HOTUBA YA NDUGU OMAR R.
MAPURI, KATIBU WA ITIKADI NA UENEZI WA CCM ALIYOITOA KWENYE MKUTANO MKUU WA
WANASALAMU WA RADIO UHURU
TAREHE 11 JUNI, 2006
MJINI KISARAWE
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa
Pwani, Ndugu Mwinshehe Mlao,
Katibu wa CCM wa Mkoa wa
Pwani, Ndugu Amina Makilagi,
Katibu wa CCM, Wilaya ya
Kisarawe, Ndugu Sofia Kilingo,
Ndugu Urembo Mawamba, Mwenyekiti
wa Wanasalamu na Mjumbe
wa Bodi ya Wakurugenzi ya Radio Uhuru,
Ndugu Juma
Ndugu Wanasalamu wa Radio
Uhuru,
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana.
Utangulizi wa Pongezi
Awali ya yote, napenda kuchukua fursa hii kukupongezeni kwa dhati
kabisa Wanasalamu wote wa Radio Uhuru kwa kuandaa mkutano wenu huu mkuu ambao
unakukutanisheni Wanasalamu kutoka maeneo yote ya nchi inakosikika Radio
Uhuru. Kufanikiwa kwa mkutano huu ni
kielelezo wazi cha kushamiri na kuendelea kuimarika kwa umoja na udugu wa
familia hii kubwa ya Wanasalamu wa Radio Uhuru.
Mpaka sasa sina taarifa ya kuwepo kwa umoja wa aina hii wa wasikilizaji
wa Radio nyingine yo yote nchini, zaidi ya Radio Uhuru. Wala sina taarifa ya kuwapo kwa umoja wowote
wa watazamaji wa televisheni wala wa wasomaji wa magazeti. Umoja wenu ni wa aina ya pekee nchini, na kwa
Yote haya na mengine mengi ambayo sikuyataja yameujenga umoja wenu hadi
kufikia hatua ya udugu wa kifamilia, au
upendo mmoja aliouzungumzia Bob Marley katika wimbo wake wa “One Love” aliouteua
Mwenyekiti Mawamba katika tangazo lake la mkutano huu. Sasa hivi tunazungumzia siyo mtandao tu, bali
familia ya Wanasalama na wasikilizaji wengine wa Radio Uhuru. La kufurahisha zaidi ni kwamba mmewaingiza na
watangazaji na watumishi wengine wa Radio Uhuru katika familia hii kubwa,adhimu
na ya aina yake. Hii sasa ndiyo inakuwa
familia ya Radio Uhuru. Huwezi kukuta pengine popote mtandao mkubwa wa
kifamilia wa aina hii zaidi ya Radio Uhuru.
Nakupongezeni tena na nina fahari kubwa nanyi.
Shukrani
Baada ya maelezo hayo ya pongezi, sasa napenda kuwashukuru waandalizi
wa mkutano huu kwa kunitunuku fursa hii
ya kuwa mgeni rasmi. Ulipofikishwa
kwangu mwaliko na Mwenyekiti Mawamba niliupokea
Historia Fupi ya Umiliki
wa Radio Uhuru
Radio Uhuru ilianzishwa kwa mara ya kwanza na makada wa CCM mwaka 1999
kwa malengo ya msingi ya kibiashara lakini pia kuipatia CCM fursa ya kuitumia
kwa shughuli za kiuenezi kwa kiasi fulani.
CCM iliitumia fursa hiyo wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa
2000. Hata hivyo, kwa vile Radio haikuwa
ya CCM na wamiliki japokuwa walikuwa makada wa CCM lakini walifungika na
maadili ya utangazaji wakati wa uchaguzi, fursa ya kuitumia Radio ilitolewa pia
kwa vyama vingine.
Baada ya Uchaguzi Mkuu kumalizika, wamiliki wa Radio Uhuru
walielekea zaidi kwenye biashara na
mwaka 2002 waliamua kuuza sehemu kubwa ya hisa zao kwa kampuni moja ya nje ya
nchi. Wamiliki wapya waliibadilisha jina
na mwelekeo Radio hiyo ambapo sasa iliitwa Uhuru FM na vipindi vikabadilika
kabisa na hata watangazaji sawia.
