yafuatayo:

 

Tanzania chini ya  chama cha mapinduzi imekuwa mbali kiushindani kiuchumi mbali zaidi  ya Kenya and Uganda  katika mwaka 2005 mchakato wa ushindani huo.Kwa mujibu wa waraka uliotolewa na shirika la masuala ya Uchumi duniani 
 “”World Economic Forum (WEF)’’ Tanzania imepanda kwa kasi na kuruka nafasi  11  ikilinganishwa na mchakato wa mwaka jana ambapo kwanza ilikuwa chini ya Kenya na Uganda.kwa mujibu wa waraka huo Tanzania ilikuwa nchi ya  71  kati ya nchi  117  zilizofanyiwa tathnini hiyo.nchi ya Uganda ilikuwa ya 87 na Kenya ilikuwa ya  92.Awali Tanzania ilikuwa ya 82 wakati Kenya ilikuwa ya 78 naUganda 79 katika mchakato huo vitu vitatu viliangaliwa pia  uimara wa uchumi, ubora wa taasisi za umma na utayari wa kiteknologia..
Tanzania ilioneshwa kuwa na uimara mkubwa wa taasisi za umma  na kuwa na nafasi ya 60, wakati uimara wa Uchumi ilikuwa ya 72 na utayari wa kiteknologia..ilikuwa nchi ya 86

 

Katika mafanikio ya ushirikiano wa Rais Wabunge na Madiwani wa serikali ya awamu ya tatu, nitatoa mfano mmoja tu wa mapambano dhidi ya  adui wetu mkubwa yaani ujinga,..Sera  ya CCM juu  ya Elimu inasema hivi:Ili elimu yeltu iwe kweli nyenzo ya msingi katika jitihada za kujenga uchumi wa kisasa wa taifa linalojitegemea na kuwawezesha kiuchumi wananchi haina budi ipewe mwelekeo wa kukuza ubunifu na mbinu za kutatua matatizo, na kujenga utamaduni wa matumizi ya sayansi na teknolojia kuanzia ngazi za chini. Aidha, mwelekeo huo uzingatie falsafa ya msingi ya Elimu ya Kujitegemea.

 

Katika kuzikabili gharama kubwa za utoaji wa elimu hasa katika mwelekeo huu mpya, itabidi Serikali iongeze kipaumbele katika bajeti ya elimu na pia kuimarisha  zaidi  shirkiano(“partnership”) na wahisani, sekta ya binafsi na jamii kupitia vyombo na taasisi zake mbali mbali (k.v. NGOs. Jumuiya za Wananchi,n.k) Aidha, itabidi jitihada ziongezwe za kuwaelimisha wazazi juu ya jukumu lao la msingi la kuchangia gharama za elimu ya  watoto wao na kuweka utaratibu wa kuwasaidia wale wasiokuwa na uwezo. Katika kipengele hiki , ni vigumu sana kwa taifa kufanikiwa endapo hakutakuwa na uhishirikiano kati ya wananchi na kwa maana ya wazazi wa watoto, uongozi wachama tawala  kwa maana ya watu hao watatu, Diwani, mbunge na rais wa serikali.Kama rais atapata kura nyingi za kutosha na madiwani pamoja na wabunge wa chama chake wakakosa  kura  katika majimbo yao ya uchaguzi , hakuna kitakachowezekana kwa kuwa itakuwa ni sawa na ule msemowa wahenga usemao figa moja  haliinjiki chungu.

