UTEUZI WA WAGOMBEA URAIS -WANACHAMA 5
KUPELEKWA NEC YA 3.5.05
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha
Mapinduzi ilikutana tarehe
2 Mei, 2005,
Miongoni mwa mambo mengine, Kamati Kuu katika kikao hicho,
ilifanya uchujaji wa majina ya wanachama wa CCM walioomba kuteuliwa kuwa
wagombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Katika kutekeleza jukumu
1.
Kuhusu Kiti cha Rais wa Zanzibar
Kamati Kuu iliafiki pendekezo la Kamati Maalum ya
Halmashauri Kuu ya Taifa kwamba lipelekwe jina moja tu la Ndugu Amani
Abeid KARUME kwa kupigiwa kura na
Halmashauri Kuu ya Taifa. Kwa hivyo,
ilimuomba Dr. Mohammed Gharib Bilal, mwanachama mwingine aliyekuwa ameomba
nafasi hiyo kuondoa jina lake. Dr. Bilal
alikubali na akaondoa jina lake. Kamati
Kuu ilimshukuru na kumpongeza Dr. Bilal kwa ujasiri huo wa kukiweka Chama mbele
kuliko utashi wa binafsi.
2.
Kuhusu Kiti cha Rais wa Jamhuri
Kamati Kuu iliamua kupitisha na kupendekeza kwa Halmashauri
Kuu ya Taifa majina matano yafuatayo:-
(1) Dk.
Abdallah Omari KIGODA
(2) Ndugu
Jakaya Mrisho KIKWETE
(3) Prof.
Mark James MWANDOSYA
(4) Dk.
Salim Ahmed SALIM
(5) Ndugu
Frederick Tluway SUMAYE
Wanachama wote hao watapigiwa kura na Halmashauri Kuu ya
Taifa katika kikao chake cha tarehe 03/05/2005 mjini
Omar Ramadhan Mapuri (Mb.),
KATIBU WA NEC
ITIKADI NA UENEZI