MKUTANO MKUU WA NANE WA TAIFA WA CCM NOVEMBA, 2007

Halmashauri Kuu ya
Taifa ya Chama Cha Mapinduzi inawakaribisha Wajumbe wote Mkoani Dodoma kwa
ajili ya kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Nane wa Taifa, utakaofanyika tarehe 3 – 4
Novemba 2007. Mkutano huo utakuwa ni wa
uchaguzi.
Mkutano Mkuu
utafanya kazi ya kuwachagua Viongozi wa Chama, watakaokuwa madarakani kwa
kipindi cha miaka mitano; (2007 – 2012).
Aidha, Mkutano Mkuu utapokea taarifa ya kazi za Chama, kwa kipindi cha
mwaka 2002 hadi 2007 na taarifa za Serikali za utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi
ya CCM ya mwaka 2000 hadi 2005.
Kamati ya Utendaji
ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu imeandaa na kupanga huduma mbali mbali za malazi,
chakula, usafiri, matibabu, burudani na huduma nyinginezo muhimu kwa wajumbe.
Huduma hizo zitapatikana kwa wajumbe kwa muda wote watakapokuwepo hapa mjini
Dodoma, kwa lengo la kufanikisha Mkutano.
Maelezo kamili kuhusu huduma hizo yanapatikana katika kitabu hiki.
Ikiwa utatokea
upungufu au kasoro ya aina yoyote katika kipindi cha mkutano, Wajumbe wanaombwa
wasisite kuwaarifu viongozi wa Kamati zinazohusika, ili waweze kuwahudumia mara
moja.
KIDUMU CHAMA CHA
MAPINDUZI
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
UTARATIBU
WA MAPOKEZI, HUDUMA ZA MAKABRASHA NA VITAMBULISHO
|
Mapokezi Mabasi yote kutoka Mikoani yaende moja kwa moja
Makao Makuu ya CCM Dodoma ambako watawakuta waelekezaji (guides) na
kuwaongoza mahali pa kwenda. Makabrasha ya Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM na Vitambulisho,
vitatolewa na Kamati zinazohusika. Makatibu Wasaidizi/Wahasibu wa CCM wa Mikoa ndio
wenye wajibu wa kuwachukulia Wajumbe wa Mikoa yao Makabrasha na Vitambulisho
vyao. |
Huduma
ya Posho Malipo ya posho na malipo mengine yanayohusu Mkutano Mkuu wa CCM wa
Taifa, yatalipwa na Kamati ya Fedha. Makatibu Wasaidizi/Wahasibu wa CCM wa Mikoa ndio wenye wajibu wa
kufuatilia malipo ya Wajumbe na Waasisi wa Mikoa yao. |
Huduma ya Afya Vituo vya afya vitakavyowahudumia Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Nane wa
Taifa wa CCM, vimeandaliwa katika maeneo yafuatayo: (i)
Makao
Makuu ya CCM (ii)
Ukumbi
wa Kizota (iii)
St.
Gasper |
|
|
|
|
|
|
Ulinzi na Usalama Suala la Ulinzi na Usalama wa Mkutano Mkuu wa Nane wa Taifa wa CCM ni
jukumu la kila Mjumbe na lipo mikononi mwa kila mmoja. Ingawa ulinzi na usalama umeimarishwa katika sehemu zote za malazi,
burudani, eneo la Kizota na Mji wa Dodoma kwa ujumla, Wajumbe wanatahadharishwa
na kushauriwa kutotembea mmoja mmoja, hususan wakati wa usiku. Vitambulisho vitatolewa kwa Wajumbe wote, Wasikilizaji, Waalikwa,
Maafisa, Waandishi wa Habari na Wahudumu.
Hakuna mtu atakayeruhusiwa kuingia ndani ya Ukumbi wa Mkutano bila
kitambulisho. Kwa hiyo, ni muhimu kwa
kila mhusika wakati wote kuwa na kitambulisho chake. |
|
Mpangilio
wa Malazi ya Wajumbe