RAIS MKAPA AMTEUA NDUGU CHARLES MAKONGORO NYERERE (CCM) KUWA MBUNGE
Rais
Benjamin Mkapa, amemteua Ndugu Charles Makongoro Nyerere kuwa Mbunge.
Taarifa
ya Ikulu ilisema uteuzi huo unaanza rasmi Jumatatu ijayo. Rais Mkapa amefanya uteuzi huo kulingana na kifungu
cha 66(1)(e) kinachompa madaraka ya kuwateua Wabunge wasiozidi kumi kulingana
na sifa zilizoainishwa katika Katiba.
Ndugu
Makongoro anakuwa Mbunge wa kumi wa kuteuliwa na kwa hiyo anatimiza idadi ya
Wabunge ambao Rais anapaswa kuwateua kwa mujibu wa Katiba.
Wengine
ni Ndugu Kingunge Ngombale-Mwiru (CC), Ndugu Omar Ramadhan Mapuri (CCM),
Brigedia Jenerali (mstaafu) Hassan Ngwilizi (CCM) na Ndugu Hamad Rashid Mohamed
(CUF).
Taarifa
iliwataja wengine kuwa ni Dkt. Abdulkader Shareef (CCM), Chifu Abdallah
Fundikira (CCM), Bi Anne Kione Malecela (CCM), Dkt. Masumbuko Lamwai (CCM) na
Bi Mwaidi Hassan Makame (CCM).