WAPINZANI FUNGUENI MACHO MUONE MAENDELEO YALIYOLETWA NA CHAMA CHA MAPINDUZI
Katika
kipindi hiki cha uchaguzi hasa wakati huu wa kampeni
imekuwa ni jamabo la kawaida kwa kila mpinzani anayesimama jukwaani kujinadi,
kuelezea mapungufu ya CCM tu bila ya kuelezea ni kitu gani atawafanyia wananchi
wananchi kwa ajili ya maendeleo yao: Si vibaya sana kufanya hivyo ila tukumbuke kuwa unapoelezea
mapungufu fulani uwe umetangulia kuelezea mafanikio ya taasisi husika.
Hivi ni
kweli kuwa CCM haijafanya lolote la maana katika kipindi chote ilichotawala kama ambavyo wanadai wapinzani? Je Tanzania tuliyonayo hii ya leo ndiyo ile ile iliyoachwa na Wakoloni? Au ndiyo ile
ile ilyokuwa kabla ya kuzaliwa kwa chama cha
Mapinduzi? Ni kweli kuwa
mboni za macho ya upinzani hazioni kabisa Neema ya maendeleo
yaliyoletwa na chama cha mapinduzi? Tunachelea kusema kwamba wapinzani wanakope
nzito zinazofunika kabisa mboni za macho yao na kuyazuia yaone mema ya chama cha Mapinduzi. Labda tuwasaidie wapinzani kwa
kuwaonesha maendeleo ya dhahiri yaliyofanywa na serikali ya awamu ya tatu ya
chama cha Mapinduzi.
Imekuwa kawaida kwa
wapizani kuwadanganya wananchi kwamba Serikali ya CCM imeshindwa kuwapatia
watoto wao elimu. Lakini takwimu inaonyesha kwamba idadi ya wanafunzi wa shule za msingi imeongezeka kutoka milioni tatu na nusu
mwaka 1995 na kufikia zaidi ya milioni saba na nusu kwaka 2005. Wakati huo huo
wanafunzi wa shule za secondary wameongezeka zaidi ya
maradufu kutoka wanafunzi 190,000 mwaka 1995 hadi wanafunzi 520,000 mwaka 2005.
Serikali ya chama cha Mapinduzi
haikuishia kwenye elimu za msingi na sekondari tu, bali hata elimu ya juu
iliangalia kwa umakini . Serikali ya CCM imeongeza idadi ya wanafunzi
wa vyuo vikuu kutoka wanafunzi 7785 mwaka 1995 hadi kufikia wanafunzi 32,181
mwaka 2005. Ili kuhakikisha kuwa kila mtoto anapata elimu, Serikali
ya Chama cha Mapinduzi imefuta ada kwa shule za msingi
na kupunguza kwa kiasi kikubwa ada ya shule za sekondari. Je
wapinzani hawajayaona haya maendeleo katika sekta ya elimu? Na kama wanayaona mbona hawayazungumzii hata kidogo? Au
maendeleo wanayotaka wao ni ya aina gani?. Kama kweli wanawatakia mema wananchi, ni vyema wapinzani
wanyanyue ndimi ndimi
za vinywa vyao kuelezea maendeleo haya.
Wapinzani wanadai serikali ya CCM
haikufanya lolote katika sekta ya afya: Hivi ni kweli
hawana macho ya kuona wala masikio ya kusikia mambo yanayofanywa na Serikali ya
CCM katika kuendeleza sekta ya afya? Tunashawishika kusema
kwamba Wapinzani wameweka pamba masikioni mwao. Na hizo pamba si za kawaida
kwani zinachuja mambo kadhaa na kuruhusu yale
wanayopenda kuasikia na kuyanena wao.
Hata hivyo hatuchoki na hatutachoka kuwakumbusha na kuwaeleza wapinzani maendeleo
yaliyofanywa na serikali ya CCM katika Serikali mbalimbali. Wapinzani
tuambieni ya kwamba kipindi cha Serikali ya awali ya Tatu kimetoa mfano mzuri
ya mafanikio katika sekta ya Afya. Kwa mfano upatikanaji wa dawa katika hospitali, vituo vya afya na Zahanati za
Serikali umeongezeka sana kwa vile kiasi cha fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa
na vifaa kimeongezeka kutoka shilingi bilioni kumi mwaka 2000 hadi shilingi
bilioni 30 mwaka 2004/05. Aidha huduma za chanjo kwa watoto umeinarika na
kuongezeka kutoka asilimia 30 mwaka 1995 hadi asilimia 90 mwaka 2004. Pia
wilaya zote miepatiwa x-ray, ultra sound machine na
majokofu mapya. Mbona wapinzani hamtaki hata kidogo kuyatupia macho haya? Au mlizaliwa kwa ajili ya kukosoa tu?
