Napenda kuwaarifu wanachama wa CCM kwamba
Toleo la Pili la Jarida la Mkereketwa
tayari limekwishatoka na kusambazwa Matawini
nchi nzima. Miongoni mwa mambo yaliyomo katika toleo
(a) Ubinafsishaji
(b) Mapendekezo ya Kamati ya
Msekwa kuhusu Namna Bora ya
Kuwapata Wagombea wa CCM katika
Chaguzi za Dola.
(c) Mapendekezo ya Kamati ya
Kingunge Ngombale-Mwiru kuhusu Uhuishaji wa Muundo
wa Chama.
(d) Wagombea waliopitishwa kugombea nafasi mbali mbali
katika chaguzi za Jumuiya za
Vijana na
Wazazi ngazi za Taifa na
Mkoa.
(e) Mengineyo mengi.
Toleo
Aidha, Toleo
Majarida yote hayo yanaweza
pia kusomwa katika Tovuti ya
CCM: www.ccmtz.org.
Wanachama wanahimizwa kwenda katika Ofisi za
Chama za Matawi, Kata, Majimbo,
Wilaya na
Mikoa zilizo karibu nao ili
wasome na kujadili yaliyomo katika majarida hayo.
Kwa upande mwingine, nawaomba Makatibu wa CCM wa ngazi
mbali mbali wakishirikiana na Makatibu wao wa
Siasa na Uenezi kuandaa mikutano ya wanachama
au Wajumbe wa Halmashauri Kuu au Kamati za Siasa
wa ngazi husika ili kusoma
kwa pamoja na kuyajadili yaliyomo
kwenye majarida hayo.
Katika kipindi cha maadhimisho ya Miaka 40 ya
Muungano, vikundi kadhaa vya muziki
vilijitokeza kutunga nyimbo za maadhimisho
hayo ambazo zilisikika katika vituo mbali mbali
vya redio na televisheni
na pia katika
kumbi za muziki.
Napenda kuvipongeza vikundi vyote vya muziki
vilivyotunga nyimbo hizo na vituo vya redio
na televisheni vilivyozicheza. Kitendo hicho ni cha kizalendo ambacho kinafaa kuendelezwa.
Pamoja na jamii
ya Watanzania kupenda
Naamini nyimbo zile zimewaelimisha
watoto na
vijana wengi kuhusu mambo ya msingi ya Muungano
wetu, elimu ambayo bila ya
hivyo pengine wasingeipata.
Omar R. Mapuri (Mb.),
KATIBU WA
NEC.,