MTAALA WA MAFUNZO YA
ITIKADI KWA WANACHAMA
NA VIONGOZI WA CHAMA
CHA MAPINDUZI
Wakati wa mfumo wa siasa wa Chama kimoja, Chama cha
Mapinduzi kilikuwa na utaratibu wa kutoa mafunzo ya itikadi kwa wananchi
waliopenda kujiunga nacho. Wakati huo,
hakuna aliyeruhusiwa kujiunga na Chama
Utaratibu huo uliachwa baada ya
Taathira za hali hiyo zimeanza kujitokeza katika dalili za
kumong’onyoka kwa misingi ya mshikamano wa kiitikadi miongoni mwa wanachama na
viongozi. Zimeanza pia kudhihirika
dalili za kuporomoka kwa maadili.
Dalili hizo zilipoanza kujitokeza, Chama kilianzisha
utaratibu wa kutoa mafunzo kwa njia ya warsha na semina kwa viongozi, hasa
baada ya chaguzi za Chama. Chama pia
kilianza kuhimiza kufufuliwa kwa madarasa ya itikadi matawini ili kutoa mafunzo
kwa wanachama, hasa wale wapya.
Wito kuhusu madarasa ya itikadi uliitikiwa kwa misisimko
tofauti katika maeneo mbalimbali ya nchi kulingana na hamasa na utashi au
mwamko wa viongozi. Yako maeneo ambayo
yamefufua madarasa, lakini pia yapo maeneo mengi tu ambako hukuti vuguvugu la
madarasa ya itikadi.
Kwa upande mwingine, wito wa Chama kufufua madarasa ya
itikadi haukufuatana na kutolewa kwa mtaala mahususi wa kitaifa wa mafunzo
hayo. Matokeo yake ni kwamba hata katika
maeneo yalikofufuliwa madarasa ya itikadi, maudhui ya mafunzo yalitofautiana
kulingana na utashi wa viongozi wa kila eneo.
Hali hii haiwezi kujenga mazingira ya mshikamano wa kiitikadi ndani ya
Chama.
Ni katika jitihada za kuondoa dosari hii, ndipo zilipoanza
juhudi za kutunga mtaala wa kitaifa wa mafunzo ya itikadi kwa wanachama na
viongozi yatakayotolewa katika mdarasa ya itikadi nchi nzima. Matokeo ya jitihada hizo ni mtaala huu
unaoambatishwa na maelezo haya ya utangulizi.
Mtaala huu umepitishwa rasmi na Halmashauri Kuu ya Taifa ya
Chama Cha Mapinduzi katika kikao chake cha tarehe 29-30 Aprili, 2006
kilichofanyika
Inatarajiwa sasa baada ya kupatikana kwa mtaala huu,
vuguvugu la madarasa ya itikadi matawini na katika maeneo mengine ya uongozi wa
Chama litafukuta nchi nzima.
Inawezekana.
Tutimize wajibu wetu.
Omar R. Mapuri,
KATIBU WA HALMASHAURI
KUU YA TAIFA
ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI
MTAALA WA MAFUNZO YA
ITIKADI KWA WANACHAMA
NA VIONGOZI WA CCM
|
SOMO/MADA |
VIPENGELE |
MADHUMUNI |
WALENGWA |
REJEA |
|
1. Historia ya CCM Tangu TANU na ASP |
a) TANU -
Kuundwa kwake - Malengo
na madhumuni ya TANU - Kuenea
kwa TANU -
Kuelekea Uhuru b) ASP -
Kuundwa kwake -
Malengo na madhumuni ya ASP -
Kuelekea Mapinduzi -
Misukosuko iliyokabiliana nayo ASP - Uhuru
wa c) CCM -
Kuundwa kwake -
Madhumuni na sera za CCM - Misukosuko
iliyohimiliwa na CCM |
Kuwaelimisha wanachama na viongozi umuhimu wa Historia ya
CCM – kwamba CCM imetoka wapi, iko
wapi na inakwenda wapi. |
Wanachama
na Viongozi wa CCM |
Historia
ya CCM tangu TANU na ASP |
|
2. Katiba ya CCM |
-Imani
ya CCM -Malengo
na Madhumuni ya CCM -Wajibu
wa Mwanachama wa CCM. -Haki ya
Mwanachama wa CCM. -Ahadi
za Mwanachama wa CCM. |
Kuwaelimisha
wanachama wa CCM na Jumuiya zake, Imani, Madhumuni na malengo ya Katiba ya
CCM. Aidha ni vema viongozi na
wanachama waelimishwe umuhimu wa kuzingatia Kanuni na Katiba ya CCM katika
kutekeleza majukumu |
Wanachama
wa CCM na Jumuiya zake. |
Katiba
ya CCM – Toleo la Mei 2005 Ibara – 4 (1-3) 5 (1-19) 14 (1-5) 15 (1-9) -
Nyongeza “A” ya Katiba ya CCM 2005 |
|
SOMO/MADA |
VIPENGELE |
MADHUMUNI |
WALENGWA |
REJEA |
|
3. Ujenzi wa Chama |
-Kazi ya
Chama ndani ya Chama -Kazi ya
Chama ndani ya jamii. -Jumuiya
za CCM Uhai wa Chama. -Tathmini
ya Uhai wa Chama katika Matawi na Mashina. |
Kuwaelimisha
wana-CCM umuhimu wa Uhai wa Chama kwa lengo la kushinda Uchaguzi |
Wanachama
na Viongozi wa CCM |
-
Programu ya CCM ya 1987- 2002,
Sura ya 8 -
Mwongozo wa CCM wa 1981 Ibara 44-53 - Makala