Kwa upande wa pili, CCM nayo baada ya mauzo hayo, ilijikuta imeondokewa
na chombo muhimu cha uenezi ilichokuwa imeanza kukitegemea. Mwaka 2004, CCM ilipitisha uamuzi wa kuwa na
Radio yake yenyewe badala ya kutegemea tu fadhila. Baada ya kuzingatia ukweli kwamba Radio Uhuru
ya awali ilikwishajulikana na kuzoeleka
na kuwa tayari ilikwishakuwa na mtandao
wa wasikilizaji madhubuti, CCM iliwakabili wamiliki wa Uhuru FM ili
waiuzie. Kwa bahati ilisadifu pia kuwa
hata wao walikuwa tayari wanafikiria kuiuza Radio hiyo baada ya kubaini kuwa ilikuwa
imekimbiwa na wasikilizaji. Waliona
ingekuwa bora zaidi kuanzisha Radio
Ilikuwa ni katika mazingira hayo ndipo CCM ilipoamua rasmi kuinunua
Radio Uhuru mwaka 2004. Lakini hata
baada ya uamuzi huo, CCM ilikuwa bado na mtazamo wa kutoonekana inaimiliki na
kuiendesha moja kwa moja Radio hiyo. Kwa
hivyo iliikabidhi kampuni moja kuinunua na kuiendesha Radio hiyo kwa niaba
yake. Kampuni hiyo nayo ikaunda kampuni
tanzu ya Peoples’ Media Communications Limited (PMCL) ya kuiendesha Radio hiyo.
Kwa bahati mbaya, utaratibu huo wa umiliki na uendeshaji ulitoa mwanya
kwa migogoro ya kiuongozi na kiutendaji iliyoathiri ufanisi na hata kuhatisha uhai wa Radio Uhuru, ambayo
sina haja ya kuifafanua hapa. CCM
ikaunda Kamati ya Kupendekeza Utaratibu Bora wa Kuendesha Radio Uhuru – maarufu
kwa jina la Kamati ya Mikidadi kutokana na jina la Mwenyekiti wake, Ndugu Mikidadi Mahamoud, Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Ilala.
Kamati hiyo iliwasilisha mapendekezo yake Chamani na Chama kikapitisha
utaratibu mpya wa kumiliki na kuendesha Radio Uhuru kwa kuzingatia mapendekezo
hayo mwezi Aprili, 2006. Vifuatavyo ni
baadhi ya vipengele vya msingi vilivyo sehemu ya utaratibu huo:-
·
CCM sasa inaimiliki moja kwa
moja Radio Uhuru badala ya kumiliki kupitia kampuni iliyo mtu wa tatu (third party).
·
Kampuni ya PMCL ambayo imepewa
jukumu la kuendesha Radio Uhuru, inamilikiwa moja kwa moja na CCM na si kampuni
tanzu tena ya kampuni nyingine.
·
Bodi ya Wakurugenzi ya Kampuni
hiyo inateuliwa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM. Uteuzi wa Bodi ya kwanza tayari
umekwishafanywa ambapo Mwenyekiti wake ni gwiji la Itikadi na Uenezi la Chama,
Mhe. Kingunge Ngombale-Mwiru, na Wanasalamu wana uwakilishi wao kupitia
Mwenyekiti wao Mzee Urembo Mawamba.
·
Mkurugenzi Mtendaji wa Radio
Uhuru anateuliwa na Kamati Kuu. Uteuzi
wa Mkurugenzi Mtendaji wa kwanza tayari umekwishafanyika ambapo ameteuliwa kada
aliyewiva, Ndugu Juma Penza.
·
Radio Uhuru tayari ina muundo
wake wa utumishi ambao utaanza kutumika wakati wowote kuanzia sasa.
·
Inatarajiwa kwamba Bodi
itapendekeza kwa Chama, sera ya utangazaji ya Radio Uhuru, ambayo bila shaka
itaegemea kwenye uenezi wa sera za Chama pamoja na kutekeleza majukumu ya
kuelimisha, kuburudisha na kuwafikishia habari wananchi.
Historia Fupi ya
Mabadiliko ya Mtazamo wa Chama Kuhusu Umiliki wa Radio Uhuru
Lakini pia hata tulipoamua kununua Radio yetu tukaanza na wazo la
kuuficha umiliki wetu.
