ITIFAKI YA
MATUMIZI YA BENDERA YA
CHAMA CHA MAPINDUZI
1.0.0 UTANGULIZI
1.0.1 Katiba ya Chama Cha Mapinduzi ibara ya 3
inaainisha wazi wazi umuhimu na nafasi ya
bendera
1.0.2 Ni dhahiri basi kuwa bendera hiyo ni alama
muhimu iliyobuniwa ili kuwa kielelezo
cha umoja pamoja na kudhihirisha azma na madhumuni ya CCM ya kutetea haki na maslahi ya wakulima
na wafanyakazi.
1.0.3 Wakati wa mfumo wa chama kimoja, bendera ya Chama
ilitumika kwa matumizi rasmi tu kwenye
ofisi za Chama, magari ya viongozi na ofisini kwenye
meza za viongozi husika n.k. Hata hivyo,
baada ya kuingia kwa mfumo wa
vyama vingi, bendera hiyo imejikuta ikitumika pia kwa shughuli za kiuenezi na hamasa, hasa wakati wa
kampeni za Uchaguzi wa Dola. Katika mazingira hayo, wanachama na
wapenzi wa CCM huitumia bendera hiyo
kwenye baiskeli, majumbani mwao,
vijiweni mwao, kwenye magari
1.0.4 Kwa kuzingatia kwamba matumizi yote hayo yana
manufaa makubwa kwake, Chama kimeamua kutoa
itifaki hii ili iwe mwongozo rasmi wa matumizi
ya bendera hii ya Chama. Kimsingi, itifaki hii inabainisha matumizi mawili makubwa ya bendera hii. Matumizi hayo ni yale rasmi kwa ajili ya ofisi na vingozi wa Chama kwa
upande mmoja, na yale ya uenezi na uhamasishaji kupitia wanachama wa
kawaida, wapenzi na mashabiki wa CCM
kwa upande wa pili.
2.0.0 MATUMIZI
RASMI YA BENDERA YA CCM
2.0.1
Bendera kwa ajili ya matumizi rasmi zitakuwa za aina mbili kuu zifuatazo:-
(a) Bendera za Viongozi Wakuu wa CCM
(b) Bendera za Viongozi Wengine wa Chama na
Majengo ya Ofisi za Chama
2.1.0 Bendera za
Viongozi Wakuu wa CCM
2.1.1 Bendera hizi zitakuwa na utepe wa rangi ya
manjano upande wa mlingoti na zitapambwa kwa urembo wa nyuzi za rangi hiyo hiyo kuizunguka bendera yote ukiondoa ule upande wa
mlingoti utakaokuwa na utepe.
2.1.2 Bendera za aina
hii zitapeperushwa na viongozi wakuu
wafuatao tu:-
(a) Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi.
(b) Makamo wawili wa Mwenyekiti wa Chama Cha
Mapinduzi.
(c) Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi.
(d) Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mgombea Urais wa Zanzibar na Mgombea Mwenza wa Jamhuri kwa
tiketi ya Chama Cha Mapinduzi wakati wa
kampeni ya Uchaguzi Mkuu wa Dola, au chaguzi nyingine zozote ambapo Chama
kitakuwa na Mgombea au Wagombea wa nafasi hizo.
2.1.3 Bendera hizi za Viongozi Wakuu zitatumika
(a) Kwenye gari la Kiongozi kwa kuegeshwa
kwenye mlingoti upande wa kushoto wa mbele wa gari
(b)
Bendera ya aina
hiyo hiyo iliyotengenezwa kwa ajili ya kuwekwa
mezani itakuwa mezani kwenye meza ya ofisi ya Kiongozi
wakati wote kwani ni udhihirisho wa mamlaka yake.
(c)
Bendera ya mezani
itatumika pia na kuwepo mezani wakati wa
mikutano yote ya chama na wakati wa mazungumzo baina
ya CCM na chama au vyama vingine, mfano vyama rafiki
na vya kidugu.
(d)
Bendera kubwa
nyumbani kwa Kiongozi Mkuu na kwa kuegesha
ofisini mwake.
2.2.0 Bendera za Viongozi Wengine wa Chama Na Majengo Ya Ofisi za Chama
2.2.1 Bendera hizi zitakuwa
na utepe wa manjano upande wa mlingoti tu. Hazitokuwa na urembo ule
uliobainishwa kwa bendera za Viongozi Wakuu.
2.2.2 Viongozi wataostahiki kupeperusha bendera hizi kwenye
meza ofisini, magari, pikipiki na
baiskeli ni hawa wafuatao:-
(a) Makatibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa
wanaoongoza Idara za Chama.