 

Wataalam wanatuelezea kwamba Uchumi wa Tanzania umekuwa ukibadilika mwaka hadi mwaka. Kubadilika huku kwa uchumi kumetokana na mabadiliko ambayo yamekuwa yakijitokeza ndani ya nchi na nchi nyingine duniani. Tanzania sio kisiwa katika dunia hii ambacho kitapitwa na mabadiliko hayo, hivyo nayo imeathiriwa kwa namna moja au nyingine.Tunapozungumzia uchumi tuna maana mfumo mzima wa uzalishaji mali, matumizi (consumption) na ugawaji/usambaji wa mazao  hayo pamoja na huduma. Uchumi unazungumzia pia kudhibiti rasilimali, kugharamia mapato na matumizi ya jamii, biashara na viwanda. Kwa maana hiyo uchumi wa dunia umekuwa unabadilika hasa kwa kuongezeka kwa ushindani katika masoko ya dunia pamoja na kuongezeka kwa kasi ya maendeleo ya sayansi na teknolojia. Nchi ambazo zitashindwa kwenda sambamba na mabadiliko hayo zina hatari ya kuathiriwa  vibaya na kuzidi kuachwa nyuma kimaendeleo.

 

Mafanikio ya jitihada za Serikali ya Awamu ya Tatu ya CCM katika kuzingatia mambo hayo, na kuboresha uchumi, ni dhahiri. Tumefanikiwa kuongeza maradufu ukuaji halisi wa uchumi wetu kutoka 3.6% mwaka 1995 hadi 6.7% mwaka 2004. Matarajio ni ukuaji wa 6.9% mwaka huu, 2005. Mfumuko wa bei umeshuka kutoka 27.4%  mwaka 1995 hadi kufikia 4.2% mwezi Juni 2005.  Akiba ya fedha za nje leo ni kubwa kuliko wakati wowote ule katika historia yetu. Uchumi wetu sasa umejengwa katika misingi imara, na unao uwezo wa kuhimili misukosuko ya ndani au nje ya nchi. Mafanikio ya ukuaji wa uchumi wetu pia yameimarisha ukusanyaji mapato. Wakati Serikali yangu inaingia madarakani, tulikuwa tunakusanya wastani wa mapato ya kodi Sh.25 bilioni kwa mwezi.  Sasa mwelekeo ni kukusanya zaidi ya Sh.150 bilioni kwa mwezi, yaani zaidi ya mara sita ikilinganishwa na 1995. Haya ni mafanikio ya kujivunia kwa Serikali na wananchi wake, na ni sifa kwa utendaji wenu Lakini kama si kwa usimamizi wa viongozi makini wa  chama cha CCM kwa Maana ya Diwani mbunge na Rais hayo yangekuwa na dosari na tusingefika hapo tulipo.

 

Ni kweli kwamba kuna nyufa ndogo za umasikini katika jamii ya watanzania,lakini kama tutakuwa makini katika kufanya maamuzi sahihi juu ya viongozi hao watatu, nyufa hizo zitazibika  kwa kipindi kifupi kama dalili njema zilivyojionyesha katiaka awamu ya tatu ya uongozi  wa CCM. Maadam tuwe na Imani madhubuti kwa hao waliopitishwa kugombea uogozi,, na sisi wenyewe kwa wenyewe tuaminiane. Wananchi tukiaminiana tutaleta kile kinachoitwa mtaji wa kijamii (social capital). Kuaminiana ni mtaji kwa sababu kunawezesha watu kushirikiana katika kutatua

matatizo mbalimbali -,ya kijamii, kiuchumi na kisiasa. Mtaji wa kijamii ukiwa mkubwa, uwezo wa umaskini kuleta rabsha katika siasa unapungua, au kuisha kabisa. Kadhalika, imani ya wananchi kwa viongozi au serikali huleta kile kinachoitwa mtaji wa kisiasa (political capital). Penye mtaji mkubwa wa kisiasa malalamiko ya wananchi yanapungua (au yanasemwa chini chini kwa sauti ndogo) na hivyo rabsha za kisiasa zinapungua

 