Lakini hofu zote hizo zilikujabainika baadaye kuwa hazikuwa za
msingi.
Lakini zaidi ya hivyo, wasikilizaji walifurahi
Jambo
Ilinidhihirikia zaidi kwamba Wanasalamu wengi wa Radio Uhuru kumbe ni
wanachama, mashabiki, wanaharakati na baadhi
Ni katika mazingira hayo ndipo liliponijia wazo la haraka haraka la
kuitumia nguvu hiyo kubwa ya uhamasishaji niliyoigundua miongoni mwenu, katika
kueneza sera za CCM.
Ndipo nilipoanza kwenye mikutano hiyo kukuombeni kuipigia debe CCM
wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu tuliokuwa tunautarajia mwishoni mwa mwaka
huo.
Nataka nichukue fursa hii kwa mara nyingine tena, kukushukuruni kwa
dhati kabisa kwa jinsi mlivyonitekelezea ombi langu kwa uwezo na ufanisi mkubwa
mpaka CCM tukapata ushindi wa kishindo uliotuduwaza wote sisi na wapinzani
wetu.
Mambo yote yaliyoziviza hofu zilizokuwapo kuhusiana na kuitambulisha
Radio kuwa ni
Matokeo ya Kuweka Bayana
Umiliki wa Radio Uhuru
Matokeo ya uamuzi wa Chama wa kuweka bayana umiliki wake wa Radio Uhuru
na kuiwekea utaratibu unaoeleweka ni kwamba tumeweza kufanya mengi ya faida
yakiwemo yafuatayo:-
·
Tuliitumia Radio Uhuru kwa
ukamilifu, kwa nafasi na kwa raha zetu katika kampeni za CCM za Uchaguzi Mkuu
uliopita. Mafanikio kila mmoja anayaona.
·
Wanasalamu wa Radio Uhuru
walijitokeza wazi wazi bila ya hofu na
kwa hamasa kubwa kuipigia ndogo ndogo na kubwa kubwa CCM wakati wakisalimiana
na kubadilishana mawazo kupitia vipindi
karibu vyote vya Radio Uhuru.
·
Watangazaji wa Radio Uhuru nao
walijitanafasi kuipigia kampeni CCM wazi wazi na bila ya woga kwenye vipindi
vyao karibu vyote.
·
Wasanii wengi wakahamasika na
kujitokeza kutunga nyimbo za kisiasa za kuinadi CCM, wagombea wake na sera zake
kwani ilipatikana Radio ya kuzipiga, na hivyo na wao kujitambulisha kwa umma.
·
Toka wakati huo, kutokana na
hamasa iliyojengeka, idadi ya Wanasalamu imekuwa ikiongezeka kila kukicha. Kuna wakati nilikuwa nikiorodhesha wanasalamu
lakini kazi hiyo sasa imenishinda. Kila
siku yanaibuka majina mapya. Hata misamiati
mipya ikaanza kusikika k.v. habari za
unju au kulamku macho au nakwenenda. Halikadhalika majina mapya ya mitaa na vijiji
hasa vya
·
Uamuzi wa kuweka bayana
umiliki wa Chama wa Radio Uhuru umewezesha kuweka uongozi wa Radio kwa
kuzingatia siyo tu taaluma, bali pia ukada na ukereketwa wa Chama. Ndiyo maana tuna Ndugu Juma Penza hapa ambaye
ni kada aliyeandaliwa na Chama Cha Mapinduzi kwa muda mrefu. Amepikwa akapikika. Amefundwa akafundika katika itikadi na
maadili ya Chama.
Matokeo ya Mabadiliko ya Uongozi
Kuletwa kwa uongozi mpya wa Radio Uhuru kumeamsha uhai mpya katika
Radio. Mara tu baada ya kuanza kazi
akiwa Kaimu Mkurugenzi, Januari, 2006, Ndugu Penza alianzisha mchakato kabambe
wa mabadiliko ya kiutendaji na kimwelekeo katika Radio Uhuru. Hadi sasa tumeshuhudia mafanikio mengi
kutokana na mchakato huo yakiwemo
yafuatayo:-
·
Migogoro ya kiuongozi na
kiutendaji imekwisha katika Radio Uhuru.