Tunatambua ya kwamba suala la
upatikanaji wa maji ni tatizo sugu katika sehemu kubwa
ya bara la Afrika na duniani kwa ujumla. Hata hivyo serikali
ya CCM imefanya kazi nzuri katika sekta ya maji kwa kupanua na kuongeza
upatikanaji wa maji nchini na pia kwa
kuanzisha miradi mikubwa ya maji kama ule wa kutoa maji ya ziwa Victoria na kuyapeleka
katika mkoa wa Shinyanga, mradi wa maji wa Chalinze katika Mkoa wa Pwani na
mradi wa maji wa Dodoma mjini. Serikali ya awamu ya tatu ya CCM imewezesha
visima vingi vya maji kuchimbwa na visima hivi
vinatumiwa hata na Wapinzani wenyewe:
Lakini bado wapinzani wamekuwa wakiwaeleza wananchi kwamba CCM
haijafanya juhudi zozote katika kuwapatia huduma ya maji.
Hivi huku kama sio kukosa shukurani ni nini? Wapinzani wanaoga,
wanafua na wanakunywa maji hivi hawajiulizi yametokea wapi? Au
wanayafuata wenyewe kwenye vyanzo vyake? Ni dhahilri kuwa Wapinzani
hawana tofauti na mtoto anayemfinya mama yake mashavu hali ya kuwa amebebwa mgongoni kwa mama huyo.
Tunawashangaa sana wapinzani wanapoona tu sehemu za barabara na madaraja
zenye kasoro na kutoona kabisa barabara nzuri na madaraja ya kuvutia
yaliyotengenezwa na serikali ya CCM.
Huko nyuma
tulizoea Wapinzani wakiongelea kero ya usafiri katika kivuka cha mto Rufuji.
Cha ajabu ni kwamba baada ya serikali ya CCM
kutengeneza daraja imara lililoondoa kabisa kero ya usafiri mto Rufiji hakuna
hata upinzani mmoja aliyeruhusu kinywa chake kupongeza jambo hilo. Au hilo daraja limeshishwa kutoka Mbinguni? Tuseme wapinzani
hawajawahi hata siku moja kusafiri kupitia Rufiji tangu daraja hilo kujengwa? Na kama ni hivyo basi tuanachukua nafasi hii kuwafahamisha
wapinzani kuwa sa Rufiji kuna daraja daraja zuri sana lililojengwa kwa juhudi za serikali ya CCM waende
wakalione. Pia kuna madaraja mengi tu makubwa na
madogo madogo yaliyojengwa chini ya serikali safi ya CCM na wapinzani wanayafahamu.
Tunaomba wapinzani waache unafiki na kuwa eleza wananchi kinagaubaga jinsi serikali ya CCM
ilivyoziwezesha sekta binafsi kuchangia kuleta maendeleo ya nchi yetu: seckta
binafsi imenezeshwa kupunguza kero mabalimbali kama vile kero ya usafiri, elimu na afya: sasa hivi tunashuhudia
jinsi miji mbalimbali ya nchi ilivyopambwa a daladala nyingi zinazotoa huduma
ya usafiri kutoka eneo moja hadi lingine. Boti ziendazo kwa
kasi zinatoka huduma nzuri na za haraka katika miji ya Da-es-salaam, Unguja na
na hivi karibuni mikoa ya Mwanza na Bukoba: Shule za watu binafsi na vyuo vya
elimu ya juu vimeongeza idadi ya Watanzania wanaopata Elimu. Zahanati vituo vya
afya na hata hospitali za watu binafsi nazo zimesaidia kuboresha huduma ya afya kwa
watanzania. Huduma hizi tunauhakika hata
wapinzani wanazipata ila tunashangazwa na tabia yao ya kudharau na kubeza maendeleo yaliyofanyika chini
ya serikali ya CCM.