ya “Ujenzi wa Chama” iliyotolewa katika Semina za Halmashauri Kuu za Mikoa, Juni 14-
21,2003. |
|
4. Sera za Msingi za CCM |
a)
Azimio la Arusha -Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea -Ujamaa na Maendelea Vijijini -Siasa ni Kilimo -Ushirika -Kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi afanye kazi. |
Kuwaelimisha
wanachama na Viongozi kwamba Ujamaa na Kujitegemea ndio chimbuko la sera za
Msingi za CCM. |
Wanachama
na Viongozi wa CCM. |
Katiba
ya CCM Toleo la Mei 2005 - Azimio
la Arusha - Ilani
ya Uchaguzi 2000- 2005 na 2005-2010. |
|
5. Mwelekeo wa Sera za CCM katika Kipindi husika |
-
Kujenga Msingi wa Uchumi wa Kisasa wa Taifa linalojitegemea. -
Mikakati ya Uwezeshaji wa Kiuchumi wa wananchi katika kupambana na umaskini. - Utawala bora na Madaraka ya wananchi. - Chama
Cha Mapinduzi na umoja wa Kitaifa; Amani na Utulivu na Mapinduzi ya uchumi. -
Vipengele vingine kwa mujibu wa mwelekeo uliopo. |
Kuwaelimisha
wana-CCM na viongozi maudhui ya Mwelekeo wa Sera za CCM katika kipindi
husika, mfano miaka ya 2000-2010. |
Wanachama
na Viongozi wao. |
-
Mwelekeo wa Sera za CCM Katika Miaka ya 2000-2010 ukurasa wa 9-75 na mielekeo mingine ya sera kadri itavyotoka. |
|
6. Utekelezaji wa Ilani za
Uchaguzi
za CCM |
- Maana
ya Ilani -
Mafanikio ya Utekelezaji katika nyanja
za:- - Ustawi
wa Jamii; Elimu na Afya. -
Miundombinu, Huduma za Kiuchumi. Mawasiliano na Uchukuzi: - Uchumi
na Biashara -
Kilimo, Utalii na Madini -
Nishati na Maji - Ulinzi
na Usalama. - Kero
za wananchi |
Kuwaelimisha
wana-CCM na viongozi wao kuhusu Ilani |
Wanachama
na Viongozi wao |
-
Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi katika Halmashauri za Wilaya na Kata/Wadi katika kipindi husika. -
Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM katika kipindi husika. |
|
7. Demokrasia katika Mfumo wa vyama vingi vya siasa. |
-
Umuhimu wa demokrasia katika nchi yetu. -
Kujikosoa na kukosoana. -
Mashindano ya vyama katika kuwania dola. -
Kupingana bila kupigana. |
Kuwaelimisha
wana-CCM na viongozi umuhimu wa kutumia demokrasia |
Wanachama
na Viongozi wa CCM. |
-Tujielimishe -Mwongozo
wa CCM wa 1981, Sehemu ya Pili - Elimu
ya Uraia. |
|
8. Wanachama wa Mstari wa Mbele wa harakati za Mapambano wakati wa
Uchaguzi. |
Majukumu/Nafasi
ya Mwanachama wa CCM/Jumuiya wakati wa Uchaguzi katika:- (a)
Kushiriki kumpata Mgombea Mzuri. (b)
Umuhimu wa kupiga kura – kumchagua mgombea wa CCM. (c)
Kuhamasisha wapenzi wa CCM kutunza shahada kisha kupiga kura kumchagua mgombea wa CCM. (d)
Kushiriki kufanikisha kampeni za CCM. (e)
Kufichua njama/hila za wapinzani. |
Kuwawezesha
wanachama wa CCM na Jumuiya zake kuelewa nafasi na majukumu |
Wanachama
wa CCM na Jumuiya zake. |
1.
Mwongozo wa CCM wa 1981. 2.
Kanuni za Utendaji Kazi Katika Chama Ndani ya Mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa Sura ya 2. |
|
SOMO/MADA |
VIPENGELE |
MADHUMUNI |
WALENGWA |
REJEA |
|
9. Miiko na Maadili
ya Uongozi |
-Maadili ya wanachama na viongozi -Miiko ya uongozi -Uadilifu katika kutafuta uongozi. -Vita dhidi ya rushwa -Vita dhidi ya hulka ya kujilimbikizia |
Kuwaelimisha wanachama na viongozi wa CCM na Serikali zake kuhusu wajibu wao wa kupambana na hulka na vitendo vya kukiuka miiko na maadili |
Wanachama na viongozi wa CCM na Jumuiya zake na wa Serikali zake. |
1. Azimio la Arusha. 2. Mwongozo wa CCM wa 1981. 3. Katiba ya CCM 4. Kanuni za Maadili za CCM |
|
10. Utandawazi |
-Maana ya Utandawazi -Historia ya Utandawazi -Wadau wa Utandawazi -Athari za Utandawazi -Mikakati ya kukabiliana na utandawazi. |
Kuwaelimisha wanachama wa CCM na Jumuiya zake, hali halisi ya mwenendo wa Dunia ya leo – kisiasa, kiuchumi na kijamii. |
- Wanachama wa CCM na Jumuiya zake. |
- Sera za Msingi za CCM |
Umetolewa na Halmashauri Kuu ya
Taifa ya Chama Cha Mapinduzi, Aprili, 2006