·
Matatizo mengi ya kiufundi
yaliyokuwapo ambayo yakiwasumbua watangazaji na wasikilizaji yamepata ufumbuzi. Mfano ni lile tatizo sugu la kuwapo kwa line moja tu ya simu. Sasa zipo lines
tano kwa ajili ya matumizi ya Wanasalamu na wasikilizaji wengine wa Radio
Uhuru. Wanasalamu sasa wanajimwaga kwa
nafasi zaidi, licha ya kuongezeka
Hii ni kwa sababu siku hizi inamaliza simu moja inaingia nyingine. Hakuna muda wa kutia goma au vanga ila labda
kwa kulazimisha kwa kuwacha kupokea simu inayongoja. Siku hizi hata wale wasikilizaji waliokuwa na
mtindo mbaya wa kuzuwia line kwa
makusudi kwa nia ya kuhujumu wamekwama, kwani
·
Matatizo mengine yaliyopatiwa
ufumbuzi ni pamoja na lile la usikivu wa Radio Uhuru Arusha na Mwanza. Sasa
akina Mzee Msengesi kule Arusha wamerudi kutamba katika anga za Radio Uhuru na
Jaffari Osama na Omary Ogola wanatoa changamoto kule Mwanza. Aidha, hali ya
vifaa mbali mbali vya studio sasa ni nzuri zaidi. Yote hayo yamewezekana
kutokana na juhudi za Radio Uhuru yenyewe bila ya kutegemea msaada kutoka
Chamani. Huko nyuma, ufumbuzi wa
matatizo hayo ulisubiri fedha kutoka Chamani.
Naomba tumpongeze Ndugu Penza na timu yake ya viongozi na watendaji.
·
Kutokana na Ari mpya, Ndugu
mpya na Kasi mpya iliyoingia Radio Uhuru, sasa umepatikana muda na hata uwezo
wa kushughulikia kwa uhakika zaidi suala la usikivu wa Radio Uhuru katika
maeneo mengine ya nchi yetu. Ni hivi
kesho
kutwa tu, Radio Uhuru itaanza kusikika kwa mara ya
kwanza
·
Hivi sasa vimeanza kusikika
vipindi vya kuelimisha vikiwemo vya dini, elimu ya uraia na vya kujenga mwamko
na kuhamasisha kuhusu maendeleo, n.k.
·
Na kwa upande wa siasa,
kutokana na kazi ya msingi iliyofanywa na uongozi mpya, wafanyakazi wote wa
Radio Uhuru hivi sasa ni wanachama kamili wa CCM na wamekwishafungua Shina la
Chama ambalo Mwenyekiti wake ni Violet Mzindakaya Mpogolo a.k.a Sister V a.k.a Mpiganaji. Pia wamekwishaanzisha darasa la itikadi.
Wito kwa Wanasalamu
Kwa heshima kubwa na taadhima napenda katika hatua hii kutoa wito kwa
Wanasalamu na wasikilizaji wengine wa Radio Uhuru kuendelea kujitokeza na
kushiriki vipindi vyote vya Radio yenu vinavyowapa fursa hiyo kwa njia ya simu,
ujumbe wa simu, barua au hata kwenda studio wanapokaribishwa. Wito wangu huo napenda kuugawa katika maeneo
mahususi yafuatayo:-
·
Kila mtakapohitajika, mjitokeze
kwa hamasa zote kufanya kazi za uenezi wa CCM na sera zake kama mlivyofanya
wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita ambapo mchango wenu kwa ushindi wa
CCM unatambuliwa hata na viongozi wa kitaifa wa Chama na Serikali akiwemo
Mheshimiwa Rais Kikwete mwenyewe. Kazi
kubwa ya sasa ni kuhamasishana katika utekelezaji wa Ilani na kushiriki
shughuli za maendeleo na kupambana na umaskini.
Ndiyo maana nilifurahi
·
Wanasalamu mjitokeze kwa wingi
katika mijadala ya vipindi mbali mbali vya Radio UHuru. Miongoni mwa miongozo ya jumla niliyokwishaitoa
kwa uongozi wa Radio Uhuru ni kwamba kila kipindi kinachoanzishwa ni lazima
kiwe na sehemu ya kuwashirikisha wasikilizaji.