Tunashangaa sana tunaposikia wapinzani wakibeza maendeleo
yaliyofanywa na CCM katika kuimarisha sekta ya mawasiliano.
Ni
dhahiri kwamba chini ya utawala bora wa serikali ya
CCM mawasiliano ya aina zote yameismarishwa kwa kiasi kikubwa. Sasa hivi idadi kubwa ya watanzania wanamudu
kuwasiliana na ndugu na jamaa zao, katika mikoa
tofauti na hata nje ya nchi kwa urahisi mno.
Chini ya utawala wa CCM makampuni mbalimbali ya
simu na mawasiliano mengine yameweza kueneza huduma hii muhimu mpaka katika
baadhi ya vijiji. Wapinzani wenyewe
wanawasiliana sana tu kwa kutumia simu za viganjani. Na cha ajabu ni pale
wanapotumia mawasiliano hayo hayo kubeza maendeleo yaliyoletwa kutokana na
kuimarishwa kwa huduma za mawasiliano.
Hapa tatutokosea tukiwalinganisha wapinzani na
mtu anaekata tawi la mti alilolikalia.
Wapinzani
wanatumia utitiri wa vyombo vya habari kueneza
propaganda zao, lakini wanasahau kuwa wingi huu wa vyombo vya habari umetokana
na utawala makini wa CCM. Chini ya
utawala wa CCM vyombo vya habari vimeongezeka kwa
kiasi kikubwa mno, idadi ya magazeti, redio, na hata vituo vya television vya
watu binafsi vimeongezeka kwa kiasi kikubwa mno. Ongezeko hili la vyombo vya habari,
linakwenda sambamba na uhuru wa vyombo vya habari
unaochochewa na demokrasia imara iliyojengwa chini ya utawala imara wa Chama
cha Mapinduzi. Chaajabu ni pale wapinzani wanapodhubutu kuudanganya umma wa
watanzania, kuwa CCM haikufanya lolote katika kuimarisha huduma hii itolewayo
na vyombo vya habari. Au wapinzani
walitarajia kuwaona na kuwasikia viongozi wa CCM
wakitangaza vipindi mbalimbali kwenye Television na radioni ndipo waamini
kwamba CCM inajali vyombo vya habari?
Maendeleo
na ustawi wa jamii yoyote hutegemea kwa kiasi kikubwa
amani na utulivu katika jamii husika. Serikali za awamu zote
za CCM. Zilijitahidi na zilifanikiwa
kuhakikisha kuwa jamii ya watanzania wote bila kujali itikadi zao, rangi na
imani zao inaishi katika mazingira mazuri ya amani na utulivu. Wapinzani kwa
nyakati tofauti wamekuwa wakibeza sera ya CCM ya kuwahakikishia wananchi wa Tanzania amani ya kudumu na utulivu wa uhakika; Wapinzani wakumbuke ya kwamba ni amani
iliyojengewa mazingire mazuri na CCM inayowawezesha hata wao kusimama majukwani
na kunadi sera za vyama vyao. Serikali
ya chama cha mapinduzi imedumisha amani na utulivu
ndani na nje ya mipaka yetu.
Tukiwasikia wapinzani wanasema amani iliyolindwa na
CCM wakati inawanufaisha hata wao, tunakumbuka usemi wa wahenda usemao “baniani
mbaya kiatu chake dawa”.
Tukiwasikiliza
wapinzani wanapokuwa majukwaani tunashawishika kujiuliza je wapinzani ni malaika ambao daima huwa sahihi kwa asilimia mia
moja? Je wapinzani huwa
hawakosei hata sikumoja?
Hatutaki kuwakumbusha wananchi watanzania juu ya wale wabunge wawili kwa
tiketi ya chama kimoja cha upinzani waliotumia madaraka yao kwenda kinyume na maadili ya bunge na
hatimaye kulidhalilisha bunge letu na nchi yetu mbele ya uso wa kimataifa. Je hii ndiyo staili
wanayoitaka wapinzani? Kama wao kweli huona mapungufu tu mbona
hili hawalisemi? Au wamesahau?; wengine kwa kukosa
hoja wanadai eti viongozi wengi wa CCM
in wazee, hivyo hawafai, wakumbuke kuwa
umri na rangi ya paka si hoja mradi anakamata panya.
Nguvu
ya Hoja,
Abiyani Chuo Kikuu.