Kwa nia njema na ufanisi katika uchaguzi wa mwaka 2005-2010 kama tusipokuwa makini kuhakikisha safu yetu ya wagombea wa CCM wote wanapata kura na kibali cha kuwatumikia watanzania itakuwa ni sawa na lile zoezi la wataalamu wa kilimo  wanapojitahidi kubebesha (buding) kwa baadhi ya mazao kwa kutegemea kupata mazao bora na mengi na bora zaidi na kujikuta kile kitawi kinanyauka au ksababisha hata lile shina mama kufa kabisa kwa ajili ya misukasuko iliyotokea katika ubebeshaji usiozingatia utafiti na ushauri wa kutaalam Tusifanye makosa ya namna hiyo katika kupiga kura ,kwa kuwachagua viongozi watakaokuwa kikwazo cha maendeleo,na utekelezaji wa ilani za chama  zenye lengo la kuleta ufanisi na maendeleo kwa watanzania kwa kuangalia  mfano mmoja wa  wa ilani ya uchaguzi wa mwaka 2005-2010,

Sura ya nane kipengele cha 120 cha ilani ya CCM, kinazungumzia wanawake na kuahidi kuwa katika kipindi cha 2005 hadi 2010,ambapo inaahidi kuzielekeza serikali zake, kutekeleza mambo mengi ikiwa ni pamoja na kuongeza ushiriki wao katika ngazi mbalimbali za uongozi. Chama kinakusudia kuwashirikisha wanawake kiutendaji na katika kufanya maamuzi ili kufikia asilimia 50 ifikapo mwaka 2010, kama inavyoelekezwa na mkataba wa Umoja wa Afrika (OAU)Pia Chama kinaahidi kuongeza nafasi za viti maalumu katika chaguzi za mitaa, vijiji , kamati za zahanati, nkkamati za bunge na za taifa , ubunge na uwakilishi, CCM katika muda huo, inaahidi kukamilisha majadiliano ya kuwezesha kuanzishwa benki ya maendeleo ya wanawake. Kipengele cha 66, cha Sura ya Sita inazungumzia huduma za jamii, na suala la elimu afya maji na maendeleo ya makazi sula la afya limezungumzia  ambapo raia wengi  wa  nchi hii, au wanawake wanaahidiwa kimaandishi kuwa serikali itashughulikia suala la afya za wanawake ili kupunguza vifo vya wazazi “Kupunguza vifo vya watoto wachanga waliozaliwa hai pamoja na wale wenye umri wa chini ya miaka mitano. Kupunguza vifo vya wazazi kutoka 529 katika kila wazazi 100,000 na kuongeza kiwango cha wazazi kuzalishwa na wakunga waliopata mafunzo bora …”

Ilani ya NCCR -Mageuzi inaahidi kujenga usawa baina ya jinsia ya kiume na kike, kutokomeza maonevu ya kihistoria na mila potofu zinazodhalilisha wanawake. Inaahidi kuwapa nafasi na fursa maalumu, ili kuboresha athari za maonevu waliyopata katika historia. Inazungumzia kuwawezesha kutumia vifaa vya kisasa majumbani, ili iwe rahisi kwa jinsi zote kushiriki katika kazi za kuhudumia familia. Inatoa ahadi ya kuundwa benki ya kuwakopesha wawekezaji wanawake itakayoendeshwa na wanawake. Kwa upande wa siasa, itakuwa na idadi iliyo sawa ya wanaume na wanawake katika vyombo vya uwakilishi, na kupanua mfumo wa uwakilishi wa uwiano. Kuridhia na kutekeleza mikataba yote ya Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kwa manufaa ya Watanzania, ili kujenga jamii yenye kutamalaki uvunjwaji wa haki za binadamu na yenye kufurahia usawa kati ya wanaume na wanawake na kuwaweka katika ngazi mbalimbali muhimu za uongozi

 

Tukumbushane sasa kila mtu na mwenzi wake tusifanye kosa la kumchagua Rais na tukawaacha wawezeshaji wake wakuu yaani , Wabunge na madiwani wa CCM vinginevyo tutashindwa kuujenga ule mnara wa babeli kwa kukosa lugha inayofanana katika kufanya maamuzi sahihi ya maendeleo ya nchi yetu na watu wake. Au tukashindwa kupata mavuno mengi kwa kushindwa kuzingatia tafiti na maelekezo ya wataalam.

 

Flora Rugambarara na Cosmas Bahali

Nguvu ya Hoja,

Abiyani Chuo Kikuu cha Dar es Salaam