Yaani kwa kadiri inavyowezekana, vipindi viwe shirikishi ili kuwapata
fursa wasikilizaji kutoa michango ya mawazo na hata kuonyesha vipaji vyao. Kwa mfano, kwa utaratibu shirikishi, Kigwa
One amefichua vipaji vya uimbaji miongoni mwa wasikilizaji. Pia Sister V na First Eddy wameweza kufichua
kipaji cha utangazaji cha Amina Midundulu pale walipomwalika studio kushiriki
kuendesha kipindi. Aidha, sina haja ya
kumtaja Zomboko wa Enzi Hizo.
·
Nawapa changamoto Wanasalamu mshiriki
mijadala ya kisiasa na mambo ya kijamii kila mnapopata fursa iwe katika kipindi
cha Radio au hata mitaani. Kwa mfano
suala la maamuzi ya Mahakama Kuu ya kupiga marufuku takrima katika uchaguzi na
kuamuru kuanzishwa kwa utaratibu wa kuwa na wagombea binafsi. Mijadala yote katika vyombo vya habari
iliyofuatia maamuzi hayo ilionekana kuonyesha kuwa Chama Cha Mapinduzi ndicho
kilichokomolewa na kuwa eti ndicho
kitachoathirika. Sijasikia mtu
akikumbusha kwamba hata kabla ya uamuzi wa Mahakama, takrima ya kushawishi
kujipatia kura ilikuwa tayari ni marufuku katika Kanuni za Maadili za CCM. Pia kuhusu suala la wagombea binafsi, mbona
sijasikia mtu akitanabahisha kuwa uamuzi huo utaweza siyo tu kuvisambaratisha,
bali hata kuvimaliza vyama vya upinzani?
Kwa maoni yangu, uwezekano ni mkubwa zaidi kwa vyama vya upinzani
kukimbiwa na wagombea wazuri kutokana na migogoro isiyokwisha ndani ya vyama
hivyo, kuliko ilivyo kwa CCM ambavyo uzoefu unaonyesha kuwa ni mahiri katika
kuyapatia ufumbuzi matatizo kila yanapojitokeza ndani yake. Maeneo haya na mengineyo yako wazi kuchangiwa
mawazo na Wanasalamu na wasikilizaji wengine wa Radio Uhuru.
·
·
Lakini napenda pia katika
hatua hii, kutoa ombi kwa Wanasalamu na wasikilizaji wengine wa Radio Uhuru
kwamba ushiriki wenu katika vipindi vya Radio uzingatie nidhamu. Haipendezi mtu kung’ang’ania line ya simu kwa muda mrefu tena hata
baada ya kuombwa kuacha kufanya hivyo.
Utakuta mtu anataka kuwasalimu watu wote, lakini kutokana na wingi wao,
hawezi kuwamaliza. Mwingine anapiga simu
lakini ikipokelewa hasemi. Haipendezi
wasikililizaji wa
Kuna nyakati atahitajika Mwenyekiti Mawamba au Katibu Jakulanga au
msikilizaji mwingine kupanda kwa dharura ya kutoa tangazo au ufafanuzi fulani. Wasikilizaji wengine watapaoombwa wasipige
simu wakati huo wakubali. Nidhamu na
kuzingatia maadili na kufikiriana na kuhurumiana ni mambo ya msingi katika
kuimarisha udugu na upendo katika familia yetu ya Radio Uhuru. Kwa hivyo wakati wote unaposhiriki katika
kipindi, wafikirie wenzako badala ya kujifikiria wewe tu.
Pongezi
Kwa Watangazaji
Hotuba yangu haitokuwa imekamilika wala sitokuwa nimetenda haki
Wafanyakazi wote wa Radio Uhuru wanaipenda kazi
Watangazaji wanawapenda wasikilizaji wao. Ni wavumilivu
Watangazaji wetu wote ni wabunifu
Kwa yote hayo na mengine mengi yanayohitaji muda kuyaorodhesha
nawapongeza kwa dhati na kuwaomba waendeleze ufanisi na ubunifu ili Radio Uhuru
iendelee kupanda hadhi.
Mwisho
Mwisho, napenda kuwatakia heri wote mlioweza kuhudhuria mkutano huu na
wenzenu wote ambao hawakupata wasaa huo.
Nakuombeni tuendeleze familia yetu hii adhimu na adimu.
ASANTENI