(b)
Wenyeviti na Makatibu
Wakuu wa Jumuiya za CCM ngazi ya Taifa.
(c)
Wajumbe wa Kamati Kuu
ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.
(d)
Wajumbe wa Halmashauri
Kuu ya Taifa ya CCM, Wenyeviti na Makatibu wa CCM wa Mikoa na Wilaya.
(e)
Wabunge na Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi wanaotokana na CCM.
(f)
Makatibu wa CCM wa
Majimbo, Kata/Wadi na Matawi.
2.2.3 Ofisi za Chama zitazostahiki kupeperusha
bendera hizi ni za ngazi zote kuanzia Shina (yakiwemo Mashina ya Wakereketwa na
Maskani) hadi Taifa. Ofisi za Jumuiya za
Chama na taasisi nyingine za Chama zitastahiki kupeperusha bendera za Chama za
matumizi rasmi.
2.3.0
Vipimo Vya Bendera
za Chama Kwa Ajili ya Matumizi Rasmi
2.3.1 Bendera
za Chama kwa ajili ya matumizi rasmi zitakuwa na vipimo vifuatavyo:-
|
|
AINA YA BENDERA KWA MUJIBU WA
MATUMIZI |
VIPIMO (milimita) |
|
|
Urefu |
Upana |
||
|
1 |
Bendera za
Mashina |
1350 |
900 |
|
2 |
Bendera za ofisi
nyingine zote za Chama, Jumuiya na Taasisi zake |
1800 |
1200 |
|
3 |
Bendera za
majumbani na kuegesha ofisini kwa Viongozi Wakuu |
1800 |
1200 |
|
4 |
Bendera za
mezani |
220 |
150 |
|
5 |
Bendera za
magari na vyombo vingine vya usafiri |
300 |
200 |
2.4.0 Masharti ya Matumizi Rasmi ya Bendera:-
2.4.1 Matumizi rasmi
ya bendera ya CCM yataambatana na masharti
yafuatayo:-
(a)
Bendera ziwe za vipimo
vilivyobainishwa.
(b) Zitundikwe
kwenye milingoti rasmi. Kwa Mashina ya majumbani zinaweza kutundikwa juu ya nyumba husika kulingana na mazingira ya
pahala.
(c) Kwenye
magari, bendera zipeperushwe kwenye mlingoti
rasmi wa gari, usawa wa mkono wa kushoto
wa gari husika. Bendera iondolewe au kufunikwa
isipepee mara tu kiongozi anapokuwa halitumii kwa muda mfupi au mrefu gari
(d) Kiongozi anapoendesha mwenyewe gari
asipeperushe bendera ya matumizi
rasmi.
(e) Ukiondoa
bendera za kwenye magari ambazo hazitopepea
wakati kiongozi hayumo garini, bendera nyingine zote za CCM zitapepea wakati wote.
Isipokuwa kwamba, pale ambapo bendera ya CCM inapepea sambamba na bendera ya
Taifa, utafuatwa utaratibu wa bendera ya
Taiufa wa kupandisha na kushusha
bendera.
2.5.0 Mtoaji
wa Bendera
2.5.1 Bendera zote kwa matumizi
rasmi zitatengenezeshwa na kutolewa na Makao Makuu ya CCM pekee na zitatengenezwa kwa kutumia vitambaa rasmi vilivyothibitishwa na
Shirika la Viwango (TBS). Vitambaa hivyo ni Pantone 109C (Kijani) na
Pantone 256 C (manjano).
3.0.0 MATUMIZI KWA
AJILI YA UENEZI WA CHAMA
3.0.1 Bendera za CCM kwa ajili ya matumizi ya uenezi
na hamasa hazitokuwa na utepe
wala urembo wa aina yoyote. Zitaweza kutumiwa na wanachama, wapenzi na
mashabiki wa CCM wakati wote ama
kwa kupeperusha wenyewe mikononi, kwenye
baiskeli zao, pikipiki, magari, sehemu zao za kazi, za mazungumzo, nyumbani n.k. Bendera hizi pia ndizo zitakazotumika kwa ajili ya kupamba
maeneo ya mikutano na shughuli
nyingine za Chama.
3.1.0
Masharti
3.1.1 Bendera
hizi hazitohusika na masharti yote yaliyobainishwa kwa ajili ya matumizi rasmi,
isipokuwa yale yaliyoainishwa kwenye Katiba ya CCM kwa mujibu wa Ibara ya 3.
3.2.0
Mtoaji wa Bendera
3.2.1 Bendera hizi zitaweza kutengenezeshwa na/au kutolewa na ofisi za CCM za Mikoa na Wilaya au kwa ruhusa/idhini za ofisi hizo.